
18-10-2025
Abu Wadaha News: Neno la Msemaji Rasmi wa Hizb ut-Tahrir katika Wilaya ya Sudan katika Mkutano na Wanahabari
Jumamosi 26 Rabi' al-Akhir 1447 Hijria, sawia na 18/10/2025 Miladia
Yenye kichwa: (Mvurugiko wa Serikali katika Jinsi ya Kudhibiti Miamala ya Dhahabu na Athari Yake kwa Thamani ya Pauni)
Baada ya kujitenga kwa Sudan Kusini mwaka 2011, na Sudan kupoteza zaidi ya 75% ya mauzo yake ya mafuta, dhahabu ilijitokeza kama mbadala mkuu wa kulipia hasara hii, na kupata mapato kutokana na fedha za kigeni, na uchimbaji madini ulienea sana nchini Sudan baada ya mwaka 2008 hivi, na uzalishaji wa dhahabu wa Sudan ukawa mkubwa, ambapo ulifikia tani 73.8 mwaka 2024, katika nafasi ya tano barani Afrika (Al Jazeera Net), lakini uzalishaji huu mkubwa haukunufaisha taifa, wala watu, kwani ulikuwa mateka ya watu binafsi, na makampuni ya kigeni na ya ndani, na hata yale yanayotokana na uchimbaji madini wa kiasili, baadhi ya makampuni na taasisi hununua na kuyasafirisha kwa magendo. Ili kuthibitisha tulichosema katika suala hili, tunakagua migodi mikubwa ya dhahabu nchini Sudan, kwa mfano tu, na jinsi serikali inavyoshughulikia migodi hii!
Moja ya migodi hii ni mgodi wa Jebel Amer uliopo kaskazini mwa mji wa El Fasher kwa kilomita zipatazo 100, na uzalishaji wake unakadiriwa kuwa tani 50 kwa mwaka, kulingana na shirika la habari la Reuters, na kuufanya kuwa mgodi wa tatu kwa ukubwa wa dhahabu barani Afrika, lakini serikali haikuweka mkono wake juu yake, bali iliacha kuwa mateka ya makundi yenye silaha, la mwisho likiwa mwaka 2017, ambapo mgodi ukawa mali ya vikosi vya msaada wa haraka, na makampuni ya Kirusi kama vile Wagner.
Licha ya ukweli kwamba kampuni ya Al-Juneid inayomilikiwa na Vikosi vya Msaada wa Haraka ilikuwa imetangaza mwaka 2021, kukabidhi mgodi wa Jebel Amer kwa serikali, lakini katika hali halisi mgodi huo umeendelea kuwa chini ya udhibiti wake hadi leo.
Na mgodi wa Hassai uliopo kaskazini mashariki mwa Sudan, kampuni ya Ariab ya Sudan inamiliki 60% ya hisa ya mgodi huo, na kampuni ya Lamancha Resources inayomilikiwa na mfanyabiashara wa Misri Naguib Sawiris inamiliki 40%.
Na mgodi wa Block 14 uliopo karibu na mpaka wa Misri kaskazini mwa Sudan, na unaitwa mradi wa Maas Sand, na kampuni ya Bear Swiss ya Australia inamiliki 70%, serikali ya Sudan 20%, na 10% kwa kampuni ya ndani ya Sudan iitwayo Maas.
Katika ripoti iliyochapishwa na Al Jazeera Net, dhahabu kutoka mgodi wa Jebel Amer, na zaidi ya migodi mingine 10 kusini mwa Darfur husafirishwa kwa magendo kwenda nchi ya Chad, na karatasi hutolewa kwake kama dhahabu ya Chad na kisha kusafirishwa kwenda Umoja wa Falme za Kiarabu. Mchakato wa usafirishaji wa dhahabu kwa magendo kutoka Sudan ni mchakato unaohusisha watu wenye ushawishi katika serikali tangu enzi ya serikali ya uokoaji, ambapo ilikuwa ikisafirishwa kupitia uwanja wa ndege wa Khartoum, na kupitia bandari za Sudan, na pia kuna makampuni yanayomilikiwa na jeshi, na mengine yanayomilikiwa na idara ya ujasusi, yanaendesha shughuli za uchimbaji madini ya dhahabu, na mapato ya makampuni haya hayaendi kwenye hazina ya serikali.
Baada ya kuzuka kwa vita kati ya jeshi la Sudan, na Vikosi vya Msaada wa Haraka; vita hivi ambavyo vimeangamiza miundombinu mingi ya kiuchumi na mingineyo, ambapo usafirishaji uliokuwa ukiingiza hazina kile kinachoitwa fedha za kigeni (dola) ulisimama, sarafu ya ndani ya Sudan, pauni ya Sudan, ilianza kudhoofika na kuanguka dhidi ya dola ya Marekani, na sarafu nyingine za kigeni, jambo ambalo liliathiri maisha ya watu ambayo kimsingi yamekuwa hayawezekani kuvumilika kutokana na vita, kwa hivyo umaskini na kunyimwa viliongezeka, na magonjwa na njaa vilienea.
Katika jaribio la kusimamisha kuzorota huku, mkutano wa Kamati ya Dharura ya Kiuchumi ulifanyika, ukiongozwa na Waziri Mkuu Kamel Idriss, siku ya Jumatano, Agosti 20, 2025, na kamati hiyo ilitoa maamuzi ya kudhibiti utendaji wa kiuchumi, kulingana na Shirika la Habari la Sudan, na muhimu zaidi ya maamuzi hayo ni:
1- Kuainisha umiliki, au uhifadhi wa dhahabu bila hati, kama uhalifu wa usafirishaji haramu.
2- Kufuatilia mauzo ya nje ili kuepuka usafirishaji haramu wa dhahabu.
3- Kuzuia ununuzi na uuzaji wa dhahabu kutoka kwa taasisi ya serikali.
Na maamuzi mengine, na licha ya ukweli kwamba walisisitiza kuzuia ununuzi na uuzaji wa dhahabu kutoka kwa taasisi ya serikali, walikiuka uamuzi huu, kulikuwa na mkutano ambapo Gavana wa Benki Kuu ya Sudan aliyeondolewa, Burai Al-Siddiq, alisisitiza kwamba Benki Kuu ya Sudan ndiyo iwe taasisi pekee ya kusafirisha dhahabu, na kulikuwa na mzozo mkali uliozuka katika mkutano huu rasmi, uliofanyika katika jengo la wizara huko Port Sudan tarehe 12/10/2025, ambapo Gavana Burai alishikilia uamuzi wa ukiritimba wa usafirishaji wa dhahabu kupitia Benki Kuu, wakati wawakilishi wa makampuni ya usafirishaji wa dhahabu walisisitiza haki yao ya kusafirisha moja kwa moja bila udalali wa Benki Kuu, na Waziri wa Fedha Jibril Ibrahim aliuunga mkono msimamo wa makampuni, hivyo Gavana alitoka kwenye mkutano akiwa amekasirika, na hiyo ilikuwa sababu ya kuondolewa kwake kazi siku iliyofuata, ambapo Al-Burhan alitoa uamuzi wa kumfuta kazi, na kumteua Amina Mirghani; mwanamke wa kwanza kushika wadhifa huu nchini Sudan. Wakati chanzo cha tatizo katika kushughulika kwa serikali na dhahabu bado kipo, nacho ni:
a- Kuweka migodi mikubwa ya dhahabu mikononi mwa makampuni na watu binafsi, badala ya kuchukuliwa na serikali, ambayo hupoteza nchi utajiri wake mwingi na huenda mikononi mwa wachache.
b- Kukosa uwezo wa kudhibiti dhahabu inayochimbwa na kujua kiasi chake.
c- Mizozo katika sera kuelekea dhahabu inayochimbwa, katika suala la kuweka bei ya ununuzi, mnunuzi, na ukiritimba, ambayo imesababisha kuenea kwa jambo la usafirishaji haramu kwenda nje ya nchi, na nchi jirani (Misri, UAE, na Chad).
d- Kukosa kufaidika na uchimbaji madini wa kiasili ambao unasafirishwa kwa magendo, ikijulikana kuwa takriban 70% ya kiasi cha dhahabu kilichozalishwa kilichotangazwa kinatoka kwa uchimbaji madini wa kiasili, ambayo inafichua ukubwa wa usafirishaji haramu unaofanyika katika dhahabu.
Na kwa kuwa suala la dhahabu linahusiana kwa karibu na sarafu, tatizo la kudhoofika kwa thamani ya pauni ya Sudan linaweza kufupishwa katika sababu kadhaa, muhimu zaidi ni:
1- Msingi wa pauni ya Sudan unategemea dola badala ya dhahabu na fedha.
2- Kuchapisha karatasi za pesa bila kufunikwa na dhahabu, au bidhaa, ambayo huongeza kiwango cha mfumuko wa bei ambao husababisha kudhoofika kwa thamani ya pauni.
3- Udhaifu wa mauzo ya nje kutokana na usafirishaji haramu, na ukosefu wa utulivu wa kisiasa, licha ya ukweli kwamba Sudan inamiliki utajiri wa kilimo, mifugo, na madini makubwa, ambayo yangefanya kuwa moja ya nchi tajiri zaidi ulimwenguni.
4- Kutegemea uagizaji wa bidhaa nyingi kama vile ngano, dawa, bidhaa za petroli, na zinginezo, na hii inahitaji dola, ambayo hufanya mahitaji ya dola kuwa ya juu, na hudhoofisha pauni, kwa hivyo watu walipoteza imani na pauni ambayo iliendelea kudhoofika kila siku, jambo ambalo liliwafanya watu, haswa wafanyabiashara, kupendelea kuweka akiba ya dola, au dhahabu, kama njia ya kuhifadhi thamani ya akiba yao, ambayo huongeza bei ya dola, na hupunguza thamani ya sarafu ya ndani.
Hii ndiyo hali halisi kuhusiana na jinsi serikali inavyoshughulika na dhahabu, na pia na sarafu ya ndani; pauni, na mvurugano, na ukosefu wa uwazi wa maono katika jinsi ya kushughulikia, unaonekana kupitia muamala huu.
Sisi katika Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Sudan, kutokana na wajibu wetu kwa umma wetu, tunatoa suluhisho la kimsingi, kuhusiana na mada hii, na hilo linatokana na itikadi ya Kiislamu, kwa hivyo tunasema:
Kwanza: Dhahabu, hasa migodi ambayo uzalishaji wake haukomi; kama vile migodi tuliyotaja tulipozungumzia migodi ya dhahabu nchini Sudan, inachukuliwa kuwa ni mali ya umma, yaani, hairuhusiwi kumilikiwa na makampuni, wala watu binafsi, bali ni haki ya umma wote, na kazi ya serikali ni kusimamia uchimbaji na uuzaji, na mapato yake yawe katika miradi ya umma kwa watu wote, au fedha zigawanywe kwao, na hakuna haki kwa serikali, yaani, hairuhusiwi serikali kushughulikia mali ya umma, kwa kuwatenga watu binafsi na makampuni, si kwa zawadi wala kwa uhusiano, wala kwa vinginevyo, Al-Tirmidhi alisimulia kupitia Abiyad bin Hammal «Kwamba alifika kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ na kumwomba ampe mgodi wa chumvi, naye akamkubalia, alipoondoka mtu mmoja kutoka kwenye mkutano akasema: Unajua umempa nini? Hakika umempa maji tele. Akasema: Basi akamnyang'anya». Na maji tele ni yale yasiyokoma, yaani alimpa mgodi usio koma, kwa sababu chumvi ni madini kama maji tele yasiyokoma, kwa hivyo si haki ya serikali kumiliki sehemu yoyote ya dhahabu kwa makampuni, na inapaswa kukubaliana na makampuni kwa kiasi maalum ambacho makampuni huchimba dhahabu kwa maslahi ya umma na si kwa ajili ya makampuni. Na makampuni hayana haki katika dhahabu inayochimbwa, na kwa hivyo inahakikisha kwamba dhahabu yote inakuwa mikononi mwa serikali, inaitumia kwa maslahi ya umma.
Pili: Asili ya pesa za nchi inapaswa kuwa dhahabu na fedha, kwani Mtume ﷺ alikubali dinari ya Kirumi, na dirhamu ya Kiajemi kama sarafu ya dola ya Kiislamu yenye uzito unaojulikana, hadi dinari ya Kiislamu ilipopigwa kwa uzito wa gramu 4.25, na dirhamu kwa uzito wa gramu 2.975 za fedha, hadi dola ilipotawala baada ya uamuzi wa Rais wa Marekani Nixon kuondoa uhusiano wa dola na dhahabu, baada ya dola kuwa sarafu ambayo ulimwengu wote unategemea karibu, na imekuja katika Ibara ya 167 ya rasimu ya katiba ya dola ya Khilafah iliyoandaliwa na Hizb ut-Tahrir yafuatayo:
(Sarafu za nchi ni dhahabu na fedha zilizopigwa au ambazo hazijapigwa. Na haifai kuwa na sarafu nyingine isipokuwa hizo mbili. Na inajuzu kwa dola kutoa badala ya dhahabu na fedha kitu kingine kwa sharti kwamba iwe na hazina ya dola kile kinacholingana na dhahabu na fedha. Inajuzu kwa dola kutoa shaba au bronzi au karatasi au zinginezo na kuipiga kwa jina lake kama sarafu ikiwa ina kile kinacholingana kabisa na dhahabu na fedha).
Na kwa nini tulibainisha dhahabu na fedha kama msingi; hiyo ni kwa sababu Uislamu ulihusisha dhahabu na fedha na hukumu zisizobadilika; kama vile fidia; dinari 1000 za dhahabu, na kiasi cha kukata mkono katika wizi wa haddi isipokuwa katika robo ya dinari au zaidi, na hukumu zingine ambazo sheria ilihusisha na dhahabu na fedha, kama vile Uislamu ulivyofanya zaka ya pesa kwa dhahabu na fedha, bali miamala yote ya kifedha iliyotajwa katika Uislamu, ni juu ya dhahabu na fedha.
Tatu: Sudan ni nchi ya dhahabu, na itakapofanya msingi wa sarafu yake kuwa dhahabu, sarafu yake itakuwa sarafu yenye nguvu zaidi yenye thamani, kwa sababu ina thamani ya asili ambayo haiathiriwi na kitu kingine chochote, na thamani yake inabaki kuwa thabiti, labda inapungua kidogo au inaongezeka kidogo, lakini kamwe haitakuwa kama kile kinachotokea sasa kwa sarafu ya ndani ya Sudan ya kudhoofika, lau itafaidika na mapato ya dhahabu yaliyopotea, kwa kutumia hukumu ya sheria katika kushughulika na dhahabu, alisema ﷺ: «…NA KATIKA HAZINA KUNA HUMUS»; yaani, dola huchukua migodi yote tele ambayo haikomi, kama vile ina haki katika (humus) kile kinachozalishwa na watu binafsi.
Nne: Ambaye anatumia suluhisho hizi za kimsingi ni dola ya kimisingi inayojitegemea, na sio dola ya kiutendaji kama hali ilivyo katika nchi yetu leo; inayoifuata kafiri mkoloni, ambaye anatafuta kunyakua utajiri, kuwafilisi waja, na kufanya kazi ya kuvunja umoja wake ili kuudhoofisha!! Hii hapa Marekani ambayo ilitenganisha Sudan Kusini ili Sudan isifaidike na mafuta, sasa inatafuta kung'oa Darfur tajiri kwa dhahabu na madini ya thamani.
Enyi watu wa Sudan: Hakuna wokovu kwenu isipokuwa kwa kufanya kazi kwa bidii na Hizb ut-Tahrir ili kusimamisha dola ya Khilafah Rashidah kwa njia ya Utume, ambayo inamridhisha Mola wenu, na kurejesha utukufu wenu, na mnaishi chini yake mnafurahia baraka ambazo Mwenyezi Mungu ameipa nchi yetu.
Na amani iwe juu yenu na rehema za Mwenyezi Mungu na baraka zake.
Ibrahim Othman (Abu Khalil)
Msemaji Rasmi wa Hizb ut-Tahrir
Katika Wilaya ya Sudan
Chanzo: Abu Wadaha News
