Organization Logo

مصر - المكتب

ولاية مصر

Tel:

info@hizb.net

www.hizb.net

Magereza ya Misri Kati ya Mateso na Mauaji Wakati Heshima Inapoporwa na Haki Kuuawa!
Press Release

Magereza ya Misri Kati ya Mateso na Mauaji Wakati Heshima Inapoporwa na Haki Kuuawa!

July 31, 2025
Location

Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Magereza ya Misri Kati ya Mateso na Mauaji

Wakati Heshima Inapoporwa na Haki Kuuawa!

Katika tukio linalojirudia la uhalifu uliofichwa, kijana Ayman Sabri alifariki ndani ya kituo cha polisi katika mkoa wa Dakahlia, kutokana na mateso ya kikatili yaliyoacha athari zake wazi mwilini mwake, na haikupita saa 48 kabla ya kijana mwingine kufariki ndani ya kituo cha polisi cha Al-Saf katika mkoa wa Giza, huku kukiwa na simulizi zinazofanana kuhusu kupuuzwa kwa makusudi, unyanyasaji na ukosefu wa ubinadamu, jambo ambalo limegeuza vituo hivyo kuwa mahali pa kifo cha polepole.

Kama ilivyo kawaida, utawala wa Misri umekanusha uhusiano wowote na suala hilo, na umedai kuwa vifo hivyo vilitokana na "sababu za asili", licha ya ushuhuda wa mashahidi, picha zilizovuja, na hali ya miili ambayo inathibitisha kuwa wamiliki wake waliteswa. Kwa nini wahalifu hawawajibishwi? Kwa nini uchunguzi wa kina na wa uwazi haufunguliwi? Na kwa nini kesi hufungwa daima na "hakuna sababu ya kufungua kesi"? Bali kwa nini utawala unasisitiza kuwalinda wahalifu na kuwaondolea hatia, ikiwa sio wao ndio akili na watekelezaji wa uhalifu huo?

Vifo katika vituo vya polisi na magereza sio ubaguzi tena au makosa ya kibinafsi, lakini imekuwa njia inayojirudia, katika mfumo wa usalama ambao hauna hofu ya kuwajibishwa, wala haupati mtu wa kuuzuia, pamoja na kutoweka kwa lazima, kukamatwa kiholela, na kunyimwa kesi ya haki, vituo vya kizuizini vimekuwa vituo vya udhalilishaji na mauaji.

Kulingana na ripoti za mashirika ya haki za binadamu, vituo vya polisi vya Misri vinashuhudia mazingira mabaya ya kizuizini, ambapo makumi ya watu wamekusanywa katika vyumba vidogo ambavyo havifai kwa wanyama, huduma ya afya inanyimwa, na mateso hutumiwa kama njia ya kuwadhalilisha wafungwa au kupata ungamo chini ya vurugu.

Hii inakiuka wazi yale ambayo Uislamu umeamuru kama wajibu wa serikali kwa raia wake, kwani dola katika Uislamu inawajibika kuhifadhi damu, heshima na utu, kwa hivyo ikiwa dola itageuka kuwa chombo cha ukandamizaji, na upanga ulioelekezwa kwenye shingo za watu, itakuwa imesaliti uaminifu, imekiuka agano, na imekuwa adui kwa raia wake mbele ya Mungu Mwenyezi. Kama alivyosema ﷺ katika kueleza hatari ya yule anayepewa mamlaka ya watu na kuwazuru au kuwadhulumu: «اللَّهُمَّ مَنْ وَلِيَ مِنْ أَمْرِ أُمَّتِي شَيْئاً فَشَقَّ عَلَيْهِمْ فَاشْقُقْ عَلَيْهِ، وَمَنْ وَلِيَ مِنْ أَمْرِ أُمَّتِي شَيْئاً فَرَفَقَ بِهِمْ فَارْفُقْ بِهِ» Hii ni dua kutoka kwa Mtume ﷺ kwa yule anayewadhulumu umma na kuwazidi nguvu, vipi hali ya yule anayewatesa na kuwaua magerezani?! Na vipi kwa yule anayefanya vituo vya polisi kuwa mahali pa kulipiza kisasi, sio haki?!

Miongoni mwa wajibu wa dola katika Uislamu ni:

- Kuhifadhi nafsi na heshima, alisema ﷺ: «إِنَّ دِمَاءَكُمْ وَأَمْوَالَكُمْ حَرَامٌ عَلَيْكُمْ كَحُرْمَةِ يَوْمِكُمْ هَذَا فِي شَهْرِكُمْ هَذَا...» Imekubaliwa.

- Kuwawajibisha washambuliaji kutoka kwa maafisa wa serikali kabla ya wengine, na labda tunakumbuka usemi wa Khalifa Rashid Omar bin Al-Khattab, Mungu amuwiye radhi: "Mliwafanya watu watumwa lini hali mama zao walizaa wakiwa huru?".

- Kusimamisha haki kwa wote, bila ubaguzi au kinga, kwani kutawala kwa kile ambacho Mungu ameteremsha hakumwachi dhalimu yeyote mwenye mamlaka.

Lakini ukweli leo unathibitisha kwamba dola ya Misri inawalinda watesaji, na inawaheshimu kwa kupandishwa vyeo na zawadi, wakati waaminifu, waheshimiwa na wabebaji wa wito wa kutumia Uislamu wanakandamizwa na kufungwa katika kambi za mateso, kesi za uongo zinatungwa dhidi yao na hukumu za dhuluma zinatolewa dhidi yao!

Enyi majeshi ya Kinana: Ninyi ni wasaidizi wa mfumo huu na vyombo vyake, na washirika wake katika dhambi, iwe mlishiriki katika uhalifu au hamkushiriki, mradi tu mmeridhika nao au mmekaa kimya juu yao, kwani alisema ﷺ: «مَنْ أَعَانَ ظَالِماً لِيُدْحِضَ بِبَاطِلِهِ حَقّاً فَقَدْ بَرِئَتْ مِنْهُ ذِمَّةُ الله وَذِمَّةُ رَسُولِهِ» Msiwe fimbo mikononi mwa madhalimu, bali kuweni kama Mungu alivyotaka muwe jeshi linalolinda umma na sio kulishambulia, na linatetea damu yake na sio kuimwaga, na linafanya kazi ya kusimamisha sheria yake na sio kulinda watawala dhalimu.

Inukeni kwa wajibu wenu, na simameni na wajibu wa ushindi, na kuweni wafuasi wa haki, rudisheni Uislamu katika nafasi yake, na Ukhalifa katika uhalisia wake, na haki katika ardhi ambayo imetoweka.

﴿إِنَّ اللهَ يَأْمُرُ بِالْعَدْلِ وَالإِحْسَانِ وَإِيتَاء ذِي الْقُرْبَى وَيَنْهَى عَنِ الْفَحْشَاء وَالْمُنكَرِ وَالْبَغْيِ يَعِظُكُمْ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ

Ofisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir

Katika Wilaya ya Misri

Official Statement

مصر - المكتب

ولاية مصر

مصر - المكتب

Media Contact

مصر - المكتب

Phone:

Email: info@hizb.net

مصر - المكتب

Tel: | info@hizb.net

www.hizb.net

Reference: PR-01985b76-5b20-7c70-9fa6-16e67b5290dd