
29/7/2025
Abu Wadaha News: Serikali ya Muungano wa Msingi ni Hatua ya Juu katika Kuharakisha Mpango wa Marekani wa Kuitenganisha Darfur, Taarifa kutoka Hizb ut-Tahrir Wilaya ya Sudan
Taarifa kwa Vyombo vya Habari
Serikali ya Muungano wa Msingi ni Hatua ya Juu katika Kuharakisha Mpango wa Marekani wa Kuitenganisha Darfur
Vikosi vya Msaada wa Haraka vilitangaza kupitia muungano wao unaoitwa Muungano wa Msingi wa Sudan "Uanzishwaji", Jumamosi 26/7/2025 BK, uteuzi wa rais na makamu wa rais wa baraza la urais, na waziri mkuu, ambayo inamaanisha kuunda serikali sambamba na mamlaka inayoendeshwa na jeshi kutoka Port Sudan, mashariki mwa nchi.
Muungano huo unaundwa na mashirika ya kijeshi, kisiasa na kiraia, maarufu zaidi ni Vikosi vya Msaada wa Haraka, na Harakati ya Watu - Kaskazini, ambapo mkataba wake wa msingi ulisainiwa Februari iliyopita, katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi.
Daima tumekuwa katika Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Sudan tukifichua mpango wa Amerika, na kuonya watu wa Sudan kwamba vita nchini Sudan vina ajenda ya kikoloni ya kuipasua Sudan, ambayo inaongozwa na kichwa cha uovu, Amerika, kupitia vibaraka wake kutoka kwa viongozi wa jeshi, na viongozi wa Vikosi vya Msaada wa Haraka. Kama vile serikali ya al-Bashir ilivyotenganisha Sudan Kusini, kwa kushirikiana na Harakati ya Watu, iliyoongozwa na marehemu John Garang, ndivyo serikali ya al-Burhan leo na Vikosi vya Msaada wa Haraka wanavyoendelea na suala la Darfur kwa mpango uleule, kupitia uondoaji wa kutiliwa shaka, na kukabidhi kambi za jeshi na miji kwa Vikosi vya Msaada wa Haraka, na kutokupeleka majeshi au ndege kukomesha uasi wao! Huku tukijua kuwa jeshi nchini Sudan lina uwezo wa kukomesha vita, na kukomboa nchi na watu, ikiwa tu hatamu itaachiliwa kutoka kwa anayeishikilia.
Al-Bashir alikiri hapo awali kwamba alipitisha mgawanyo wa Kusini chini ya shinikizo la Amerika, akisema: "Kutengwa kwa Kusini kulikuwa chini ya shinikizo la Amerika, na kwamba mpango wa Amerika ni kuigawanya Sudan katika mataifa matano." (Tovuti ya Sputnik ya Urusi).
Baada ya hapo, kukawa na kukiri kutoka kwa nguzo za utawala wake, na mawaziri wake wa mambo ya nje, ambayo inamaanisha kwamba walikuwa na ufahamu wa mpango huo, na wanautekeleza, na leo hali ileile inajirudia huko Darfur, kwa kupanga kuitenganisha kupitia Vikosi vya Msaada wa Haraka, ambavyo vilisimamiwa na kamanda wa jeshi, al-Burhan.
Inaumiza sana kwamba kichwa cha uovu, Amerika kafiri mkoloni, inaweza kusimamia mapigano ambayo yanavuna roho nchini Sudan, kupitia vibaraka wake; ambao wanatekeleza mpango huo hadharani na sio kwa siri, kwa uwazi na sio kwa kificho, wakisaidiwa na vyombo vya habari vinavyoshirikiana, vinavyopotosha, na wanasiasa mamluki ambao hawana chochote ila viti vilivyochakaa, wanavyokalia, na kafiri mkoloni anavishughulikia.
Kupasua nchi za Waislamu ni uhalifu mkubwa, na kila mtu anayeshiriki ndani yake atabeba dhambi yake, Mtume ﷺ alisema kuhusu Arfaja bin As'ad: «Yeyote anayewajia hali yenu ikiwa imeungana chini ya mtu mmoja, akitaka kuipasua fimbo yenu, au kuwatenganisha kundi lenu, basi muuweni» Ameipokea Muslim. Na Muslim amepokea kutoka kwa Abu Saeed al-Khudri, akisema Mtume ﷺ: «Ikiwa watafanya bai'a kwa makhalifa wawili, basi muuweni yule wa mwisho kati yao», ambayo inasisitiza ulazima wa kuhifadhi umoja wa umma, na kutogawanyika kwake.
Kwa msingi huo, sisi katika Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Sudan, tunawaita watiifu kutoka kwa maafisa wa jeshi, na watu wa nguvu na kinga, kusimamisha uhalifu huu mbaya, na kuizuia Amerika, na mataifa yote ya kikoloni na zana zao, kutekeleza mipango yao mibaya katika nchi yetu, na kuunga mkono mradi mkuu wa umma, kwa kusimamisha Khilafah Rashidah kwa njia ya Utume; kwani ndio njia pekee ya kutoka na ukombozi.
Mtume ﷺ anasema: «…kwani yeyote atakayeishi miongoni mwenu ataona tofauti nyingi, basi shikamaneni na Sunnah zangu na Sunnah za Makhalifa Waongofu Waongozwa, shikamaneni nazo na ziumeni kwa magego».
Jumatatu, 3 Safar 1447 AH
2025/07/28 BK
Ibrahim Othman (Abu Khalil)
Msemaji Rasmi wa Hizb ut-Tahrir katika Wilaya ya Sudan
Chanzo: Abu Wadaha News
