
2/9/2025
Rada: Mjumbe wa Marekani Thomas Park Anadhihirisha Kiburi cha Kimarekani kwa Nchi za Kiislamu
Imeandikwa na Mwalimu/Abdullah Hussein (Abu Muhammad Al-Fatih*)
Matamshi ya Barak - ambaye alionya waandishi wa habari dhidi ya kuchochea machafuko na kuenenda kama wanyama - yalitolewa wakati sauti za wanahabari ziliingiliana wakijaribu kupata matamshi kutoka kwake na kutoka kwa mjumbe wa Marekani Morgan Ortagus, akitishia kusitisha mkutano ikiwa hali ya machafuko itaendelea.
Barak aliwaambia waandishi wa habari "Tutaweka seti tofauti ya sheria hapa.. Nataka mnyamaze kwa muda." Aliongeza, "Mara tu hali hii itakapokuwa ya fujo, na inakaribia tabia ya wanyama, tutaondoka." Aliwataka pia kuwa na "tabia ya kistaarabu, fadhili na uvumilivu," akibainisha kuwa kutofuata sheria hizi ni sehemu ya matatizo katika eneo hilo.
Maoni:
Hivi ndivyo wanasiasa wa Magharibi na watawala wao, haswa Wamarekani, wanashughulika na kiburi, ukaidi, dharau, majivuno, na kejeli, na watawala wa nchi za Kiislamu, wasomi wao mbalimbali, na watu wa Ulimwengu wa Tatu. Je, matusi haya yaliyotolewa na mjumbe wa Marekani dhidi ya waandishi wa habari, hawakupata mtu yeyote kati yao wa kumjibu, akikataa tabia hii ya dharau na majivuno, kama alivyofanya mwandishi wa habari wa Iraq Muntadhar al-Zaidi mwaka wa 2008 alipompiga kofi Rais wa Marekani Bush Jr. alipozuru Iraq, katika mkutano na waandishi wa habari, ambaye alionyesha majivuno, kiburi na tabia ya bwana na watumwa?!
Mjumbe wa Marekani anawatukana waandishi wa habari, au tuseme, anawatukana watu wetu wote huko Lebanon na eneo lote la Kiislamu anapotuelezea kuwa sisi ni watu wa fujo na wanyama, na kwamba machafuko ndio tatizo linaloikabili eneo hilo.
Na swali ni nani anayeanzisha fujo katika nchi yetu? Je, si Marekani ya kikoloni, isiyo na huruma, kwa kuzidisha migogoro ya kimadhehebu, kisiasa na kijeshi ndani yake? Hili ndilo lililoonyeshwa na Condoleezza Rice, Waziri wake wa Mambo ya Nje wakati wa utawala wa Bush Jr., kwamba sera ya Marekani katika Mashariki ya Kati ni (kuchochea machafuko ya ubunifu).
George Friedman, mtafiti wa Kimarekani katika masuala ya baadaye, anaona kwamba sera ya Marekani kuelekea nchi za Kiislamu, na lengo lake (ni kurarua nchi ya Kiislamu na kupanda machafuko ndani yake na kuzichochea pande zake dhidi ya kila mmoja, ili iweze kuzuia kuibuka kwa Milki ya Kiislamu kwa njia hii), basi sera ya Marekani daima, ambayo inachukuliwa na wajumbe na kusimamia utekelezaji wake, ni kuendeleza mzozo kati ya vipengele vya nchi za Waislamu ili kuziandaa kwa kuraruliwa na kuvunjwa na kuondoa utawala wa Uislamu ili kufikia maslahi yake katika nchi yetu.
Kama ilivyo Sudan, mkutano huo wa siri kati ya Jenerali Burhan, Mkuu wa Baraza la Utawala, na mjumbe wa Marekani Massad Boulos huko Uswizi, ambao ulidumu kwa saa tatu, maagizo yalikuwa kuendelea na utiaji saini wa makubaliano ya Abraham na kuanzisha uhusiano wa kawaida na shirika la Kiyahudi la wavamizi, na kuendelea na utekelezaji wa mpango wa kutenganisha Darfur. Hivi ndivyo wajumbe hawa wanavyobeba kwa nchi za Kiislamu; kuchochea vita na uharibifu, kulinda shirika la Kiyahudi na kuliwezesha kupanuka katika eneo hilo, na kumeza ardhi mpya huko Misri, Jordan na Saudi Arabia, kama Netanyahu alivyosema kwa kuanzisha (Israeli Kuu), na kuzuia utawala wa Uislamu katika nchi za Kiislamu ili iwe chini ya ustaarabu wa Magharibi daima.
Kinachotakiwa kutoka kwa watu wa nchi za Kiislamu, na vipengele vyao vyote na makundi yao, ni kuasi dhidi ya hali hizi na kujikomboa kwa kurudi kwenye kanuni ya Uislamu mkuu ambayo inahakikisha umoja wetu na kuanzisha haki kati yetu, basi simameni imarishe ukhalifa Mwenyezi Mungu awarehemu.
Chanzo: Rada
