
8-11-2025
Rada: Chini ya Mwavamuli wa Kimataifa na kwa Ushiriki wa Watawala wa Kiislamu
Amerika Inafanya Kazi Kuizingira Gaza na Kuhakikisha Usalama wa Wayahudi
Imeandikwa na Ustadh/Salah El-Din Adada
Vyanzo rasmi vilifichua siku ya Alhamisi kwamba Marekani ilisambaza rasmi rasimu ya azimio kuhusu Ukanda wa Gaza kwa wajumbe wa Baraza la Usalama la Kimataifa, ikitoa wito wa kuanzishwa kwa baraza la amani na mfuko wa ufadhili kwa ajili ya ujenzi mpya, na kubainisha miundombinu ya mipango ya utawala katika Ukanda wa Gaza siku iliyofuata, na kuikabidhi kwa nguvu ya kimataifa inayojumuisha hasa wanajeshi kutoka nchi za Kiislamu. Kifungu cha saba cha rasimu hiyo kinasema kwamba kikosi hicho kitafanya kazi na taasisi ya Kiyahudi na Misri, pamoja na kikosi kipya cha polisi cha Palestina ambacho kitaanzishwa chini ya usimamizi, ili kulinda maeneo ya mpaka na kuleta utulivu wa mazingira ya usalama huko Gaza, kwa kuhakikisha mchakato wa kuondoa silaha katika eneo hilo, ambao unajumuisha uharibifu na kuzuia ujenzi mpya wa miundombinu, uwezo wa kijeshi, uwezo wa kushambulia, na kuondoa silaha za makundi kwa kudumu.
Ni wazi kwamba Marekani imeazimia kupanga mambo ya kiusalama katika eneo hilo kwa njia ambayo inahakikisha usalama wa kituo chake cha Mashariki ya Kati, taasisi ya Kiyahudi, kwa miaka mingi ijayo baada ya kugundua hatari kubwa inayokizunguka na kutishia mustakabali wake. Matukio ya tarehe 7 Oktoba 2023 ndiyo yaliyopiga kengele na kutoa onyo la uwepo kwa taasisi hii. Kwa hivyo, haishangazi kwamba mjumbe wa Marekani Tom Barak anaitishia jeshi la Lebanon kwa kuwapa muda unaoisha mwishoni mwa Novemba hii ili kufanya mabadiliko katika hali inayohusiana na suala la silaha za chama cha Iran, na kwamba ikiwa hilo halitatokea, taasisi ya Kiyahudi itaweza kuzindua mashambulizi na Marekani itafahamu hilo. Katika muktadha huo huo, masharti ya Marekani katika mazungumzo na Iran yanakuja ambapo inataka kukabidhiwa uranium iliyorutubishwa na kupunguza upeo wa makombora ya balistiki hadi chini ya kilomita 500.
Na huko Gaza Hashem, Marekani inaharakisha hatua za kuondoa silaha na kuharibu miundombinu na uwezo wa kijeshi huko, kwa njia ambayo inadhani itahakikisha usalama wa Wayahudi kwa miongo mingi ijayo. Na kwa sababu inajua kwamba kazi hii ni chafu na imefunikwa na kauli mbiu ya amani, inajitahidi kuikabidhi kwa vikosi vinavyohusiana na nchi za Kiislamu na inapendelea kushirikisha vikosi vya Mamlaka ya Palestina pamoja nao, ili mchakato huo ufunikwe na tabia ya maslahi ya kitaifa badala ya kueleweka kwa ukweli wake kama vikosi vinavyounga mkono vikosi vya Wayahudi.
Na hivyo, watawala wa Waislamu, baada ya kukamilisha miaka miwili ya kukatisha tamaa na kupanga njama dhidi ya Gaza na watu wake, kwa kunyamazia kimya uhalifu uliofanywa na taasisi ya Kiyahudi, na kutochukua hatua kwa majeshi ya umma kuinusuru, bali na kuisaidia taasisi ya Kiyahudi kwa pesa, bidhaa, silaha na upotoshaji, wanaingia mwaka wao wa tatu ili kukamilisha juhudi zao za awali katika huduma ya Marekani na Wayahudi kwa kushiriki kwao katika kupanga hali kwa njia ambayo inahifadhi usalama wa taasisi hiyo ya baadaye na kuzima moto wa mapambano dhidi ya uvamizi.
Hakika, watawala hawa ni vibaraka wa Magharibi, na watumishi wa miradi yao ya kikoloni, wanaharakisha kwa pesa na askari wakati Amerika inawaita kuwaokoa taasisi ya Kiyahudi, wakati wao hunyamaza kimya kama watu wa makaburi, hawasikiki wakisema chochote wakati umma wao unawaita kutoka chini ya vifusi na wazee wao, wanawake na watoto.
Kile ambacho Marekani inataka ni hatari sana! Kwa mpango huu, inajaribu kuhamisha majeshi ya Waislamu hadi hatua ya tatu! Hatua ya kwanza ilikuwa wakati majeshi ya Waislamu yalipoikabili taasisi ya Kiyahudi katika vita vya maigizo, kisha hatua ya pili ilikuwa kwamba walisimama na kutazama mauaji dhidi ya watu wa ardhi takatifu huku wao wakiwa walinzi wa mpaka wao, lakini leo Marekani inataka kuingiza majeshi ya Waislamu katika hatua ya tatu, ambayo ni kuwageuza kuwa nguvu ya kijeshi inayounga mkono taasisi ya Kiyahudi moja kwa moja katika ardhi inayokaliwa ya Palestina, na hili ni jambo hatari ikiwa litatokea.
Kwa hivyo, umma wa Kiislamu, haswa wale wenye maoni na wamiliki wa majukwaa kutoka kwa wanahabari na washawishi, wanapaswa kuonya umma juu ya masilahi yao ili wasianguke katika uovu wa hatua hii. Na Waislamu wote wajue kuwa hakuna njia ya kutoka katika njama hii dhidi ya ardhi takatifu ya Palestina, na sehemu zingine takatifu za Waislamu, nchi zao na masilahi yao isipokuwa kurekebisha dira ya majeshi yao kwamba waaminifu ndani yao wanapaswa kuchukua hatua na kutoa ushindi kwa Hizb ut-Tahrir ili kusimamisha mfumo wa kisiasa ambao uliitetea kwa karne nyingi, ambayo ni mfumo wa Khilafah, leo kabla ya kesho, ili kurejesha nchi zake zote kutoka Palestina hadi Kashmir kutoka kwenye makucha ya ukoloni na zana zake, ﴿Na kwa yakini Mwenyezi Mungu atamsaidia anayemsaidia Yeye. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu, Mwenye kushinda.﴾.
Mhandisi Salah El-Din Adada
Mkurugenzi wa Ofisi Kuu ya Habari ya Hizb ut-Tahrir
Chanzo: Rada
