Organization Logo

فلسطين - مكتب

الأرض المباركة (فلسطين)

Tel: 0598819100

info@pal-tahrir.info

www.pal-tahrir.info

Mbele ya macho na masikio ya tawala zilizosaliti Msikiti wa Al-Aqsa unageuzwa kuwa mahali patakatifu kwa Wayahudi!!
Press Release

Mbele ya macho na masikio ya tawala zilizosaliti Msikiti wa Al-Aqsa unageuzwa kuwa mahali patakatifu kwa Wayahudi!!

August 04, 2025
Location

Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Mbele ya macho na masikio ya tawala zilizosaliti

Msikiti wa Al-Aqsa unageuzwa kuwa mahali patakatifu kwa Wayahudi!!

Mbele ya macho na masikio ya watawala wa Waislamu, Wayahudi wanavamia viwanja vya Msikiti wa Al-Aqsa uvamizi baada ya uvamizi, na wa mwisho ulikuwa jana Jumapili, ukiongozwa na adui wa Mungu, Ben Gvir, na idadi ya Wayahudi wenye msimamo mkali katika uvamizi mkubwa zaidi wa Msikiti wa Al-Aqsa.

Mbele ya macho na masikio ya mfalme wa Jordan, Sisi na Erdogan, na watawala wengine, Wayahudi wanaingia kuunajisi Msikiti wa Al-Aqsa katika kumbukumbu ya kile wanachokiita "uharibifu wa Hekalu" na Ben Gvir atangaza kuwa (Israeli itaongeza udhibiti wake juu ya Jerusalem na Mlima wa Hekalu), na atangaza siku ya uharibifu wa hekalu lao linalodaiwa kuwa udhibiti wa Msikiti wa Al-Aqsa kama mahali patakatifu kwa Wayahudi.

Mbele ya macho na masikio ya umma wa Muhammad , tawala zilizosaliti zinatosheka na kulaani baada ya kulaani na matamko hafifu ambayo hayana uzito wala thamani: Ni nini thamani ya maneno yao: "Hakuna mamlaka (kwa Israeli) juu ya Msikiti wa Al-Aqsa"?! Na ni nini maana ya kuitaka Umoja wa Mataifa kuingilia kati kusitisha mashambulizi na kupunguza idadi ya walowezi wanaoingia?! Ingawa suala hilo limepita mashambulizi hadi hatua za kivitendo za kuufanya Msikiti wa Al-Aqsa kuwa sinagogi ambamo ibada zao zinafanyika.

Enyi umma wa Muhammad ﷺ, Enyi umma bora mliotolewa kwa watu:

Watawala hawa vibaraka wamewapa Wayahudi kifuniko cha kuharibu Ukanda, kuwaua watu wake na kuwafanya wawe na njaa, na sasa wanawapa kifuniko cha kuufanya Msikiti wa Al-Aqsa kuwa sinagogi ambamo ibada zao na sala zao zinafanyika. Basi mnafanya nini?

Imekuwa wazi kama jua la adhuhuri, kwamba Msikiti wa Al-Aqsa, Baitul Maqdis na damu ya watu wa ardhi iliyobarikiwa haiathiri isipokuwa wale wanaoamini Mungu na Mtume Wake, na haisukumwi ila na wale wanaotaka Mungu na Mtume Wake na nyumba ya Akhera, na ukombozi wake hautegemei isipokuwa wale ambao wamefanya utumwa kwa Mungu lengo la maisha yao.

Na hakuna aliyebaki ila yule aliyemwamini Mungu Mwenyezi kutoka katika umma huu ili wawe vyombo vya kubomoa viti vya enzi vya usaliti, na mikono ya kujenga jengo la Uislamu:

Vyombo vya kubomoa tawala ambazo hazijui ila kula njama, kusaliti na kutoa matamko ya kulaani, na zimeligawa umma na kuuzuia kuunga mkono Gaza na Msikiti wa Al-Aqsa.

Na vyombo vya ujenzi vinavyojenga jengo la Uislamu, ambamo umma unakusanyika, na majeshi yanasonga mbele kuukomboa Msikiti wa Al-Aqsa na ardhi iliyobarikiwa na kuwasaidia watu wa Gaza, kwa hivyo ukombozi wa Baitul Maqdis unategemea kuondolewa kwa tawala vibaraka ili umma wa Kiislamu uwe na uamuzi wake, na kila wito usio hivyo ni kutupia jivu machoni na kuchelewesha ukombozi na ushindi.

﴿Basi ahadi ya Akhera itakapokuja, ili waziharibu nyuso zenu, na ili waingie msikitini kama walivyoingia mara ya kwanza, na ili waharibu kila walichokishinda kwa uharibifu mkubwa

Ofisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir

Katika Ardhi Iliyobarikiwa Palestina

Official Statement

فلسطين - مكتب

الأرض المباركة (فلسطين)

فلسطين - مكتب

Media Contact

فلسطين - مكتب

Phone: 0598819100

Email: info@pal-tahrir.info

فلسطين - مكتب

Tel: 0598819100 | info@pal-tahrir.info

www.pal-tahrir.info

Reference: PR-01987006-ce58-7e3c-ad26-1e4085385aff