Taarifa kwa Vyombo vya Habari
"Amani" ni Kificho cha Ukoloni
(Imetafsiriwa)
Kile kinachoitwa makubaliano kati ya taasisi haramu ya Kiyahudi na harakati ya Hamas, ambayo ilitolewa na Washington, inawasilishwa katika vyombo vya habari vya Magharibi, na kwa bahati mbaya pia katika baadhi ya nchi za Waislamu, kama hatua kuelekea amani.
Lakini ukweli ni kwamba sio chochote ila kurudia mtindo wa zamani: mradi wa kikoloni, taasisi ya Kiyahudi, inazidi kuimarishwa na kulindwa, huku uhalifu wake ukifunikwa na vazi la "amani".
Istilahi kama vile "kusitisha mapigano" na "msaada wa kibinadamu" zinaonekana kuwa za upatanishi kwa nje, lakini kwa kweli ni zana mbaya na za kejeli.
Je, tunawezaje kuzungumzia kuhusu misaada, wakati nguvu zinazoandaa misafara ya misaada ndizo zinazotoa mabomu kwa ukoloni na kuupa kifuniko cha kidiplomasia ambacho kimeharibu Gaza?!
Na ni vipi kusitisha mapigano kunaweza kuwa na uaminifu, wakati taasisi ya Kiyahudi imevunja makubaliano mara kwa mara kila inapofaa maslahi yake kufanya hivyo?
Historia iko wazi: miongo kadhaa ya uhamishaji, adhabu za pamoja, na mauaji ya kimbari yaliyofanywa na taasisi ya Kiyahudi, kwa msaada wa Amerika, Magharibi, na tawala za wasaliti katika nchi za Waislamu.
Hakuna haki au fidia iliyotolewa kwa watu wa Palestina, na makubaliano haya hayatakuwa ubaguzi.
Mtindo huu umerudiwa nchini Iraq, Syria, Afghanistan, Libya, Sudan, na nchi nyingine nyingi za Waislamu; ambapo nchi zinaharibiwa chini ya kauli mbiu ya "amani" na "utulivu", huku zikipelekwa kwa kweli kwa uvamizi, mgawanyiko, na machafuko.
Na hivyo kila mtu anabaki mateka wa mzunguko mbaya: makubaliano ya muda yanauzwa kwa ulimwengu kwa jina la "amani", lakini kwa kweli yanapelekea tu kuimarisha uvamizi zaidi.
Taasisi ya Kiyahudi inapata wakati, uhalali, na usalama, huku watu wa Palestina wakiachwa kwa mzingiro, udhalilishaji, na ahadi za uongo.
Amani ya kweli haitatimia kamwe mradi tu dhuluma ya msingi, ambayo ni unyakuzi wa Wayahudi wa Palestina, bado unaendelea.
Suluhisho la kweli pekee liko katika kurudi kwa Palestina kuwa sehemu ya Khilafah, wakati Waislamu wataungana chini ya bendera ya Khalifa mmoja anayetetea maslahi ya Umma na kukomesha mradi wa kikoloni milele.
Kwa muda mrefu mnyanyasaji anazawadiwa, na mnyanyaswa anaombwa kuwa na subira, Palestina itaendelea kusalitiwa kwa jina la "amani", ambayo kwa kweli ni aina mpya ya uvamizi.
Okay Pala
Mwakilishi wa Habari wa Hizb ut Tahrir
Huko Uholanzi