Taarifa kwa Vyombo vya Habari
Miradi ya Kiyahudi ya Marekani ni miradi ya uhalifu ya usaliti
Iwe imetekelezwa na Shirika la Ukombozi au wengineo
Kituo cha tano cha Waebrania kilitangaza, kama ilivyoripotiwa na Al Jazeera, habari kwamba Netanyahu anafanya mkutano kujadili kubadilisha wakuu wa koo na viongozi wa Mamlaka ya Palestina huko Hebron, na taarifa ilitolewa na Mkoa wa Hebron (kujibu mashauriano ya serikali ya uvamizi kuhusu kutenganisha Hebron na jiografia ya kitaifa na kuiwakilisha kwa utawala wa koo).
Kwa hivyo, sisi katika Ofisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir katika Ardhi Takatifu ya Palestina tunaeleza na kusisitiza yafuatayo:
1- Mamlaka ya Palestina ilikuja chini ya udhamini wa Amerika na kwa idhini ya chombo cha Kiyahudi ndani ya mradi wa kisiasa ambao unategemea kuachia ardhi takatifu kwa chombo cha Kiyahudi, na kutekeleza mahitaji ya usalama kwa faida yake. Imetekeleza jukumu hili la usaliti kikamilifu, na rais wake alijivunia hili katika mikutano ya kilele ya Kiarabu na kwenye jukwaa la Umoja wa Mataifa. Ikiwa Amerika na Wayahudi wataona ni muhimu kubadilisha baadhi ya watu wa Mamlaka au kukomesha Mamlaka ya Oslo na kuanzisha mamlaka mpya chini ya jina lolote, itakuwa ni muendelezo wa mradi wao wa kusuluhisha suala la Palestina, iwe kupitia Shirika la Ukombozi au kupitia chama kingine chochote wanachokianzisha. Amerika na Wayahudi walipoamua kumaliza Yasser Arafat na idadi ya watu wanaomuunga mkono, walikuja na Mahmoud Abbas na kikundi kilichofanya kazi chini ya usimamizi na usaidizi wa Jenerali wa Marekani Dayton. Mamlaka haikuwa chochote ila mkono wa usalama kwa chombo cha Kiyahudi, na ikiwa chombo hicho kitasitisha huduma zake, haitakuwa kwa heshima ambayo Mamlaka inabeba, lakini kwa sababu itakuwa imekamilisha kile inachotaka kutoka kwake na kisha kuitupa mahali ambapo wasaliti hutupwa baada ya kumaliza kazi yao. Chama ambacho uvamizi utakuja nacho kitakuwa tu cha aina ya Mamlaka, na haitakuwa chochote ila mkono wa usalama kwa Wayahudi.
2- Watu wa Palestina hawakuchagua Shirika la Ukombozi, lakini liliwekwa juu yao kwa lazima ili kuachia sehemu kubwa ya Palestina kwa Wayahudi, na kuliwakilisha kama mwakilishi pekee na halali wa watu wa Palestina ni kutukuza jukumu lake la usaliti ambalo halikubaliki kwa yeyote anayemwamini Mungu na Siku ya Mwisho. Jaribio lolote linalofanywa na Mamlaka kupata utambuzi kutoka kwa watu wa Palestina wa uhalali wake ni jaribio la kubeba mzigo wake na dhambi zake kwa watu wa Palestina, ambao hawahusiki nazo.
3- Chama chochote kinachofanya kazi na uvamizi, bila kujali jina lake, ni sehemu ya uvamizi, na chombo kati ya vyombo vyake. Kupamba majina kwa jina lolote hakumfanyi msaliti ila kuwa msaliti, na hakumtoi mshirika na uvamizi kutoka kwa unyanyapaa wa aibu na fedheha katika ulimwengu huu na Akhera. Ufuatiliaji wowote, iwe wa shirika na mamlaka yake au chama kingine chochote kilichoanzishwa na uvamizi, utabeba hatia na dhambi yake mbele ya Mungu kwa yeyote anayeridhika na kufuata, sio yule anayekataa na kuokolewa. Yeyote anayetangaza msimamo wowote unaounga mkono Shirika, Mamlaka, au chama chochote kilichoanzishwa na uvamizi, basi amejipeleka kwenye safu ya wasaliti na haamwakilishi watu wake au ukoo wake, hata akidai hivyo.
Mwisho: Tunawaita watu wa Palestina kwa ujumla, na watu wa Hebron na familia zao haswa, kwa wito wa Mungu Mwenyezi: ﴿Enyi mlio amini! Msimfanyie hiana Mwenyezi Mungu na Mtume, wala msizifanyie hiana amana zenu, nanyi mnajua﴾, na tunawaonya dhidi ya kudanganywa na Mamlaka kwa kutangaza misimamo ya kuunga mkono au Shirika au chama kingine chochote kilichoanzishwa na Amerika na Wayahudi. Uzembe haumuondoi mtu hatia, na kuridhika hakumaanishi ila kuwafuata wasaliti katika usaliti wao.
Suala la Palestina haliwakilishwi na shirika, wala halimilikiwi na ukoo, bali ni suala la taifa zima, na watu wa Palestina hawana haki zaidi kuliko Waislamu wengine ndani yake, na mfano wake ni wajibu kwake. Ni suala la dini na itikadi, na suala la ardhi iliyobarikiwa, ambayo haitatuliwi na dola dhaifu kati ya makucha ya uvamizi, bali inaachiliwa huru na mikono ya waumini waaminifu kutoka kwa umma wa Muhammad ﷺ, ili irudi kama ilivyokuwa, ua na mnara wa Sham, na kuwa kitovu cha nyumba ya Uislamu kama alivyobashiri Mtume ﷺ. ﴿Nao wanasema: Ushindi huu utakuwa lini ikiwa mnasema kweli? Sema: Siku ya Ushindi haitawafaa walio kufuru kuamini kwao, wala hawatapewa muhula. Basi wajitenge nao, na ungojee; hakika hao wana ngojea﴾.
Ofisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir katika Ardhi Takatifu ya Palestina