Organization Logo

السودان - مكتب - ناطق

ولاية السودان

الخرطوم شرق- عمارة الوقف الطابق الأرضي -شارع 21 اكتوبر- غرب شارع المك نمر

Tel: 0912240143- 0912377707

spokman_sd@dbzmail.com

www.hizb-ut-tahrir.info

Mvua ni Neema na Rehema, na kwa Kukosa Uangalizi, Imekuwa Janga!
Press Release

Mvua ni Neema na Rehema, na kwa Kukosa Uangalizi, Imekuwa Janga!

August 29, 2025
Location

Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Mvua ni Neema na Rehema, na kwa Kukosa Uangalizi, Imekuwa Janga!

Mvua kubwa na mafuriko yaliyokumba maeneo mengi ya Sudan yalisababisha vifo vya watu 42, majeruhi 31, na uharibifu wa zaidi ya nyumba elfu nne.

Tunamuomba Mwenyezi Mungu, Subhaanahu wa Ta’ala, awaraham na awasamehe ndugu zetu waliofariki kutokana na mvua hizi, na Mwenyezi Mungu awarehemu na awape makazi ya mashahidi. Pia tunamuomba Subhanahu atukuzie katika hukumu yake.

Inasikitisha sana kwamba msimu wa mvua hauji ghafla, bali ni miezi inayojulikana na kurudiwa kila mwaka. La kushangaza zaidi ni kwamba vituo vingi vya hali ya hewa vilionya juu ya mvua kubwa, lakini vyombo vya serikali havijachukua hatua za kuepusha athari zake, ambazo zilikuwa mbaya zaidi katika vijiji vya Jimbo la Mto Nile, Mashariki mwa Sudan, na hata Kordofan, na maeneo mengine. Serikali haina uhusiano wowote na huduma, la sivyo ingewaelekeza maafisa wake kufungua mifereji, kujenga madaraja, kukagua mabonde, kuwahamisha watu na wanyama kwenda maeneo ya juu, na kukagua nyumba za watu na uwezo wao wa kuhimili mvua. Lakini wamejikita katika mambo mengine yasiyo matatizo yao. Kwa hivyo, wameachana kabisa na majukumu yao ya kutunza maslahi yao, isipokuwa kutoa rambirambi kwa familia za wale ambao nyumba zao zimeporomoka juu ya vichwa vyao! Mvua, ambayo kimsingi ni rehema na neema kutoka kwa Mungu, imebadilika na kuwa janga na adhabu!

Wajibu wa utunzaji kwa upande wa serikali ni jukumu ambalo Uislamu umeamua kwa mtawala kuelekea raia. Mtume ﷺ anasema: «.. NA IMAMU ALIYE JUU YA WATU NI MCHUNGAJI NA ATAULIZWA JUU YA UCHUNGAJI WAKE». Mtume ﷺ alionyesha jukumu hili kivitendo alipokuwa mtawala wa Waislamu katika Madina. Anas bin Malik, Mwenyezi Mungu amridhie, alisimulia: «MTUME ﷺ ALIKUWA MWENYE AKHLAKI NZURI ZAIDI, MWENYE KARIMU ZAIDI, NA MWENYE JASIRI ZAIDI. NA SIKU MOJA WATU WA MADINA WALISHTUKA USIKU. WATU WALIKIMBILIA UPANDE WA SAUTI, MTUME ﷺ AKAWAONGOZA WATU KWA SAUTI, AKISEMA HAMTATISHWA, HAMTATISHWA. NAYE ALIKUWA JUU YA FARASI WA ABU TALHA, MWILI MTUPU, HAKUNA TANDIKO JUU YAKE, NA PADA LAKE SHINGONI. AKASEMA NIMEKUTA BAHARI, AU YEYE NI BAHARI» Imepokewa na Bukhari.

Enyi watu wa Sudan: Imewathibitishia bila shaka yoyote kwamba mifumo hii ya vibaraka haitunzi mambo yenu, bali ni janga kwenu, basi iondoeni, na fanyeni kazi ya kumridhisha Mola wenu pamoja na Hizb ut-Tahrir ili kusimamisha dola ya utunzaji; Dola ya Khilafah Rashidah ya pili kwa njia ya Utume, muishi chini yake kwa furaha na heshima.

﴿ENYI MLIO AMINI! MUITIKIENI MWENYEZI MUNGU NA MTUME ANAPOKUITENI KWENYE YALE YANAYO KUHUMISHENI

Ibrahim Othman (Abu Khalil)

Msemaji Rasmi wa Hizb ut-Tahrir

Katika Wilaya ya Sudan

Official Statement

السودان - مكتب - ناطق

ولاية السودان

السودان - مكتب - ناطق

Media Contact

السودان - مكتب - ناطق

Phone: 0912240143- 0912377707

Email: spokman_sd@dbzmail.com

السودان - مكتب - ناطق

الخرطوم شرق- عمارة الوقف الطابق الأرضي -شارع 21 اكتوبر- غرب شارع المك نمر

Tel: 0912240143- 0912377707 | spokman_sd@dbzmail.com

www.hizb-ut-tahrir.info

Reference: PR-0198f2b0-f4a0-7544-b3d2-977352cccee2