
2025-09-09
Abu Wadaha News: Ujumbe kutoka Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Sudan Wakutana na Mkuu wa Baraza la Maulamaa katika Jimbo la Nile Nyeupe
Habari kwa vyombo vya habari
Ujumbe kutoka Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Sudan Wakutana na Mkuu wa Baraza la Maulamaa katika Jimbo la Nile Nyeupe
Siku ya Jumatatu iliyopita, 8/9/2025, katika mji mkuu wa Nile Nyeupe; Mji wa Rabak, ujumbe kutoka Hizb ut-Tahrir/ Jimbo la Sudan, ulikutana na Sheikh Allama Abdullah Al-Nour Toutou, Imamu na Khatibu wa Msikiti Mkuu wa Asalaya, na Mkuu wa Tawi la Nile Nyeupe la Baraza la Maulamaa wa Sudan nyumbani kwake katika kitongoji cha Asalaya. Ujumbe huo ulikuwa chini ya uongozi wa Dkt. Ahmed Mohamed, mwanachama wa Hizb ut-Tahrir, akifuatana na Maprofesa Faisal Madani, Abdul Majeed Othman Abu Hajar, na Al-Zein Abdul Rahman; Wajumbe wa Hizb ut-Tahrir, ambapo mkutano huo ulikuwa sehemu ya kampeni ya Hizb ut-Tahrir ya kuzuia kujitenga kwa Darfur.
Amir wa ujumbe huo, Dkt. Ahmed, alizungumza kuhusu ziara hiyo kuja kama sehemu ya kampeni iliyozinduliwa na chama hicho ili kuzuia kujitenga kwa Darfur, akieleza mpango wa Marekani wa kutaka kuitenga Darfur, kupitia mpango wa mipaka ya damu, kwa kuvunja kilichovunjika tayari, na jinsi mpango huo unavyoelekea kwenye kujitenga kama ilivyotenganishwa kusini, akieleza kuwa muumini haumi kutoka tundu moja mara mbili, hivyo hatutaruhusu Darfur itenganishwe kama kusini ilivyotenganishwa kwa haki ya kujitawala. Amir wa ujumbe huo alisisitiza umuhimu wa umoja wa umma na kwamba ni mojawapo ya masuala muhimu, na kwamba umma hauwezi kusimamisha miradi ya kafiri isipokuwa kwa kusimamisha Khilafa itakayowaunganisha.
Sheikh alifichua na kufafanua, baada ya kukishukuru chama hicho, akisema: Ziara katika suala hili linalohusiana na umma wa Kiislamu na umoja wake, haitoshi kwa saa hizi, na akasema: Magharibi inaufanyia umma vitimbi na kuandaa njama usiku na mchana, na akasema wazi: Ninahitajika kufanya nini haswa? Tukamwambia: Kufanya kazi ya kuwahamasisha watu kushindwa mpango wa kutaka kuitenga Darfur, na kwamba watu wanapaswa kujua kwamba hakuna njia isipokuwa kwa umoja wa umma kwa kusimamisha Khilafa Rashidah.
Sheikh alihitimisha hotuba yake kwa kuwashukuru vijana wa chama hicho, na akasema: Hii ni mara yake ya kwanza kukutana na vijana kutoka Hizb ut-Tahrir katika ziara kwake, ingawa alisoma kuwahusu, na akajisajili ziara katika maonyesho ya kitabu mwaka 2012. Akiahidi kwamba kilichosalia cha umri wake kitakuwa katika kuhudumia mradi wa umoja wa umma, Mungu akipenda, na akasema: "Ahadi ni kwa Mungu".
Ibrahim Othman (Abu Khalil)
Msemaji rasmi wa Hizb ut-Tahrir
Katika jimbo la Sudan
Chanzo: Abu Wadaha News
