Taarifa kwa Vyombo vya Habari
Utambuzi wa Urusi kwa Serikali ya Afghanistan: Hatua ya Ziada ya Kuzuia Kuibuka kwa Mfumo wa Kiislamu katika Kanda
(Imetafsiriwa)
Urusi, Alhamisi, ilitangaza kukubali kwake rasmi hati za utambulisho za balozi mpya wa Afghanistan, na hivyo kuwa nchi ya kwanza kutambua serikali ya Taliban.
Ofisi ya habari ya Hizb ut-Tahrir / Wilaya ya Afghanistan inaona kwamba utambuzi huu ni sehemu ya mchakato mpana zaidi, ambao kupitia huo mfumo wa sasa utaunganishwa hatua kwa hatua katika mfumo wa taifa wa kimataifa wa kilimwengu, ambao utawaondoa, baada ya muda, Taliban kutoka lengo kuu la Kiislamu la kuanzisha dini ya Mwenyezi Mungu na kuieneza. Zaidi ya hayo, utambuzi huu unaweza kuibadilisha Afghanistan kuwa uwanja wa mapambano kati ya nguvu za kikanda na kimataifa.
Tangu mabadiliko ya mfumo nchini Afghanistan, Urusi imejitahidi sana kujenga uhusiano thabiti na mamlaka mpya. Mabadiliko haya ya kisiasa yanatokana na wasiwasi wa Urusi kuhusu usalama wa taifa na maslahi yake ya kimkakati katika Asia ya Kati. Moscow ina hofu ya kuongezeka kwa Uislamu wa kisiasa, kurejeshwa kwa Khilafah, na kuunganishwa kwa Umma wa Kiislamu. Urusi inatarajia kutoka kwa mfumo wa sasa wa Afghanistan kukandamiza wapiganaji wa jihadi katika Asia ya Kati. Kwa sababu hii, Rais wake Putin alitangaza waziwazi mnamo Julai 4, 2024: "Taliban bila shaka ni washirika wetu katika kupambana na ugaidi." Kauli hii inafichua wazi mtazamo wa Urusi wa udanganyifu na unyonyaji kwa serikali ya Afghanistan.
Utambuzi, katika enzi yetu ya sasa, ni chombo cha kisiasa cha kisasa kinachotumiwa kuhudumia maslahi ya kitaifa ya nchi zenye nguvu. Ni manufaa ya kisiasa ambayo Urusi imeitoa kwa msingi wa hesabu zake za kimkakati pekee, na inatarajia serikali ya Afghanistan kutafuta na kudumisha manufaa haya kwa kuweka kipaumbele maslahi ya kimwili pekee, na kuacha vigezo vingine vyote, ikiwa ni pamoja na maadili na kanuni za Kiislamu. Kama Rais wa Marekani Donald Trump alivyotarajia kutoka kwa mfumo mpya wa Syria, hofu hizi za pamoja kati ya nchi zisizo za Kiislamu zinaonyesha mkakati wao wa pamoja wa kudhibiti Uislamu wa kisiasa na kuzuia kuibuka kwa mfumo wa Kiislamu katika kanda.
Zaidi ya hayo, hamu ya kupata manufaa haya ya kisiasa kutoka kwa nchi adui kama vile Urusi haitokani na itikadi ya Kiislamu, bali na akili iliyojengwa juu ya ufuasi wa mambo halisi na mwelekeo wa faida. Vile vile, Amanullah Khan alituma ujumbe rasmi kwa Vladimir Lenin, akiomba msaada wa kisiasa kutoka kwa Umoja wa Kisovieti, ambao ulikuwa nchi ya kwanza kutambua utawala wake. Hata hivyo, kihistoria - hata katika utawala wa Vladimir Putin - Urusi bado ni miongoni mwa maadui wakubwa wa Uislamu na Waislamu, na kikwazo kikuu kwa umoja wa Umma wa Kiislamu. Uhalifu wake dhidi ya Waislamu nchini Urusi, Asia ya Kati, Caucasus, Syria, Afghanistan na maeneo mengine hauwezi kukanushwa.
Hakuna shaka kwamba uhusiano wa kidiplomasia, kisiasa na kiuchumi na nchi kafiri lazima uwe kulingana na kile ambacho Uislamu unakubali, na hii ina mifano ya kihistoria. Tangu zama za Nabii Muhammad ﷺ kupitia zama za Makhalifa Warashidi na baada yao, uhusiano wa nje wa Waislamu daima uliendeshwa kulingana na itikadi ya Kiislamu na kanuni ya al-wala' wal-bara' (mapenzi na chuki kwa ajili ya Allah). Sera ya nje ya Khilafah ilitumikia ujumbe wa kueneza Uislamu kupitia da'wa na jihadi ili kupanua wigo wa utawala wa Kiislamu. Mfano wazi wa hili ni kutumwa kwa wajumbe na Nabii ﷺ kwa majumba ya makaisari wakati huo.
Diplomasia katika Uislamu inategemea dhana kama vile kuonyesha dini, al-wala' wal-bara', na kuainisha nchi kama Dar al-Islam au Dar al-Kufr. Dhana hizi hazina nafasi katika mfumo wa taifa wa kilimwengu; kwa kweli, mara nyingi hushughulikiwa kama hatari. Mfumo wa sasa hauwezi kutafuta sera ya kigeni na diplomasia ya Kiislamu isipokuwa kama inalenga kuanzisha mfumo wa kisiasa uliojikita katika Uislamu wenyewe, na sio mfumo uliounganishwa katika mfumo wa kilimwengu. Hii inawezekana tu kwa kurejesha Khilafah, vinginevyo taifa la sasa litazidi kuelekea kwenye upotovu, likiendeshwa na uhalisia wa kisiasa na kuhusika katika mfumo wa kimataifa wa kilimwengu.
Kwa bahati mbaya, hii ndiyo upotevu ule ule wa kisiasa ambao watawala wengine katika nchi za Kiislamu waliingia - na bado wanaingia leo - na kusababisha mikono yao kufungwa na vikwazo vya mfumo wa kimataifa.
﴿WALE WANAOWAFANYA MAKAFIRI KUWA MARAFIKI BADALA YA WAUMINI, JE, WANATAFUTA UMAARUFU KWAO? BASI UMAARUFU WOTE NI WA ALLAH.﴾
Ofisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir katika Wilaya ya Afghanistan