
15/7/2025
Al-Yamamah: Udugu wa kweli hauwezi kuwepo isipokuwa chini ya dola ya Kiislamu ya Khilafah
Ufuatiliaji: Al-Yamamah Press
Chama / Wilaya ya Sudan, kilifanya, saa nne za jioni jana Jumatatu, 19 Muharram 1447 Hijria, sawa na 14/07/2025 Miladia, mhadhara wake wa kisiasa wa kila wiki, mbele ya Hoteli ya Al-Haramain katika Soko Kuu, katika mji wa Port Sudan, ambapo alizungumza Mwalimu Muhammad Jami Abu Ayman, msaidizi wa msemaji rasmi wa Hizb ut-Tahrir katika Wilaya ya Sudan, na mhadhara ulikuwa na kichwa: (Uhusiano wa Kiislamu wa Udugu ndio uhusiano mpya ambao Mtume ﷺ alianzisha baada ya Hijra badala ya uhusiano wa kikabila). Abu Ayman alizungumza juu ya umbo la jamii baada ya kuanzishwa kwa Mtume, swalla Allaahu 'alayhi wa sallam dola katika mji, na jambo la kwanza alilofanya, alikuwa ni kuunganisha kati ya wahajiri na Ansari ambao dini ya Kiislamu iliwakusanya na Uislamu ukaunganisha kati yao, ambapo mawazo yao yalikuwa moja na hisia zao zilikuwa moja, hivyo kupanga uhusiano wao na Uislamu ilikuwa jambo la wazi, na kwa hiyo Mtume, swalla Allaahu 'alayhi wa sallam, alianza kuanzisha mahusiano kati yao kwa misingi ya itikadi ya Kiislamu, na akawalingania kuwa ndugu katika Mwenyezi Mungu, udugu ambao una athari inayoonekana katika miamala yao, mali zao, na masuala yao mengine, na akawafanya kama mwili mmoja. Kisha alizungumza juu ya athari ya udugu huu kwenye mahusiano mapya, na jinsi Ansari walivyoshughulika na ndugu zao wahajiri, na jinsi walivyoacha ushirika wao wa kikabila na wote wakaunganishwa na uhusiano mkuu wa Uislamu ... Mhadhara huu ulikuwa na athari kubwa katika mioyo ya waliohudhuria, ambapo mmiliki wa mgahawa alimletea mzungumzaji maji, na akamletea kiti, kama mmoja wa mama alivyotoa chakula kama heshima kwa mzungumzaji, na kama usemi wa faraja yake kwa yale yaliyosemwa katika mhadhara, na hii ni ishara nzuri kwamba makaa ya imani bado yanawaka katika mioyo ya Waislamu, wanaume na wanawake. Hitimisho lilikuwa kwamba mzungumzaji aliwapa Waislamu habari njema za kurudi kwa Khilafah Rashidah kwa misingi ya unabii ambayo inawaangalia watu kwa msingi wa udugu wa Kiislamu, sio kwa misingi ya kabila, upande au rangi, na kwamba Khilafah pekee ndiyo inayowahamisha watu kutoka hali ya migogoro na mapigano, hadi maisha mazuri, ndugu wanaopendana, na hii haipo katika mifumo mingine, si ya kiraia, si ya kijeshi, si ya kidemokrasia, au nyinginezo. Na alielezea dhana ya kufanya kazi kwa dola hii inayorejea hivi karibuni, kwa idhini ya Mungu, akitoa ushahidi kwa hadithi ya Mtume ﷺ (Mwenye kufa na hana ahadi ya utii shingoni mwake, amekufa kifo cha kijahiliya). Imesimuliwa na Muslim. Na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, Mola wa walimwenguOfisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir katika Wilaya ya Sudan
Chanzo: Al-Yamamah

