Organization Logo

الأردن المكتب الاعلامي

ولاية الأردن

Tel:

info@hizb-jordan.org

http://www.hizb-jordan.org/

Mfumo wa Jordan unatetea taasisi ya Kiyahudi adui kwa kuzuia makombora na ndege zisizo na rubani zilizoelekezwa kwake
Press Release

Mfumo wa Jordan unatetea taasisi ya Kiyahudi adui kwa kuzuia makombora na ndege zisizo na rubani zilizoelekezwa kwake

June 14, 2025
Location

Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Mfumo wa Jordan unatetea taasisi ya Kiyahudi adui

kwa kuzuia makombora na ndege zisizo na rubani zilizoelekezwa kwake

Taasisi ya Kiyahudi ilizindua shambulio dhidi ya Iran alfajiri ya Ijumaa, Juni 13, 2025, ikilenga mitambo yake ya nyuklia, viwanda vya makombora ya balistiki, na viongozi wa kijeshi, na kusababisha uharibifu mkubwa kwa maisha na mitambo ya kijeshi na raia, kwa msaada na ushirikiano wa Amerika. Iran iliahidi, kama kawaida, majibu madhubuti na ya uharibifu kwa taasisi ya Kiyahudi kupitia shambulio na ndege zisizo na rubani na makombora na ilifanya mawimbi ya mashambulio haya asubuhi na jioni ya siku hiyo hiyo, ikivuka anga ya Iraqi, Syria na Jordan, baadhi yake ikisababisha uharibifu katika baadhi ya mitambo katika miji ya taasisi hiyo kabla ya baadhi yake kuzuiwa katika anga inayozunguka kabla na baada ya kufika katika taasisi ya Kiyahudi.

Katika muktadha huu, mkuu wa mfumo alisema kuwa Jordan haitakuwa uwanja wa vita kwa mzozo wowote, na haitaruhusu usalama na utulivu wake kutishiwa. Waziri wa Mambo ya Nje Al-Safadi alisema kuwa Jordan haitaruhusu ukiukwaji wa mamlaka yake na kutishia usalama wake. Chanzo cha kijeshi chenye mamlaka katika kamandi kuu ya vikosi vya jeshi la Jordan - jeshi la Kiarabu, kilisisitiza kwamba ndege za jeshi la anga la kifalme na mifumo ya ulinzi wa anga ilizuia idadi ya makombora na ndege zisizo na rubani zilizoingia katika anga ya Jordan asubuhi ya Ijumaa, ikimaanisha zile zinazotoka Iran kuelekea taasisi ya Kiyahudi.

Kwa hatua hizi, mfumo unathibitisha kile kinachojulikana tangu kuanzishwa kwake kwamba kazi yake ya kisiasa na kijeshi ni kulinda na kuwezesha taasisi ya Kiyahudi, kutoka kwa hatari ambazo zinaweza kutishia uwepo wake, na rekodi yake iliyovunjika katika kutoa maelezo ya kuzuia kwake ndege zisizo na rubani na makombora haya - kwamba ni kulinda usalama, utulivu na raia wake - haimshawishi mtu yeyote kutoka kwa watu wa Jordan, na imekuwa ikifanya kazi bila aibu kutoka kwa Mungu, Mtume wake, au jamii ya Waislamu, katika kutetea taasisi ya Kiyahudi kupitia mikataba, makubaliano na ushirikiano wa kiusalama na kijeshi ambao haujasimama hata wakati wa vita vya mauaji ya kimbari, uhamishaji na njaa kwa watu wa Gaza ambao haukushindwa na vikosi vyake vya jeshi ambavyo vinailinda taasisi ya Kiyahudi kutokana na makombora yanayoishambulia, kwa hivyo Mwenyezi Mungu anawaonya watawala kama hao akisema: ﴿Enyi mlio amini! Msiwafanye Mayahudi na Wakristo kuwa marafiki. Wao ni marafiki wao kwa wao. Na miongoni mwenu mwenye kufanya urafiki nao, basi huyo ni miongoni mwao. Hakika Mwenyezi Mungu hawaongoi watu madhaalimu﴾.

Iwe mfumo unataka au la, Mayahudi na taasisi yao ndio adui wa kwanza wa Mungu, Mtume wake, na watu wa Jordan. Unaweza kuona furaha ambayo inajaza mioyo ya watu wanapoona makombora yanaelekea kuelekea taasisi ya Kiyahudi, na jinsi matumaini yao yanavyokatishwa tamaa yanapozuiwa na kuanguka kabla ya kufika ﴿Hakika utawakuta walio wakali zaidi kwa uadui kwa walio amini ni Mayahudi﴾. Pia, Amerika, ambayo watu wa Jordan wanachukulia kama adui, ndio inayoipa taasisi hii vifaa na silaha, kwa hivyo yeye ni adui wa Uislamu na Waislamu, na yeye ndiye aliyeharibu Iraq, Afghanistan, Syria, Yemen na Sudan moja kwa moja au kupitia mawakala wake. Mfumo na uzingatie kukimbilia kufikia maslahi yake na kuwalinda Mayahudi, kwani hawana rafiki isipokuwa maslahi yao.

Enyi Waislamu, enyi majeshi ya Waislamu: Wakati umefika wa kuitikia wito wa Mungu na ahadi yake ya kuwawezesha mnapojibu amri zake za kuanzisha dola yenu ya Kiislamu na kutekeleza sheria zake, na wakati umefika wa kujitenga na watawala wenu ambao harufu ya usaliti wao inazidi pua, kwa hivyo tunawakaribisha kwenye utawala wa Kiislamu na dola yake ambayo kwayo ni heshima yenu na utu wenu na kwayo ni ushindi wenu dhidi ya taasisi ya Kiyahudi na kufukuzwa kwa Amerika na Ulaya kutoka nchi za Waislamu. Enyi watu wa nguvu na ulinzi, ikiwa mmechukua hatua ya kutowaunga mkono watu wa Gaza na mmeenda kinyume na amri za Mungu, vipi mnaridhika kutetea taasisi ya Kiyahudi kwa vikosi vyenu kuzuia makombora yaliyoelekezwa kwake, hata kusababisha madhara madogo ndani yake?! Tembeeni kuelekea Palestina mkiukomboa Msikiti wa Al-Aqsa na Palestina iliyobarikiwa.

﴿Mwenyezi Mungu amewaahidi wale walio amini miongoni mwenu na wakatenda mema kwamba atawafanya makhalifa katika ardhi kama aliowafanya makhalifa wale walio kuwa kabla yao, na kwa yakini atawathibitishia Dini yao aliyo wapendelea, na atawabadilishia amani baada ya khofu yao. Waniabudu Mimi, wala wasinishirikishe na chochote. Na watakao kufuru baada ya haya, basi hao ndio wapotovu

Ofisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir katika Wilaya ya Jordan

Official Statement

الأردن المكتب الاعلامي

ولاية الأردن

الأردن المكتب الاعلامي

Media Contact

الأردن المكتب الاعلامي

Phone:

Email: info@hizb-jordan.org

الأردن المكتب الاعلامي

Tel: | info@hizb-jordan.org

http://www.hizb-jordan.org/

Reference: PR-01976e66-5650-71cc-83a2-fcae1705963f