Habari Muhimu 2025/10/13
Mada kuu:
- · Nchi 6 za Kiarabu zimeongeza ushirikiano wa kijeshi kwa siri na taasisi ya Kiyahudi wakati wa vita vyake dhidi ya Gaza
- · Mkutano wa Sharm el-Sheikh: Misri kuwa mwenyeji wa viongozi wa dunia kumaliza vita vya Gaza
- · Afghanistan inazishutumu kundi fulani huko Pakistan kwa kuharibu uhusiano kati ya nchi hizo mbili
Maelezo:
Nchi 6 za Kiarabu zimeongeza ushirikiano wa kijeshi kwa siri na taasisi ya Kiyahudi wakati wa vita vyake dhidi ya Gaza
Gazeti la Washington Post lilibaini kuwa nchi sita za Kiarabu ambazo ni (Jordan, Saudi Arabia, Misri, Bahrain, Falme za Kiarabu, na Qatar) zimepanua ushirikiano wao wa kijeshi na uvamizi huo katika miaka mitatu iliyopita, likinukuu vyanzo vyenye ufahamu. Gazeti hilo lilisema kwamba licha ya kulaani vikali taasisi ya Kiyahudi hadharani kutoka nchi za Kiarabu wakati wa vita vya Gaza, nyingi zao zimehifadhi kwa siri ushirikiano wa karibu wa kijeshi, ujasusi nayo. Kulingana na hati za Kimarekani zilizovuja ambazo gazeti na Shirikisho la Kimataifa la Waandishi wa Habari za Upelelezi zilipata, angalau nchi sita za Kiarabu zilishiriki katika mfumo wa siri wa kikanda wa ulinzi unaojulikana kama "ujenzi wa usalama wa kikanda." Kuwait na Oman zimeorodheshwa kama washirika watarajiwa wa baadaye. Gazeti hilo lilisema kuwa utaratibu huo, ulioanzishwa kwa uratibu na Kamandi Kuu ya Marekani (CENTCOM), ulifanya kazi kama mtandao wa siri wa kubadilishana habari, mafunzo ya pamoja na uratibu wa kiutendaji kwa lengo la kukabiliana na ushawishi wa kikanda wa Iran na kuimarisha uhusiano wa kijeshi na taasisi ya Kiyahudi.
Kufichuliwa kwa jambo hili ni matokeo tu. Waislamu, haswa wale wenye ufahamu, na hata watu wa kawaida katika nchi hizo, walikuwa wanajua kabisa kuwa mifumo yao inashirikiana na taasisi ya Kiyahudi ambayo inafanya vita vya ukomeshaji wa uzao ambavyo ni mbaya zaidi katika enzi hii dhidi ya Gaza. Kilichofanywa ni kwamba wamegeuza ushirikiano wao wa wazi kabla ya ukomeshaji wa uzao kuwa ushirikiano wa siri wakati wake. Wamehamisha uratibu na uhusiano wao kutoka hadharani kwenda kwa siri, si kwa chochote ila kuhofia usukani wao kuanguka na watu wao kuwaasi. Hata hivyo, ushirikiano huu haujasimama kwa dakika moja. Badala yake, wamefikia hatua ya kuipatia taasisi ya Kiyahudi wahalifu kila njia ya uzima ambayo inahakikisha kwamba inabakia na inaendelea na uhalifu wake. Kwa hivyo, haishangazi kwamba gazeti la Kimarekani linafichua jambo hili sasa. Ukweli kwamba watawala wa Waislamu ni watumwa wanyenyekevu kwa Marekani ni wazi kama jua la utosi. Hawathubutu kuasi, bali hutekeleza kile inachoamuru. Je, Marekani ingeweza kutekeleza mpango wa usaliti wa Trump bila wao? Marekani inalazimisha utawala wake juu ya nchi zetu kupitia wao.
-----------
Mkutano wa Sharm el-Sheikh: Misri kuwa mwenyeji wa viongozi wa dunia kumaliza vita vya Gaza
Misri itakuwa mwenyeji wa mkutano wa kimataifa huko Sharm el-Sheikh, Jumatatu, kwa ushiriki wa zaidi ya viongozi 20 wa ulimwengu, kwa lengo la kukamilisha makubaliano ya kina ya kumaliza vita katika Ukanda wa Gaza. Mkutano huo unakuja kwa mwaliko wa Misri na Amerika, ambayo inatafuta kuzindua awamu inayofuata ya mpango wake wa amani, ambayo ni pamoja na kufikia makubaliano ya mwisho ya kusitisha mapigano, na kuweka mipango ya baada ya vita katika ukanda huo, haswa kuhusiana na utawala, usalama, na ujenzi mpya. Rais wa Marekani Donald Trump anatarajiwa kuwasili Misri mchana wa Jumatatu baada ya ziara ya taasisi ya Kiyahudi, ambapo atatoa hotuba mbele ya Knesset na kukutana na familia za wafungwa wa Kiyahudi ambao Hamas itawaachilia, kabla ya kushiriki katika sherehe rasmi ya kusaini makubaliano ya kusitisha mapigano, akiandamana na Rais wa Misri Sisi na idadi ya viongozi wa nchi zinazodhamini makubaliano hayo.
Ni mchezo wa kuigiza wazi, ulioongozwa na Marekani na kuamuru Misri kuupanga! Huu si mkutano, bali ni sherehe ya kupiga magoti miguuni mwa Trump, mnyongaji mkuu na msaidizi wa kwanza wa taasisi ya Kiyahudi. Hawatkutana kushauriana, bali watasimama katika safu moja kama watumwa kumsifu bwana wao na kumpa ishara za shukrani kwa kusimamisha vita, vita ambavyo aliviunga mkono mwenyewe! Wanataka kwa mkusanyiko huu wa aibu kuhalalisha mpango wa usaliti na kuupitisha kwa umma. Na bwana wao awapapase mabegani na kuwapongeza kwa kufanikiwa kwao katika kusimamia mauaji ya halaiki ya enzi! Mkutano huu unaodaiwa si chochote ila ni mbio za watumwa kuthibitisha nani mwaminifu na mnyenyekevu zaidi kwa Marekani.
------------
Afghanistan inazishutumu kundi fulani huko Pakistan kwa kuharibu uhusiano kati ya nchi hizo mbili
Waziri wa Mambo ya Nje Kaimu katika serikali ya Afghanistan Amir Khan Muttaqi ameyashutumu makundi nchini Pakistan kwa kujaribu kudhoofisha uhusiano kati ya nchi hizo mbili. Muttaqi alisema wakati wa ziara rasmi nchini India, ambayo ni ya kwanza ya aina yake tangu 2021, kwamba serikali yake haina matatizo yoyote na watu wa Pakistani au na wanasiasa nchini Pakistan. Alisisitiza kuwa baadhi ya makundi maalum nchini Pakistan yanajaribu kudhoofisha uthabiti, akieleza kuwa hakuna harakati ya Taliban ya Pakistan ndani ya ardhi ya Afghanistan, na kwamba vipengele ambavyo Islamabad inaona kama tishio kwake ni watu waliokimbia makazi yao ambao walitoka ndani ya Pakistan yenyewe. Alisema kuwa Afghanistan inalinda mipaka yake, anga yake na haki zake za uhuru, na kwamba itajibu ukiukaji wowote itakaofanyiwa. Kwa upande wake, msemaji wa serikali ya Taliban alisema kuwa taarifa za kuaminika zinathibitisha kwamba kiongozi wa shirika la Dola katika jimbo la Khorasan, Shihab al-Muhajir, na wasaidizi wake wa karibu Abdul Hakim Tawhidi, Sultan Aziz Azzam, na Salah al-Din Rajab (wanaohusishwa na uongozi mkuu wa shirika la Dola) kwa sasa wanajificha ndani ya ardhi ya Pakistan.
Ajabu iliyoje! Ndugu wanapigania nini? Na damu yao inamwagwa kwa faida ya nani na roho zao zinatolewa? Na wanashindania mipaka gani ya kishetani? Hii ni mipaka ya aibu iliyochorwa na Sykes na Picot, mipaka ambayo dini yetu au taifa letu haitambui. Kuhusu watawala wa Pakistani, jambo lao limefichuliwa, hawana chochote ila vibaraka mikononi mwa Amerika. Lakini msiba mkubwa ni Afghanistan, ambayo inajigamba kuwa ni emirate ya Kiislamu! Tunawauliza: Je, vita hivi vinaamriwa na Uislamu au na Washington? Ikiwa mlikuwa emirate ya Kiislamu kama mnavyodai, mngepaswa kukanyaga mipaka hii ya ukafiri kwa miguu yenu, na kuandaa majeshi ili kung'oa mizizi ya watawala wasaliti vibaraka, na kuunganisha taifa na kuunganisha nchi za Waislamu chini ya bendera moja. Fahamuni kwamba kumwaga damu ya Mwislamu ili kulinda mstari uliowekwa na mkoloni kafiri ni mojawapo ya madhambi makubwa zaidi mbele ya Mungu, na uhalifu usiosameheka! Mchezo wa Marekani uko wazi: kuchochea mzozo kati ya Pakistan na Afghanistan ili kuizamisha Pakistan katika dimbwi la jirani yake, na lengo halisi la haya yote ni kwamba India ijitolee kwa kazi yake ya msingi, ambayo ni kukabiliana na China. Hiyo ndiyo yote iliyopo, vita mnayoiona kati ya Pakistan na Afghanistan si chochote ila ni tukio katika mchezo huu wa Marekani.

