
28/6/2025
Rada: Hizb ut-Tahrir Wilaya ya Sudan Yatoa Taarifa Muhimu
Tofauti kubwa iliyopo baina ya heshima chini ya kivuli cha Uislamu, na unyonge chini ya ukandamizaji wa tawala tegemezi.
Kamati Kuu ya mitihani ya shahada ya Sudan imetoa wito kwa jamii ya kimataifa na mashirika husika kuendelea kuunga mkono juhudi za Wizara ya Elimu, na kuchangia katika kuwawezesha wanafunzi wote wa Sudan, kufanya mitihani, haswa maeneo yaliyoathirika na vita, na hali ngumu za kibinadamu. (Suna, 26/06/2025).
Bado kuna kundi la watu wetu wana matumaini mema kwa Umoja wa Mataifa na mashirika yake, na wanatarajia msaada kutoka kwa wale wanaoitwa jamii ya kimataifa na mashirika ya kimataifa, licha ya historia yake ambayo inathibitisha kuwa haitoi kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, kwani siyo vyama vya hisani, bali ina ajenda ambayo inafichuka kila wakati kuhusu uadui wake wa wazi kwa Uislamu na Waislamu.
Mnamo mwaka wa 2016, UNESCO ilifanya mkutano wa kuzuia (itikadi kali za vurugu), na mojawapo ya matokeo yake ilikuwa kwamba "lazima suala la kubadilisha mitaala ya elimu katika Mashariki ya Kati, na maeneo mengine ambayo yanashuhudia ustawi wa mawazo kali, lishughulikiwe".
Neno hili (mawazo kali) linatumiwa na linamaanisha Uislamu pekee, kwa sababu nchi za Magharibi zinazodhibiti ulimwengu leo, zinataka Uislamu wa ukasisi, ambao hauna uhusiano wowote na maisha, kwa upande wa mifumo ya utawala na siasa, mfumo wa kiuchumi, na mfumo wa kijamii, ili wasipate kikwazo katika kutekeleza mipango yao, bali wanaendelea na matendo yao yote ya uhalifu dhidi ya Waislamu; ya mateso na mauaji, na kujitenga kwa Sudan Kusini, na vita vinavyoendelea sasa nchini Sudan, ni matokeo ya kufuata Magharibi ya kibepari, na mashirika yake ya uhalifu.
Jukumu la mashirika haya yanayoitwa ya kibinadamu linazidi kile kilichotangazwa, hadi kujaribu kupotosha maoni ya umma, kwa kusambaza habari potofu kuhusu ukweli wa hali katika maeneo ambayo yanaendesha shughuli zake, ili shughuli zake ziendelee, pamoja na kufanya majukumu ya ujasusi yenye shaka kwa niaba ya nguvu za kimataifa, hata idadi ya wachunguzi walielezea kuwa ni zana za ukoloni mamboleo! Bali ni miongoni mwa zana hatari zaidi za mizozo ya kimataifa.
Na nchini Sudan, ni mara ngapi mashirika haya ya kimataifa yamefichuliwa yakifanya kazi ya ujasusi, na upelelezi kwa maslahi ya nchi za Magharibi, na hiyo haishii tu katika kukusanya taarifa, bali inazidi kueneza sumu za mgawanyiko, na mapigano kati ya makundi ya wakazi, kama ilivyotokea Sudan Kusini, ambapo mashirika haya yamechangia kwa upendeleo wao kwa upande mmoja wa mzozo, katika kuzidisha migogoro hii, wakitumia kinga walizopewa.
Ukombozi wetu uko mikononi mwetu wala si mikononi mwa maadui zetu ambao wanatuwindia; iwe ni wale wanaotuonyesha uadui waziwazi, au wale wanaovaa unafiki kama vazi la marafiki, na vazi la "washirika" (wafadhili).
Kuhusisha masuala ya elimu; ambayo ni muhimu zaidi katika kulea na kutengeneza vizazi kupitia hayo na mashirika haya yenye shaka, ni sawa na kujiua kisiasa, na ni maangamizi makubwa, ambayo athari zake za uharibifu kwa jamii zinaonekana mapema au baadaye.
Elimu inawakilisha nguzo muhimu katika uamsho wa Waislamu, na ili iwe hivyo lazima kuwe na mfumo wa kisiasa uliojengwa juu ya itikadi ya Uislamu mkuu, mfumo ambao unajumuisha maono ya kisiasa tofauti, ya juu, na huru kwa nchi yake, kuondoa wanadamu kutoka katika giza la ukafiri, upotofu na ujinga, hadi kwenye nuru ya Uislamu na uadilifu wake, ambao huleta kwa wanadamu katika nyanja zote za maisha; kiroho, kiakili, kiadili, kisiasa, kiuchumi, na zinginezo, na katika sayansi na teknolojia. Mfumo huu wa kisiasa, kwa kauli moja, ni mfumo wa Khilafah Rashidah kwa njia ya Utume, ambao unatekeleza Uislamu na mifumo yake kikamilifu, na ambao uliongoza ulimwengu kwa karne kadhaa katika ubora wa taasisi zake za kitaaluma, na uvumbuzi wake wa hali ya juu, na uvumbuzi, pamoja na mchango wake mkubwa katika maendeleo ya binadamu, basi ni tofauti kubwa iliyopo baina ya heshima chini ya kivuli cha Uislamu, na unyonge chini ya kivuli cha mifumo ya utegemezi.
Ijumaa ٠٢ Muharram 1447 Hijria
2025/06/27 Miladia
Msemaji Rasmi wa Hizb ut-Tahrir katika Wilaya ya Sudan
Chanzo: Rada
