
2025-06-30
Radaa: Hizb ut-Tahrir Wilaya ya Sudan.. Taarifa kwa Vyombo vya Habari
Tangu Ijumaa tarehe 27/6/2025, vyombo vya habari vimeripoti kuwa Rais wa Eritrea, Isaias Afwerki, amekubali kuwafunza wapiganaji 50,000 kutoka majimbo ya Kaskazini na Mto Nile, mafunzo ya hali ya juu ya kijeshi, kufuatia ombi lililotolewa na mkuu wa taasisi ya Kaskazini, Muhammad Sayyid Ahmed Al-Jakoumi, mkuu wa njia ya Kaskazini katika makubaliano ya Juba ya amani ya Sudan.
Tumesubiri hadi Jumapili tarehe 29/6/2025 kuona majibu ya serikali, na msimamo wake kuhusu habari hii mbaya, jibu lilikuja likishtua, ambapo mkuu wa taasisi ya Kaskazini alifafanua kwa chanzo kimoja cha habari; mpelelezi, kwamba jeshi na vyombo vya usalama vilifahamishwa juu ya agizo la kuwafunza vikosi hivi, na akasema: "Tunafanya kazi ya kupanga nao, na hatuwezi kuchukua hatua yoyote isipokuwa kwa idhini yao"!
Tangazo hili linakuja wakati dalili za mgawanyiko wa Sudan zikionekana, na udhibiti wa vikosi vya msaada wa haraka juu ya majimbo ya Darfur, na kutishia kutangaza serikali sambamba, na udhibiti wa kikanda na kikabila juu ya hotuba ya kisiasa, na kuimarisha mgao wa madaraka, kwa wakati huu Burhan anaendelea kuinua kauli mbiu ya (kikosi cha wanamgambo kwa kila mkoa), ambapo wanamgambo wapya wanaundwa kila asubuhi mpya! Kisha, hatari zaidi ya hii, ni mafunzo ya wanamgambo kwa wanachama wao nje ya nchi; Eritrea, na tangazo la Al-Jakoumi linakuja katika muktadha huu!
Sisi katika Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Sudan, kwa kuzingatia habari hii ya kushtua, tunathibitisha yafuatayo:
Kwanza: Tulikuwa tumeonya mara kwa mara juu ya hatari ya kuongezeka kwa wanamgambo wenye silaha, na kwamba wao ni majembe ya kubomoa dola, na njia ya kumwingiza kafiri mkoloni anayetaka kuigawanya Sudan, na kuirarua kupitia ukabila na chuki za kibaguzi, na hapa ndipo jukwaa la ujinga linakamilika kwa kaskazini mwa Sudan pia kuwa na wanamgambo, kama ilivyo kwa mikoa mingine ya Sudan!
Pili: Uislamu umeharamisha kupigana chini ya bendera za ushabiki na upofu, Mtume (SAW) amesema: "Na yeyote anayepigana chini ya bendera ya upofu, akikasirika kwa ajili ya ushabiki, au anatoa wito wa ushabiki, au anashinda ushabiki, kisha akauawa, basi kifo chake ni cha kijahiliya."
Tatu: Kuzungumza kuhusu kwamba wanamgambo hawa au wale, watakuwa chini ya uongozi wa jeshi, ni kujificha, mwanzo huanza daima hivi, kisha hutokea yale ambayo hayafurahishi, na tuna vikosi vya msaada wa haraka kama mfano mbaya zaidi wa utengenezaji wa wanamgambo.
Nne: Serikali kwa kitendo chake hiki, inataka kuimarisha mpango wa mipaka ya damu, ili kutekeleza Sykes-Picot mpya ya Marekani ya kuirarua Sudan iliyobaki.
Wajibu kwa jeshi ni kuanza mara moja kuunganisha vikosi vyote vya silaha vilivyoenea nchini, chini ya bendera yake tu, ili kuifanya kuwa nguvu moja thabiti, na yenye uwezo wa kulazimisha mamlaka ya dola, kisha kuipa nusra Hizb ut-Tahrir ili isimamishe Khilafah Rashidah ya pili kwa misingi ya Utume, na kuunganisha umma kwa msingi wa Uislamu mkuu, na kutekeleza hukumu za Kiislamu, na kung'oa ushawishi wa kafiri mkoloni kutoka nchini mwetu, na kutoka nchi zote za Waislamu.
﴿Enyi mlio amini! Muitikieni Mwenyezi Mungu na Mtume anapo kuwaiteni kwenye litakalo kuishieni ﴾
Jumatatu 05 Muharram 1447 AH
2025/06/30 AD
Ibrahim Othman (Abu Khalil)
Msemaji rasmi wa Hizb ut-Tahrir katika Wilaya ya Sudan
Chanzo: Radaa
