Trump Anataka Kuitega Hamas Katika Mtego wa Mgawanyiko!
Tangu Marekani iliporejea katika uwanja wa Wapalestina kwa nguvu, haswa chini ya uongozi wa Trump, ilionekana wazi kuwa haitafuti suluhu ya mzozo, bali kuunda upya ili kuhudumia mradi wa udhibiti wa taasisi ya Kiyahudi, na kuvunja umoja wa uamuzi wa Wapalestina. Jambo hatari zaidi lililotokana na mchakato huu lilikuwa ni jaribio la kuivuta Hamas katika mtego wa mgawanyiko chini ya anwani nzuri kama vile ujenzi mpya, utulivu, maendeleo ya kiuchumi ... na mengineyo.