
8/8/2025
Rada: Mkataba wa Kimataifa Ikiwa Mwadilifu Ataiba, Huachwa, Na Ikiwa Mnyonge Ataiba, Anaadhibiwa!!
Imeandikwa na/Ibrahim Muhammad (Msimamizi)
Mtaalamu wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya haki za binadamu nchini Sudan, Radwan Nweisser, aliwasili Port Sudan siku ya Jumapili, 27/07/2025, na mara moja akaanza mikutano na maafisa, ikiwa ni pamoja na Wizara ya Mambo ya Nje, ambayo ilisema katika taarifa yake kwamba Nweisser "aliwasilisha vipaumbele vya ziara yake wakati wa mkutano, ambayo ni pamoja na kufuatilia haki inayohusiana na vita, programu za kurudi kwa hiari kwa wakimbizi wa ndani na wakimbizi, na kuwezesha uwasilishaji wa misaada ya kibinadamu." (Sudan Tribune, 27/7/2025)
Maoni:
Ziara hii, iliyodumu hadi mwisho wa wiki, ni ya tatu ya aina yake tangu Nweisser ateuliwe na Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Binadamu mnamo Desemba 16, 2022, alipotembelea nchi hiyo mnamo Februari 2023 na Julai 2024. Baraza la Haki za Binadamu liliamua, Mei 11, 2023, kupanua mamlaka ya mtaalamu huyo kujumuisha ufuatiliaji wa kina na kuandika ukiukwaji wote wa haki za binadamu na ukiukwaji tangu Oktoba 25, 2021, pamoja na yale yanayotokana moja kwa moja na mzozo wa sasa. Wakala wa kafiri mkoloni, Radwan Nweisser, alirekodi katika daftari lake visa vya ukosefu wa usalama na udhibiti, akisema: "Tuna wasiwasi kuhusu kesi kali nchini, hivi karibuni, ambazo hazina taratibu zinazohitajika na zilizowekwa katika sheria."
Je, huyu anayeomboleza kwa machozi ya mamba haoni, kama mabwana zake katika Magharibi ya kikafiri mkoloni, mauaji, uhamaji na mauaji ya watu wa Gaza yanayofanywa na dola la Kiyahudi, kiasi kwamba Waziri Mkuu wake wa zamani Ehud Olmert alielezea vita inayoanzisha dhidi ya Ukanda wa Gaza kama janga la kibinadamu, kwani aliona kuwa kinachoendelea ni vita yenye nia za kisiasa maalum na haina uhusiano wowote na malengo halali, na kwamba matokeo yake ya moja kwa moja ni kuugeuza Ukanda wa Gaza kuwa eneo la majanga ya kibinadamu. (Al Jazeera Net, 27/5/2025)?!
Shirika hili na baraza lake linalodaiwa la haki za binadamu hayaoni uhalifu huu kwa sababu sheria yake ni sheria ya msitu. Ikumbukwe kwamba Amerika ilisisitiza mnamo Februari 2025, kujiondoa kwake kwa mara ya pili kutoka kwa baraza hili, ambapo agizo la utendaji lilitolewa na Trump kujiondoa tena na kusimamisha ufadhili uliolengwa kwake, akizingatia kuwa halifai na kwamba linaegemea upande wa taasisi ya Kiyahudi, na kwa hivyo baraza la haki za binadamu limeibuka kutumikia maslahi ya Uingereza na Ulaya katika uwanja wa mzozo wa kimataifa.
Mashirika ya kimataifa na kama wao mashirika ya kikanda na mashirika yote yaliyoundwa kwa misingi isiyo ya Uislamu, na yanatumia sheria zisizo sheria za Uislamu, haijuzu kwa dola kushiriki ndani yao, kama vile Umoja wa Mataifa, na mikono yake yote kutoka Mahakama ya Kimataifa ya Haki, Shirika la Fedha la Kimataifa na Benki ya Dunia, na kama mashirika ya kikanda kama vile Jumuiya ya Nchi za Kiarabu na mengineyo.
Kujitoa kutoka kwa mashirika haya ambayo hayathamini utakatifu wowote na kujifanya polisi wa kimataifa, bali ni kwa njia ya wajinga na mataifa yaliyopita, ikiwa mwadilifu ataiba miongoni mwao; Amerika na mwanawe, taasisi ya Kiyahudi, wanamwacha na hawatumii wapelelezi kumchunguza, na ikiwa mnyonge ataiba katika nchi tegemezi zinazoongozwa na wateja wao, wanamwadhibu!
Kujitoa kutoka kwa mkataba huu batili wa kimataifa na taasisi zake ni wajibu kwa watu wote huru wa ulimwengu na kila dola yenye mamlaka, vipi kuhusu taifa bora lililoletwa kwa watu, ambalo Mungu alilifanya kuwa mwangalizi wa ubinadamu﴿NA HIVYO TUMEKUFANYENI UMMA WA WASTANI ILI MUWE MASHAHIDI JUU YA WATU NA MTUME AWE SHAHIDI JUU YENU﴾?! Lakini hili haliwezekani kutoka kwa nchi tegemezi za kitaifa zilizopo katika nchi za Waislamu. Ushuhuda juu ya mataifa hauwezi kuwa ila katika kivuli cha dola ya Kiislamu; Ukhalifa kwa misingi ya unabii, ambayo hufanya mamlaka kuwa ya sheria, kwa hivyo inakuwa na mamlaka na uongozi na inakuwa dola ya kwanza ulimwenguni.
Chanzo: Rada
