
2025-07-23
Rada: Kuzimika kwa Nyota ya Amerika na Kuchomoza kwa Wazo la Ukhalifa. Imeandikwa na Mwanasheria/ Hatem Jaafar (Abu Awab)
Rais wa 47 wa Marekani, Donald Trump, alikuja madarakani kukabiliana na urithi uliokumbwa na migogoro ya ndani na nje, na changamoto kubwa zinazoikabili Marekani, muhimu zaidi ikiwa ni kuyumba kwa hadhi yake ya kimataifa. Hata hivyo, Trump, ambaye ni mtu mkaidi, anayejiamini, anayefahamu mapambano na migogoro na hatakata tamaa, kiasi kwamba aliwatisha wapinzani wake na kujilazimisha kuongoza chama, na sasa anarejea kwa mara ya pili Ikulu ya White House kwa nguvu, akiwa na ushindi mkubwa dhidi ya mgombea wa chama cha Democratic Kamala Harris, na akisaidiwa na makampuni makubwa ya kibepari, katika sehemu zake mbili za ubepari wa kawaida unaowakilishwa na kampuni za mafuta, silaha na reli, na mengineyo ambayo kimsingi ni miongoni mwa misingi ya chama cha Republican, bali yanamuunga mkono, na hata kampuni za kibepari za kiteknolojia, zinazowakilishwa na kampuni za Silicon Valley; Meta, Apple, Amazon na zinginezo, ambazo zilimuunga mkono Kamala Harris katika uchaguzi, kabla ya kuharakisha kujiunga na msafara wa wanaomuunga mkono Trump, ambapo nyingi zao zililipa kiasi cha dola milioni moja kwa sherehe ya kuapishwa kwa Trump. Trump amekuja kwenye kiti cha mamlaka wakati huu akiwa na silaha ya mawazo na mipango ya mrengo wa kulia wa kihafidhina, ambao ni harakati ya kisiasa iliyoanza tangu kuzaliwa kwa Amerika, na iliyoimarika katika miaka ya hamsini ya karne iliyopita, kama harakati ya kisiasa yenye ushawishi, inayotaka utawala wa mtu mweupe wa Kiprotestanti na kurudi kwa maadili ya familia, na miongoni mwa watu wake mashuhuri wa kisiasa ni Rais Reagan.
Kwa kuwa jambo muhimu zaidi linalowatambulisha watawala wa Marekani ni kasi ya mabadiliko, kwa sababu wanategemea hasa tafiti za vituo vya maoni na fikra, sera za Trump katika muhula wake wa urais huu zinatokana na Taasisi ya Urithi (Heritage Foundation), ambayo ni taasisi ya utafiti na elimu iliyoanzishwa mwaka 1973, na bajeti yake ya kila mwaka ni karibu dola milioni 80, na inachukuliwa kuwa moja ya vituo muhimu zaidi vya maoni ya mrengo wa kulia wa kihafidhina, na uanzishwaji wake ulikuwa jibu la kuibuka kwa idadi ya vituo vya fikra huria kama vile Taasisi ya Brookings. Tafiti za Taasisi ya Urithi zilichangia sana katika kumsaidia Rais Reagan kushinda Vita Baridi, katika miaka ya themanini ya karne iliyopita.
Sera za Trump za sasa zinatokana na utafiti, uliochapishwa na Taasisi ya Urithi ya Kihafidhina mwaka 2023, unaojulikana kama Mradi wa Mpito wa Urais 2025, na mipango ya mradi imewekwa katika kitabu kilicho na mapendekezo ya kisiasa yenye kichwa:[Mandate For Leadership: The Conservative Promise. "Mamlaka ya Uongozi, Ahadi ya Kihafidhina"] Utafiti huu, ambao gharama yake ya maandalizi ilifikia dola milioni 22, na ambao sera za Trump zinatafsiri kivitendo, unalenga kuvunja dola kuu, kurejesha mamlaka kwa watu, kukomesha mgawanyiko wa kisiasa wa Marekani, kwa ajili ya mrengo wa kulia wa kihafidhina, kurekebisha nyufa za ndani, kutibu madeni ya shirikisho, ambayo yamefikia dola trilioni 36.2, na nje ya nchi kuimarisha hadhi ya kimataifa ya Marekani.
Mstari mkuu unaoongoza sera ya nje ya Trump ni kupunguza matumizi, kulazimisha, na kuwatumia wengine.
Ama katika nchi za Waislamu, sera ya Trump ni kupambana na kurejea kwa Uislamu, hasa Ukhalifa; njia ya kivitendo ya kuigiza Uislamu katika dola, ndiyo maana Marekani imechukua kuhifadhi kituo chake cha kijeshi cha hali ya juu katika nchi yetu; kitengo cha Kiyahudi, kama kipaumbele.
Ama kwa upande wa njia na mbinu, Trump anategemea matumizi ya nguvu ngumu, au tishio la kuitumia, na anapuuza kabisa nguvu laini yenye madhara na uharibifu mkubwa, ndiyo maana anafanya mauaji ya kimbari huko Gaza mbele ya kamera, na anataka kuiondoa watu wake, akitumia mkono wake, kitengo cha Kiyahudi, na hajali hisia za Waislamu, wala hisia za watu huru kote duniani, bali anatumia ndege zake kulipua mitambo ya Iran, akikiuka sheria za kimataifa, na taasisi ambazo Marekani ilianzisha ili kuonyesha uongozi wake kwa ulimwengu. Bali anataka kuingiza nchi zaidi katika eneo hilo, kuingia katika makubaliano ya Abraham ya kuanzisha uhusiano wa kawaida na kitengo cha Kiyahudi, ambacho anataka kukiteua kama kaka mkubwa kwa watawala wa nchi ndogo vibaraka, kwani televisheni ya Kiarabu ilimnukuu Trump akisema: (Kuna nchi nyingi zinazotaka kujiunga na makubaliano ya Abraham na Iran ilikuwa tatizo). Hakuna shaka kwamba Trump, ambaye amejawa na ulevi wa nguvu, na utiifu wa watawala wa ulimwengu kwa maagizo yake, hajui aina mbili za ukweli:
Kwanza: Ukweli unaohusiana na Amerika na sera yake ya ndani, ambayo ni:
Kwamba Amerika imepiga hatua katika mwelekeo wa kushuka, na kwamba sera yake anayoifuata ni mkakati wa udhaifu, anajaribu kupitia hiyo kuirejesha nchi yake kuwa kubwa tena kama ilivyo katika kauli mbiu yake (MAGA), na kwamba jamii nchini Amerika inakabiliwa na nyufa za ndani; mara kwa misingi ya siasa na maslahi kati ya dola na dola kuu, na mara nyingine kwa misingi ya rangi kati ya wazungu na watu weusi, wakati sera zake zinaimarisha nyufa hizi, na anataka kurejesha utawala kwa mtu mweupe kulingana na maono ya mrengo wa kulia wa kihafidhina, yote hayo yanaashiria kudhoofika kwa jamii na dola. Vile vile, Amerika, ambayo ilitoka baada ya Vita vya Pili vya Dunia, inajiuza yenyewe kama chanzo cha uhuru na maadili ya juu, kama nchi iliyokuwa koloni la nchi kadhaa za Ulaya, Amerika hii imefichuliwa ubaya wake sasa, na mataifa yametambua kuwa ni dola ya kwanza ya kikoloni ulimwenguni, na kwamba ni himaya ya uovu kabisa, haina thamani yoyote, kama vile Wamongolia na Watatari ambao walivamia ulimwengu, na kwa hivyo imeangusha ustahiki wake wa kuongoza ulimwengu isipokuwa kwa nguvu yake katili.
Pili: Ukweli unaohusiana na Uislamu na Waislamu, ambao ni:
Kwamba Uislamu ni dini ya haki ambayo imetoka kwa Mwenye Hekima Mjuzi, ili kurekebisha hali ya mwanadamu katika maisha haya ya dunia, na kwamba Muislamu aliyeinuka ni mja wa Mwenyezi Mungu Subhanahu wa Ta'ala Bwana wake na Mola wake, na kwamba Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye Nguvu Mwenye Uwezo Mkuu, Mwenye Ujabari na Ufalme, ambaye viumbe vinanyenyekea mbele ya utukufu wake, na kwamba Mwenyezi Mungu ndiye Msaidizi wa waja wake Waumini katika maisha ya dunia na Akhera: ﴿Hakika Sisi tunawasaidia Mitume wetu na wale walioamini katika maisha ya dunia na siku watakaposimama mashahidi﴾, huyu Muislamu anayepanda hadi daraja la utumwa kwa Mwenyezi Mungu Mmoja Mwingi wa kulipa, na anategemea Mwenyezi Mungu, na anaomba msaada na misaada kutoka kwa Mwenyezi Mungu, haangalii nguvu ya Amerika, wala ukuu wake unaodaiwa, na katika historia kuna ushahidi mzuri.
Na kwamba matukio makubwa ambayo yameponda umma kwa nguvu, na kuuchukiza kwa uchungu katika miongo iliyopita na bado yanaendelea, yameunda njia ya kufikiri ndani yake, na yamevutia mawazo yake kwa yaliyopita yake tukufu, na ya sasa yake mbaya, na imetambua ukweli wa msemo wa Al-Farooq Omar, Mwenyezi Mungu amuwiye radhi, "Sisi ni watu ambao Mwenyezi Mungu ametutukuza kwa dini hii, hivyo tunapotafuta utukufu katika yasiyo hayo, Mwenyezi Mungu anatutweza", na imetambua kwamba dini hii haitakuwa hai katika maisha yake ikishughulikia migogoro yake, na matatizo yake, isipokuwa kwa dola yake ya ukhalifa juu ya njia ya unabii, hivyo wazo la ukhalifa lilionekana, na bado linaendelea kupanda katika nchi za Waislamu kwa juhudi za watu wanyoofu, mpaka limekuwa maoni ya jumla kwao, hata kafiri mkoloni, akiongozwa na Amerika inayoporomoka, hakupata budi ila kuweka baadhi ya vijiti katika magurudumu ya wazo la ukhalifa, lakini hakuna chochote, kwani limebebwa katika nyoyo za Waislamu na limefafanuliwa katika akili za watu wanyoofu; ambao wanabeba mchoro wa uhandisi wa kuanzisha uongozi sahihi juu ya njia ya unabii, ukizungumzia ulazima wa kurejea kwake, wajibu wa kuwasaidia Waislamu wanaoonewa wanawake, watoto na wazee huko Gaza na katika nchi nyingine za Waislamu, na matatizo ya Waislamu yanayotokana na kuishi bila mifumo ya Uislamu, na mahitaji ya Waislamu ya kurejea kwao kuwa umma mmoja tofauti na watu wengine, na uaminifu wa watawala wa Waislamu ambao wamewaingiza katika vyanzo vya aibu na fedheha kati ya mataifa, na uporaji wa utajiri wa Waislamu ambao wanakufa kwa njaa huko Gaza, na mipaka ya Darfur, yote hayo yanaamuru kurejea kwa ukhalifa na yanaeleza kuibuka kwa wazo lake, ambalo lilitoka katika itikadi hai yenye nguvu, iliyobebwa na umma ambao ni bora kuliko umma wowote uliotolewa kwa watu, ﴿Mlikuwa umma bora kuliko umma wowote uliotolewa kwa watu, mnaamrisha mema na mnakataza maovu na mnamwamini Mwenyezi Mungu﴾.
Chanzo: Rada
