Taarifa za Habari za Tarehe 2025/07/07
Mada Kuu:
- · Watu 80 wameuawa shahidi Gaza huku uhalifu wa mauaji ya kimbari ukiendelea
- · Utawala wa kikoloni unaharakisha mpango wa mauaji ya kimbari huko Gaza kabla ya usitishaji vita unaowezekana
- · Mgogoro wa mafuta unatishia kusimamisha hospitali za eneo hilo
Maelezo:
Watu 80 wameuawa shahidi Gaza huku uhalifu wa mauaji ya kimbari ukiendelea
Wizara ya Afya huko Gaza, ilitangaza Jumapili, kwamba idadi ya wahasiriwa wa mauaji ya kimbari yanayoendelea katika Ukanda wa Gaza imeongezeka hadi mashahidi 57,418 na majeruhi 136,261 tangu Oktoba 2023. Katika ripoti ya kila siku ya takwimu ya idadi ya mashahidi na majeruhi kutokana na uchokozi wa utawala wa kikoloni dhidi ya Ukanda wa Gaza, wizara hiyo ilisema kuwa hospitali za Ukanda wa Gaza zilipokea mashahidi 80 na majeruhi 304 katika saa 24 zilizopita, wakiwemo mashahidi 8 wa misaada, na majeruhi zaidi ya 40. Aidha, jumla ya idadi ya Wapalestina waliopoteza maisha yao walipokuwa wakijaribu kufikia misaada ya kibinadamu imeongezeka hadi mashahidi 751 na majeruhi zaidi ya 4,931, tangu Mei 27 iliyopita, kwa mujibu wa chanzo hicho. Tangu wakati huo na mbali na usimamizi wa Umoja wa Mataifa, utawala wa kikoloni ulianza kutekeleza mpango wa kusambaza misaada ya kibinadamu kupitia kile kinachoitwa Shirika la Kibinadamu la Gaza linaloungwa mkono na Amerika na Shirika la Kiyahudi.
Mbele ya macho na masikio ya watawala wasaliti katika nchi za Waislamu, haswa katika nchi jirani, shirika la Kiyahudi linaendelea na mauaji yake na umwagaji damu siku baada ya siku. Watawala hawa, badala ya kuhamasisha majeshi yao makubwa, hawayatumii isipokuwa kulinda viti vyao vya enzi, kuwanyanyasa Waislamu, na kutumikia nguvu za ukoloni. Mara tu wanapokaa kimya, shirika la Kiyahudi huendelea na makosa yake na ukatili, na kuwa katili zaidi katika mauaji yake. Lau majeshi yao yangehamasishwa, shirika hili lisingekuwa na athari yoyote. Na jambo baya zaidi ni kwamba, badala ya kukusanya majeshi, wanashirikiana na shirika kulilinda, kulihuisha na kutoa sababu za maisha kwalo. Kwa hivyo, ikiwa Waislamu wanataka kuondoa kabisa shirika hili, hawana budi kuondoa watawala hawa kwanza, kwani shirika hili sio chochote ila kivuli cha watawala hawa, na asili itakapotoweka, kivuli kitatoweka bila shaka.
----------
Utawala wa kikoloni unaharakisha mpango wa mauaji ya kimbari huko Gaza kabla ya usitishaji vita unaowezekana
Utawala wa kikoloni unakimbizana na wakati ili kukamilisha operesheni ya "Magari ya Gideon" kwa lengo la kuondoa watu kutoka kaskazini mwa Ukanda wa Gaza na kupanua eneo la buffer, kabla ya kufikia makubaliano yanayowezekana ya kusitisha mapigano ya muda ambayo yanaweza kuzuia mauaji yake yanayoendelea tangu Oktoba 7, 2023 ndani ya vita vya mauaji ya kimbari. Kwa mujibu wa Shirika la Anadolu, kutoka kwa chanzo kilicho karibu na makundi ya Kipalestina, ambacho kilipendelea kutotajwa, "Israel inajaribu kutumia siku chache zilizosalia kabla ya utulivu wowote unaotarajiwa, kupanua eneo la uharibifu na mauaji ya miji, hasa kaskazini na mashariki mwa jimbo la kaskazini, na mashariki mwa mji wa Gaza, na mashariki mwa Khan Yunis kusini mwa ukanda huo." Aliongeza kuwa "Israel inataka kuharibu kile kilichosalia cha misingi ya maisha katika maeneo hayo, ili kumaliza fursa yoyote ya Wapalestina kurudi huko kama ilivyofanya katika kambi ya Jabalia", ambayo iliharibu karibu kabisa katika nusu ya pili ya 2024.
Inasikitisha sana na kuumiza kwamba shirika la wavamizi wa ardhi yetu linatuondoa sisi ambao tunapaswa kuwa wale wanaomwondoa, badala yake kumng'oa na kumtupa mbali. Lakini ole, kwa sababu ya watawala wasaliti, tumekuwa sisi tuliotimuliwa na kufukuzwa kutoka makwao! Sababu kubwa ya hali yetu hii iko katika watawala wasaliti. Mradi watawala hawa wamekaa juu ya vifua vyetu, uhamaji wetu, mauaji yetu, na umwagaji damu yetu utaendelea.
-----------
Mgogoro wa mafuta unatishia kusimamisha hospitali za eneo hilo
Wizara ya Afya huko Gaza ilionya, Jumamosi, juu ya kusimamishwa kwa kazi ya idara zinazookoa maisha katika hospitali za ukanda huo kutokana na mgogoro wa mafuta unaohitajika kuendesha jenereta za umeme, ikisisitiza kuwa mgogoro huo unaendelea ndani ya viashiria visivyo na kifani kutokana na kuendelea kufungwa kwa vivuko na utawala wa kikoloni tangu Machi iliyopita. Wizara hiyo ilisema katika taarifa kwamba "mgogoro wa uhaba wa mafuta unaohitajika kuendesha jenereta za umeme katika hospitali bado haujatatuliwa ndani ya viashiria visivyo na kifani." Ilisisitiza kwamba "shinikizo linaloongezeka kutoka kwa majeruhi mahututi wanaofika hospitalini, linaongeza hitaji la kuhakikisha uendeshaji unaoendelea wa jenereta za umeme kuendesha idara muhimu." Ilisema kuwa hiyo inakuja katika "muktadha wa sera ya udhibiti ambayo shirika la Kiyahudi linakusudia kufuata katika kuruhusu uingizaji wa kiwango cha mafuta ambacho hakitoi muda wa ziada kwa uendeshaji wa hospitali."
Shirika la Kiyahudi, likiungwa mkono na Marekani, limekuwa likifanya mauaji ya kimbari katika Ukanda wa Gaza tangu Oktoba 7, 2023, na kuacha takriban Wapalestina 193,000 kati ya waliouawa shahidi na waliojeruhiwa, wengi wao wakiwa watoto na wanawake, na zaidi ya watu 10,000 hawajulikani walipo, pamoja na mamia ya maelfu ya wakimbizi na njaa ambayo imepoteza maisha ya wengi, wakiwemo watoto kadhaa. Angalieni hali ambayo umma huu umefikia, je, kazi yake ni kuhesabu tu mashahidi wake? Umma ambao uliongoza mataifa mengine kwa karne nyingi, na ulikuwa kimbilio kwa wale wanaotafuta hifadhi, na msaada kwa wale wanaoomba msaada, leo uko katika nafasi ya yule anayeomba msaada na hifadhi! Ikiwa kengele za hatari zinalia leo huko Gaza, sababu ya hii ni watawala wasaliti. Wakati watawala hawa wanaishi katika anasa na ubadhirifu, watu huko Gaza wanajitahidi kuishi na wanapambana na mauti. Wanahitaji kile Wayahudi wanagawanya au kuruhusu kugawanywa. Laana iwe juu ya watawala hao ambao wameishusha umma kwenye kiwango ambacho hawana chochote ila kuhesabu waliouawa wao.

