Taarifa kwa Vyombo vya Habari
Magonjwa ya Mlipuko Yawaangamiza Watu Katika Kivuli cha Ukosefu wa Taifa la Ustawi
Ugonjwa hatari wa mazingira; kipindupindu, homa ya dengue, na malaria, zinawaangamiza watu huko Khartoum, Al Jazirah, na majimbo ya Darfur, huku kukiwa na uzembe mbaya na ukosefu wa aibu wa serikali, ambayo ilijiita serikali ya matumaini! Tumaini gani hili wakati watu wanaishi katika mazingira ambayo hayafai hata kwa wanyama, mazingira yanayodhibitiwa na wazalishaji wa magonjwa, kutoka kwa mbu wa malaria, mbu wa dengue, na nzi?!
Hakika magonjwa yameingia kila nyumba, na hayajamwacha mtu yeyote, haswa huko Khartoum, ambapo hakuna nyumba ambayo haina wagonjwa wa dengue, na serikali, inayowakilishwa na Wizara ya Afya, haichukui hatua yoyote isipokuwa kuhesabu wagonjwa na wafu, na kwa kufanya hivyo, wanafikiri wanafanya vizuri! Serikali inatumia pesa kwa kile ambacho hakina faida kwa watu, na inafanya kazi ya kupoteza pesa za umma kwa kila kitu isipokuwa afya ya watu wa nchi walioshindwa! Je, gharama na matumizi ya ujumbe uliosafiri kwenda New York kuhudhuria mkutano wa Umoja wa Mataifa, bila faida au wema wowote unaotarajiwa kutoka kwao kwa nchi na watu; haingetosha kunyunyizia Khartoum na maeneo mengine yaliyoathirika, na kuondoa wazalishaji wa magonjwa?! Lakini kwa nini wanafanya hivyo wakati wao ni watesaji waliopewa mamlaka juu ya shingo za watu, na wafanyikazi wanaoinua nambari na takwimu, na kuwaomba mabwana zao katika Shirika la Afya Ulimwenguni na wengine?!
Watu wameacha haki zao, walipowaruhusu wanasiasa kama hao, mawakala wa nchi za kikoloni za kibepari, kunyakua mamlaka yao, na kuwatawala bila mfumo wa Uislamu, na wazo kwamba serikali ndiyo mlezi wa masuala ya raia likatoweka.
Katika mfumo wa Uislamu, Mtume ﷺ alizingatia afya, na akahimiza tiba na matibabu kwa wote, kwa hivyo daktari alipewa yeye na akamfanya kwa umma, na hospitali (hema la matibabu) ilikuwa karibu na Msikiti wa Mtume, na ilisimamiwa na Sahaba mtukufu Rufaida Al-Aslamia, kama vile makhalifa na wakuu walivyoanzisha hospitali katika dola ya Ukhalifa katika enzi zake za kustaajabisha kwa ajili ya kuwatibu wagonjwa, na kutoa matibabu muhimu bure kwa raia bila kujali jinsia yao, dini, au dhehebu, iwe walikuwa matajiri au maskini.
Hakika watu wa Sudan, na ulimwengu, wanahitaji sana leo huduma hii na jukumu ambalo litachukuliwa na dola ya Ukhalifa Rashidun, ambayo ndiyo tumaini la kweli, na mwokozi wa ubinadamu.
Msemaji Rasmi wa Hizb ut-Tahrir
Katika Wilaya ya Sudan