
2025-09-23
Rada:Hakuna ukombozi kwenu watu wetu nchini Sudan
Wala amani wala usalama ila katika kivuli cha utawala wa Kiislamu
Katika historia yote, wingi wa makabila nchini Sudan haujawahi kuwa sababu ya migogoro na mapigano, bali sababu ya hayo ni mzozo mkali wa kisiasa na kijeshi kati ya nchi za kikoloni na vibaraka wao, ambao umeangamiza mazao na vizazi, hasa baada ya kuzigawa nchi na kupanda mbegu za fitina na mapigano ya kikabila na kidugu kama inavyotokea leo, na kama ilivyokuwa ikitokea katika zama za ujahiliya. Tangu kupotea kwa Uislamu na kuangushwa dola yake, watu wamerudi kwenye hukumu za kijahiliya wakipigana kwa misingi ya ukabila ambao Mtume ﷺ alikataza na kusisitiza kuhusu hilo, aliposema: «Mwenye kupigana chini ya bendera ya upofu, akiita ubaguzi au anaghadhibika kwa ajili ya ubaguzi, basi kifo chake ni cha kijahiliya».
Kwa hivyo, ni lazima watu wa Sudan watambue kwamba siasa zilizopo, ambazo hazina fikra sahihi za kisiasa na zina uhusiano na Magharibi kafiri, ndizo sababu ya migogoro na matatizo, kutokana na mgawanyiko wa kisiasa unaotegemea misingi ya ukabila mbaya, ambapo serikali zilizopita zimetumia makabila kama kuni za migogoro yao, na zimefuata mfumo wa vyama katika mgawanyiko wa kikabila. Yaliyotokea Darfur na yanayoendelea ni mfano bayana wa hilo, pale ambapo baadhi ya makabila yaliunga mkono harakati za uasi za silaha, na hivyo kuifanya serikali nayo iwaapishe makabila yanayoiunga mkono na kuwatumia katika kupigana na waasi. Na linganisha na mfumo huu namna serikali zilizopita zilivyoshughulika na maeneo yote nchini Sudan, ambayo yameleta hali ya wasiwasi na tahadhari katika maeneo yote hadi nchi nzima imekuwa pipa la baruti linaloweza kuwaka wakati wowote, huku mshindi pekee katika mzozo huu na mapigano ya kikabila ya kinyama ni watu wa nchi, ambao bado wanalipa gharama kubwa kwa damu na roho zao, kwani kwa bahati mbaya wao si chochote ila zana duni zinazotumiwa kuuana!
Uislamu umeheshimu sana utakatifu wa damu ya Muislamu, kwani Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema: ﴿Na anayemuua Muumini kwa kukusudia, basi malipo yake ni Jahannamu, atadumu humo, na Mwenyezi Mungu amemkasirikia na amemlaani, na amemuandalia adhabu kubwa﴾ Na Mtume ﷺ amesema: «Kuangamia kwa dunia ni wepesi zaidi kwa Mwenyezi Mungu kuliko kumuua Muumini bila haki» na pia akasema: «Waislamu wawili wanapokutana na panga zao, basi muuaji na muuwaji wote wawili wataingia motoni» Hivyo tuko wapi katika kumfuata Mtume ﷺ? Na tuko wapi katika kufuata kitabu cha Mwenyezi Mungu Mtukufu anayesema: ﴿Enyi watu! Hakika Sisi tumekuumbeni kutokana na mwanamume na mwanamke. Na tumekufanyeni mataifa na makabila ili mjuane. Hakika aliye mtukufu zaidi kati yenu kwa Mwenyezi Mungu ni huyo aliye mchamngu zaidi. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi, Mwenye khabari.﴾ Kwa hivyo, ilikuwa lazima kwetu kujitahidi kusimamisha umwagaji damu unaoendelea na kusimamisha mpango wa Magharibi kafiri kwa kufuata amri za Mwenyezi Mungu na Mtume wake, yaani kwa kuhukumu kwa Uislamu, kwani mapigano ya kikabila hayatakoma, hali haitatulia, na ukatili dhidi ya roho za wasio na hatia hautakoma ila kwa kurudi kwenye Uislamu na kubatilisha kila kitu kinachokinzana nao.
Lakini Uislamu hautakuwepo ila kwa mamlaka, yaani dola itakayoutekeleza na kuubeba ulimwenguni kwa da'wa na jihad, nayo ni dola ya Khilafah Rashidah ya pili kwa njia ya Utume, ambapo utawala ndani yake utakuwa ni jukumu na sio faida, itatimiza wajibu wa kuwahudumia watu kwa afya, elimu, usalama, na kuwawezesha watu katika kilimo na viwanda na kufungua njia za ufugaji ili kusiwe na msuguano kati ya wakulima na wafugaji, itakata mikono ya waharibifu bila kusita, na itakomesha dalili zote za mauaji, uchomaji moto, na uporaji, kwa kutekeleza hukumu kwa wanaokiuka sheria.
Hakika dola ya Khilafah ndiyo pekee inayoweza kuunganisha watu kama umma mmoja kwa misingi ya Uislamu mtukufu na sio kwa misingi ya ubaguzi wa rangi, ukabila, au utaifa, kwani inakwenda kwa hukumu za Uislamu na mamlaka yake, mamlaka hii ambayo iliwakusanya Waislamu na kuwafanya ndugu wanaopendana kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, iliunganisha baina ya Abu Bakr Mwarabu na Bilal Mhabeshi na Salman Mpersia na Suhayb Mrumi na Hamza Mquraishi, na Muadh Al-Ansari…
Hakika Uislamu mtukufu ndio pekee katika historia ya wanadamu ambao uliunganisha watu, rangi na makabila mbalimbali katika umma mmoja, haukuwa umefungwa katika Madina bali ulienea katika kisiwa chote na kulikuwa na ushindi wa Kiislamu wa kueneza Uislamu, Waislamu waliteka Iraq, na ilikuwa ikikaliwa na Wakristo, Wamazdakia na Wazoroasta kutoka Waarabu na Wapersia, na waliteka Uajemi na ilikuwa ikikaliwa na Waajemi, Wayahudi na Warumi, na waliteka Sham na ilikuwa eneo la Kirumi linalokaliwa na Wasuri, Waarmenia, Warumi na Waarabu, na waliteka Afrika Kaskazini ambako kuna Waberber, na waliteka Sindh, Khwarazm, Samarkand na Andalusia, na waliunganisha watu hao wote katika umma mmoja, bila ubaguzi wowote kati yao, kwa hivyo nuru ya Uislamu ilizunguka pande zote za dunia katika kipindi kifupi; hii ni kwa sababu amri za Uislamu zinahitaji kuwatazama raia kwa mtazamo wa kibinadamu, sio mtazamo wa kibaguzi, au kimadhehebu, kwani hukumu za Uislamu zilitumika kwa kila mtu, kwa hivyo watu wote walikuwa raia wa dola ya Kiislamu bila tofauti kati ya Muislamu na asiye Muislamu na hakuna anayemdhulumu mwingine na ikiwa itatokea, basi Uislamu unamkemea na kumzuia, Mwenyezi Mungu amesema: ﴿Wala kuchukiana na watu kusikupelekeeni kutowatendea uadilifu. Fanyeni uadilifu. Hivyo ndio karibu zaidi na uchamungu.﴾, na watu wote wako sawa katika hukumu mbele ya mahakama, na mfumo wa utawala unahitaji umoja kati ya sehemu za dola, kama unavyohitaji kuhakikisha mahitaji ya kila jimbo bila kujali mapato yake kwa hazina, ambayo inafanya kuungana kuwa jambo lisiloepukika kati ya watu wa majimbo yote ya dola.
Kwa hivyo, ilikuwa ni wajibu kwa kila Muislamu na Muislamu kufanya kazi ya kusimamisha faradhi hii kuu iliyopotea, ngome ya Khilafah Rashidah kwa njia ya Utume. ﴿Hakika huu Umma wenu ni Umma mmoja, na Mimi ndiye Mola wenu, basi niabuduni.﴾.
Imeandikwa na mwalimu/ Rana Mustafa
Chanzo: Rada
