
18-10-2025
Abu Wadahah News: Msimamo na Neno la Hizb ut-Tahrir /Wilaya ya Sudan katika Msikiti wa Chuo cha Uhandisi huko Port Sudan
Kama sehemu ya kampeni ya (Feli mpango wa kutenganisha Darfur) iliyoanzishwa na Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Sudan, chama kilifanya msimamo mbele ya Msikiti wa Misri (Chuo cha Uhandisi) katika mji wa Port Sudan, Ijumaa hii, 25 Rabi' al-Thani 1447 Hijria, sawia na 2025/10/17 Miladia, ambapo Sheikh Naser Reda, Mkuu wa Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut-Tahrir katika Wilaya ya Sudan, alihutubia umati wa waumini waliofurika baada ya Sala ya Ijumaa.
Wakati wa hotuba, vijana wa chama walibeba bendera na mabango yaliyoandikwa misemo kama: (Feli mpango wa Amerika wa kutenganisha Darfur - Wachukulieni hatua mawakala na wasaliti, na zuieni kutenganishwa kwa Darfur - Zuieni kujitenga kwa Darfur kabla haijajiunga na Sudan Kusini - Watu wa Fashir wanauawa na vita na njaa, basi himeni kuwaokoa kwa dola ya Khilafa - Serikali ya uanzishwaji sambamba, mpango wa Kimarekani wa kutenganisha Darfur, basi zuieni kuanzishwa kwake - Marekani inaharakisha mpango wake wa kutenganisha eneo la Darfur, na hakuna kinga ila kwa kuifanya suala la umoja wa nchi kuwa suala la hatima), na kauli mbiu zingine ambazo waumini walikuwa wakipiga picha yaliyomo, na kurekodi hotuba iliyotolewa na Ustadh Naser akianza na kauli ya Mwenyezi Mungu: (HII DINI YENU NI DINI MOJA, NA MIMI NDIMI MOLA WENU, BASI NIABUDUNI).
Na kwa kauli ya Mtume, swala na salamu za Mwenyezi Mungu zimshukie, katika hadithi sahihi kutoka kwa Muslim kutoka kwa Arfaja, alisema nilimsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu, swala na salamu zimshukie, akisema (Hakika yatakuwepo mambo na mambo, basi yeyote anayetaka kutenganisha jambo la umma huu wakati wao wote wameungana, basi mpigeni kwa upanga, yeyote yule. Na katika riwaya: basi muuweni).
Akisisitiza juu ya umoja wa umma na umoja wa taasisi yake ya kisiasa, na akionya dhidi ya kitendo chochote kinachotenganisha kundi, na kugawanya dola. Kisha alieleza kuwa sisi katika Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Sudan, tunawaita watu wa nguvu na ulinzi, na tunawasihi watu wa nchi kusimama dhidi ya mipango ya Magharibi kafiri mkoloni, wanaotaka kuigawa nchi yetu, na kuuvunja umoja wake, kwa kufuata kauli yake, swala na salamu zimshukie: (Yeyote atakayekujieni na jambo lenu lote likiwa juu ya mtu mmoja anataka kuuvunja fimbo yenu au kutenganisha kundi lenu, basi muuweni) na kwamba Mwenyezi Mungu anawaita kwa kauli yake: (ENYI MLIO AMINI! MUITIKIENI MWENYEZI MUNGU NA MTUME ANAPOKUITENI KWENYE YALE YANAYOKUHUMISHENI, NA MJUE KWAMBA MWENYEZI MUNGU HUIINGILIA KATI YA MTU NA MOYO WAKE, NA KWAMBA KWAKE YEYE MTAFUNGULIWA), basi itikieni wito wa Mwenyezi Mungu Mtukufu na msingi maisha katika kumtii Mwenyezi Mungu Mtukufu, kwa kusimamisha Khilafa Rashidah juu ya njia ya Utume.
Mwishoni mwa msimamo kulikuwa na takbira na tahalili, na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, Mola wa walimwengu.
Ofisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir katika Wilaya ya Sudan
Chanzo: Abu Wadahah News
