
2/9/2025
Rada: Taarifa kwa Vyombo vya Habari kutoka Hizb ut-Tahrir Wilaya ya Sudan Enyi watu wa Sudan, mna uwezo wa kufelisha mpango wa kuikata Darfur, basi simameni kwa utiifu kwa Mwenyezi Mungu!
Imeandikwa na: Ibrahim Othman Abu Khalil
Katika hatua iliyotarajiwa, kiongozi wa vikosi vya usaidizi wa haraka, Muhammad Hamdan Daglo, aliapa kama rais wa baraza la urais la kile kinachoitwa serikali sambamba, katika Nyala, mji mkuu wa kusini mwa Darfur, Jumamosi, 30/8/2025, na vile vile naibu rais, wajumbe wa baraza la urais, na waziri mkuu walikula kiapo.
Hatua hii ilitarajiwa kama sehemu ya mpango wa uhalifu wa Amerika, unaolenga kuitenganisha Darfur, kupitia vibaraka wake kutoka kwa viongozi wa jeshi, viongozi wa vikosi vya usaidizi wa haraka, na mamluki wa siasa.
Hatua hii ilikuja kwa kasi, kufuatia mkutano wa Burhan na mshauri wa rais wa Amerika, Mussad Boulos huko Zurich, Uswizi, ambayo iliharakisha hatua hiyo kabla ya kuanguka kwa Al-Fasher.
Kuhusiana na uhalifu huu hatari, athari za watu wa Sudan zilitofautiana katika makundi yao tofauti, na zilikuwa kama ifuatavyo:
– Wale wanaokimbilia kutekeleza mpango huo, na watekelezaji wake, wakitarajia kile Amerika inacho, na hawa lazima wachukuliwe hatua na kuzuiwa kutekeleza uhalifu huu mkuu.
– Wale waliofadhaika ambao wanaomba watu wakubali hali halisi, kana kwamba kujitenga kwa Darfur ni hatima isiyoepukika ambayo lazima iridhiwe! Hawa ni pamoja na wanasiasa, wanahabari, na wengineo, na hatari yao inadhihirika wanapoamka na kueneza kufadhaika kwa wengine, na hawa lazima wachukuliwe hatua na kuwafahamisha vipengele vya nguvu vinavyowawezesha kufelisha mpango huo.
– Kundi lisilojali kinachoendelea kana kwamba kinachotokea kiko katika sayari nyingine! Kwa sababu hawajui kinachoendelea karibu nao, na hawa lazima waelimishwe na kuhamasisha nguvu zao ili kufelisha mpango huo.
– Jamii ambayo mpango huo umefichuliwa, na inatarajia matukio na kuona zaidi ya ukuta, na inastahili kuchukua mchana na usiku, na kuhamasisha nguvu za makundi yote, sio tu kufelisha mpango wa kuigawanya Sudan na kuikata Darfur, lakini pia kwa ajili ya kuunda upya maisha, na kuipindua meza, na kuiondoa umma wetu kutoka kuwa lengo la njama za Magharibi makafiri na miradi yake ya uhalifu, hadi kuwa mbeba mienge ya uongofu na nuru kwa Magharibi haya makafiri, na katika sehemu zote za dunia.
Sisi katika Hizb ut-Tahrir / Wilaya ya Sudan, tulikuwa, na bado tuko waangalifu uchi, ambaye anafichua njama, na kuchochea hima za kufelisha mipango ya uhalifu.
Enyi watu wa Sudan: Mna uwezo wa kufelisha mpango huu unaolenga kuivunja nchi yenu katika toleo lake la pili, ambalo linakusudiwa kuitenganisha Darfur, ikiwa mtamtegemea Mwenyezi Mungu kwa kumtegemea kweli kweli, na kumwomba msaada Yeye Subhaanahu wa Ta’ala, na mtafanya yafuatayo:
* Kwamba mjitenge na kila kibaraka msaliti, ambaye amechukua jukumu la kutekeleza mpango huu, kwa kuunda serikali sambamba, au kwa uzembe na kuiacha Al-Fasher ili vikosi vya usaidizi wa haraka vikamilishe udhibiti wake wa eneo lote la Darfur.
* Kwamba muhamasishe nguvu za wanyoofu kutoka kwa watu wa nguvu na ulinzi, ili kufelisha mpango huo na kuchukua hatua dhidi ya vibaraka na wasaliti.
* Hamasisheni nguvu zote za vyombo vya habari, mimbari za misikiti, na vinginevyo ili kufichua mpango huo, na zana zake za utekelezaji ndani, na kuhamasisha watu kusimama kuukabili.
* Hamasisheni nguvu za wanyoofu, wasio na uhusiano wowote na wasaliti, kutoka kwa viongozi wa makabila, wakuu wa koo, wasomi, wenye maoni, viongozi, wanasiasa, wanasheria, na wazee wote, kuunda ukuta imara unaolinda umoja wa kile kilichosalia cha nchi yetu.
Je, hii yote si nguvu kubwa, inayoweza kufelisha mpango wa Amerika, ambao ni hila za shetani, ﴿Hakika hila za shetani ni dhaifu﴾, ﴿Na wanapanga na Mwenyezi Mungu anapanga, na Mwenyezi Mungu ndiye mbora wa wapangaji﴾, na Mtume ﷺ anasema: «Hakika atakayeishi miongoni mwenu baada yangu ataona tofauti nyingi, basi shikamaneni na sunna yangu na sunna za makhalifa waongofu waongozaji, shikamaneni nazo na ziumeni kwa magego». Imesimuliwa na Al-Arbadh bin Sariyah Radhi za Allah ziwe juu yake, na ameitoa Abu Daud, Tirmidhi, Ahmad na Ibn Hibban.
Chanzo: Rada
