
7/8/2025
Abu Wadaha News: Marekani Yaahirisha Mkutano wa Nne* *Hadi Mambo Yatakapoiva Sudan*
*Imeandikwa na Mwalimu Ibrahim Muhammad (Msimamizi)*
Rais wa Marekani Trump alimkabidhi faili la Sudan kwa Massad Boulos, mshauri wake ambaye alikuwa na jukumu kubwa katika kuvutia kura za Waarabu kwa ushindi wa Trump katika kampeni yake ya uchaguzi, na ndiye aliyeitisha mkutano wa Washington, ambao ulifutwa.
Imetangazwa kufutwa kwa mkutano wa kamati ya pande nne kuhusu Sudan, ambao ulikuwa umepangwa kuandaliwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio, pamoja na mawaziri wa mambo ya nje wa Saudi Arabia, Misri na Umoja wa Falme za Kiarabu, Jumatano Julai 30, bila kutaja sababu au tarehe mpya ya mkutano, jambo ambalo lilizua maswali kuhusu sababu za kufutwa, na kusababisha kufadhaika miongoni mwa wanasiasa na wafuatiliaji.
Lengo la mkutano huu lilikuwa kuzindua mazungumzo ya kina ya kisiasa kati ya pande mbili zinazokinzana, kusimamisha uingiliaji wa kigeni, na kusisitiza umoja na uhuru wa Sudan, kulingana na taarifa ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani. Pamoja na kutoa taarifa ya pamoja inayotaka kukomeshwa kwa uhasama, na kuzindua mipango ya kukuza ufikiaji wa misaada inayoitwa ya kibinadamu.
Mfuatiliaji wa matukio nchini Sudan anagundua kuwa Amerika ndiyo inayoshikilia nyuzi zote za mchezo, kwani ndiyo iliyochochea vita kati ya vibaraka wake Burhan na Hemedti kwa lengo la kuondoa ushawishi wa Ulaya, haswa Uingereza, na Amerika ndiyo iliyoanzisha jukwaa la Jeddah kumaliza mzozo, na kuzuia suluhisho mikononi mwake yenyewe bila wengine, na ndiyo iliyoagiza kuongeza muda wa vita, na ndiyo iliyoanzisha jukwaa la Uswizi la kupulizia mchanga machoni, kisha ikatengeneza kile kinachoitwa nne ambazo ziliondoa Uingereza, kisha ikaziakhirisha mara mbili, mambo haya yote yanaonyesha kuwa Amerika ndiyo inayoendesha hali nchini Sudan, ikisogeza faili wakati wowote inapopenda, na kuifunga wakati wowote inapopenda. Shirika la habari la Ufaransa liliripoti kwamba mkutano wa nne uliakhirishwa kutokana na mzozo kati ya Misri (zana ya Amerika) na Umoja wa Falme za Kiarabu (zana ya Uingereza) kuhusu aya iliyopendekezwa na Umoja wa Falme za Kiarabu katika taarifa ya mwisho inayotoa wito wa kuondolewa kwa jeshi na Vikosi vya Msaada wa Haraka, kutoka kwa mustakabali wa mchakato wa kisiasa, jambo ambalo Marekani haipendi kusikia, kwa ajili hiyo Marekani ilichochea vita kati ya vibaraka wake Burhan na Hemedti, na kwa vitendo imeanza kuzingatia vibaraka wake kwa kuanzisha ushawishi wao kila mmoja katika maeneo anayoyadhibiti. Serikali mbili zimeundwa katika nchi moja, kwa wakati mmoja!
Kwanza: Marais wawili wa Baraza la Utawala; Burhan na Hemedti.
Pili: Manaibu wawili wa mabaraza mawili ya utawala; Malik Agar, naibu wa Burhan, na Al-Helou naibu wa Hemedti.
Tatu: Mawaziri wakuu wawili; Kamel Idris akiwa na serikali ya Burhan, na Al-Taayshi akiwa na serikali ya Hemedti.
Nne: Wapo magavana wa majimbo katika serikali hizo mbili walioteuliwa na marais wa mabaraza mawili ya utawala.
Na pia mawaziri, wengine wao wameteuliwa katika serikali hizo mbili, na wengine wanasubiri…
Je, yote hayo hayamaanishi kuanza kivitendo kuligawanya Sudan?!
Kwa ujumla, Amerika inataka kuweka watu wa Sudan mbele ya ukweli usioepukika, ambao ni kuwatambua vibaraka wake, na kisha wakae chini, kupitia uangalizi wa Amerika, kugawanya Sudan; huyu ng'ombe ambaye amechinjwa na watu hao wawili baada ya kuwasha vita visivyo na maana na vichafu ili kujitenga na utawala wa Sudan kwa manufaa ya ushawishi wa Amerika.
Ama kwa harakati zingine za silaha, zinaweza kupata makombo, au mabaki ya mifupa katika uundaji wa serikali hizo mbili, kila mmoja kulingana na nguvu na ushawishi wake.
Mfuatiliaji wa hali nchini Sudan, anagundua kuwa Amerika inachelewesha suluhisho hadi vyombo vya Uingereza vitakapoondolewa kabisa (harakati za Darfur zenye silaha, na watu wake kutoka miongoni mwa raia), ikiwezekana, au kuwatii chini ya udhibiti wa vibaraka wake, na Minawi ameonyesha nia ya kuingia katika maelewano na Vikosi vya Msaada wa Haraka, Rais wa Harakati ya Ukombozi wa Sudan, Mani Arko Minawi, alisema: "Tutaendelea kuwasiliana na jumuiya ya kimataifa na nguvu za kisiasa hadi Vikosi vya Msaada wa Haraka ikiwa tutapata maono mazuri kwao" (Al-Jazeera, 30/7/2025).
Mkutano wa nne umeakhirishwa kama ilivyoakhirishwa mikutano mingine hadi Amerika ijitoe kutawala nchi au ushawishi wake uwe ndio unaoshinda.
Amerika ndio taifa la kwanza duniani, kwa hivyo ina sehemu kubwa katika shida zote zilizopo ulimwenguni, kwani ndiyo inayoibua maeneo ya mvutano katika maeneo yanayowaka, kwani inaunda mizozo, huchochea shida, na huleta mvutano, kisha baada ya hapo inasimamia mizozo hii, na kutafuta suluhisho kwake, inafanya yote hayo kama sehemu ya mkakati wake wa kutawala ulimwengu.
Inasikitisha kwamba Waislamu wanapigana kwa ajili ya maslahi ya makafiri wakoloni. Na ni upuuzi kudhani kwamba suluhisho linatoka kwa maadui hawa, kwa hivyo kuunganisha suala la nchi za Kiislamu na wasio Uislamu, ni kujiua kisiasa. Suluhisho liko mikononi mwetu kwa kuifanya Uislamu pekee kuwa msingi wa kutatua masuala yetu. Hili halipo katika mataifa ya kitaifa kwa sababu ni nchi za kiutendaji zinazofuata amri za mabwana zao. Kuifanya itikadi ya Kiislamu kuwa msingi wa maisha, ndiko kunawakomboa Waislamu kutoka kwa uingiliaji wa makafiri, na hilo halitakuwa isipokuwa chini ya Ukhalifa ulioongoka kwenye njia ya Utume.
* Mwanachama wa ofisi ya habari ya Hizb ut-Tahrir katika jimbo la Sudan
Chanzo: Abu Wadaha News
