Organization Logo

الباكستان مكتب

ولاية باكستان

Twitter: http://twitter.com/HTmediaPAK

Tel:

HTmediaPAK@gmail.com

http://www.hizb-pakistan.com/

Ukosoaji wa Trump kwa India... Maslahi ya Marekani si Urafiki wa Pakistani
Press Release

Ukosoaji wa Trump kwa India... Maslahi ya Marekani si Urafiki wa Pakistani

September 09, 2025
Location

Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Ukosoaji wa Trump kwa India... Maslahi ya Marekani si Urafiki wa Pakistani

Rais wa Marekani Donald Trump alitangaza mnamo Julai 30, 2025 msururu wa ushuru wa kulipiza kisasi dhidi ya India, na kuikosoa kwa kuwa na "vikwazo vya kibiashara visivyo vya kifedha vyenye kuchosha na visivyopendeza," na kuiwekea ushuru wa 25% pamoja na faini. Ingawa Trump alikiri "urafiki" na India, aliikosoa vikali kwa kununua vifaa vya kijeshi vya Urusi na mafuta ya bei rahisi kutoka kwayo, huku Marekani ikiwa inashughulika na kuishinikiza Urusi kukomesha vita nchini Ukraine. Katika karipio la hadharani lisilo la kawaida, Trump alielezea uchumi wa Urusi na India kama "uliokufa" na akaonya Rais wa zamani wa Urusi Medvedev "azungumze kwa uangalifu."

Msimamo huu unaoonekana kupingana wa Rais wa Marekani unathibitisha ukweli kwamba Marekani, iwe inaongozwa na Trump au mtu mwingine, haina rafiki wa karibu isipokuwa maslahi yake. Ikiwa ina urafiki na mtu, ni kwa ajili ya kuhudumia na kufikia maslahi yake maalum, na si kwa mwelekeo kwa upande mwingine. Katika muktadha huu, ni wazi kwamba Trump anafanya kazi kulingana na ukweli huu, lakini kwa tabia ya jambazi wa kimataifa na mnyanyasaji ambaye anadai wateja wake na mataifa yaliyo chini yake kama India na mengineyo kujisalimisha kwake kikamilifu. Anaonyesha sifa za maneno kwa kila mtu anayempendeza na kuinama kwa mapenzi yake, na hasiti kuwadhalilisha na kuwatusi wengine wanaojaribu kumuasi au kuchelewa kuonyesha utii na kujisalimisha kwake kwa sababu ya shinikizo la ndani walilo nalo. Sera hii ya Trump ndiyo sura halisi ya Marekani, kama kiongozi wa kimataifa wa uliberali na ubepari usio na dini. Itikadi hii ndiyo iliyomsukuma Trump katika kipindi cha miezi sita na nusu iliyopita kupata makubaliano bora ambayo yanatumikia tu maslahi ya kiuchumi na kijiografia ya Marekani.

Marekani kwa muda mrefu imechukua China na Urusi kama mahasimu wakuu. Kwa hivyo, inafanya kazi kwa zana zote za shinikizo na mawakala ili kukabiliana na kukwamisha juhudi na sera za makundi ya kimataifa yanayoongozwa na China na Urusi, kama vile kundi la Brazil, Urusi, India, China na Afrika Kusini (BRICS), Shirika la Ushirikiano la Shanghai (SCO), Umoja wa Kiuchumi wa Eurasia (EAEU), Shirika la Mkataba wa Usalama wa Pamoja (CSTO), na mengineyo. Kwa hivyo, Marekani imewekeza sana katika uhusiano wake na India tangu mwishoni mwa miaka ya tisini ili kuitumia kuzuia China. Ushirikiano huu wa kimkakati bado unaendelea hadi sasa, ambapo tawala zake za Republican na Democratic zilizofuatana zimeipa India teknolojia ya hali ya juu ya kijeshi, makubaliano ya nyuklia ya kiraia, na kufungua taasisi za kiuchumi za Magharibi kwa India. Mwelekeo huu si kwa uzuri wa macho ya India, bali ni kuinenepesha na kuitumia kukabiliana na wapinzani wake katika eneo hilo, China na Urusi.

Utawala wa Trump hautabadilisha mwelekeo wa kimkakati kati ya Marekani na India unaolenga kuzuia China, bali unashughulika na India ndani ya sera ya fimbo na karoti. Uwekaji wa ushuru na faini, matamko na uonevu ni fimbo ambayo Trump anatumia dhidi ya mteja wake India ili kufanya juhudi kubwa katika kumtumikia na kufungua uchumi wake wa ndani zaidi ili kuunda fursa kwa makampuni ya Marekani. Katika mchakato huu, Trump pia anatumia Pakistan kuishinikiza India. Hii ndiyo sababu anaonyesha "mwelekeo" kuelekea Pakistan na kumtishia Modi kuhatarisha serikali yake ili kukidhi matakwa yake katika ratiba ya haraka.

Enyi Maafisa Waaminifu katika Vikosi vya Wanajeshi vya Pakistani: Msidanganywe na ukosoaji wa Marekani wa hadharani kwa serikali ya Modi wala sifa ya Trump kwa Pakistan. Dini ya ukafiri ni moja, na Mwenyezi Mungu ameithibitisha kwa kusema: ﴿NA WALE WALIO KUFURU, BAADHI YAO NI MALEZI KWA BAADHI, MSIFANYE HIVYO, LITAKUWA JARIBU DUNIANI NA UHARIBIFU MKUBWA﴾. Ukweli ni kwamba ushirikiano wa kimkakati kati ya Marekani na India bado una nguvu na unalenga Pakistan na Waislamu wa kanda hiyo, wala tusisahau jinsi utawala wa Trump ulivyodanganya utawala wa Iran katika mazungumzo ya nyuklia ili kupanga njia kwa ajili ya taasisi ya Kiyahudi kushambulia vituo vya nyuklia vya Iran. Trump amesema katika mahojiano mengi ya vyombo vya habari huko nyuma kuhusu tishio la silaha za nyuklia za Pakistani na asili yake ya Kiislamu. Pia, Naibu Mshauri wa zamani wa Usalama wa Kitaifa wa Marekani, John Vener, alisema katika hotuba yake katika kituo maarufu cha utafiti cha Marekani mnamo Oktoba 2024 kwamba mfumo wa makombora ya Pakistani ya masafa marefu ni tishio kwa Marekani. Kwa hivyo, taasisi za Marekani na akili zinaendelea kuiona Pakistan kama mahali pa tishio kwao. Na tumeona jinsi utawala wa Trump ulivyotoa msaada wa kidiplomasia kwa shambulio la India dhidi ya Pakistan mnamo Mei 2025 na kuwashinikiza watawala watiifu wa Pakistani kujizuia kukabiliana na uchokozi wa Modi. Lau si ushujaa wa simba wetu na ndege zetu katika vikosi vya wanajeshi ambao walimlazimisha Modi na Trump kushindwa, matokeo yangekuwa mabaya.

Enyi Maafisa katika Vikosi vya Wanajeshi vya Pakistani: Nchi za Waislamu zinapitia hatua muhimu siku hizi, na kiwango cha joto cha mitaani kimefikia kilele chake kutokana na mauaji ya halaiki yanayofanywa na taasisi ya Kiyahudi huko Gaza kwa msaada wa Marekani, ambayo inahitaji kuunganisha nchi za Kiislamu chini ya Ukhalifa ulioongoka. Kikwazo pekee kinachozuia hilo ni kusitasita kwenu kuwaondoa watawala mawakala wa Trump, na kuupa Nusra Hizb ut Tahrir ili kusimamisha Khilafah. Fursa ya kuanzisha Khilafah ipo leo, basi msiikose mkaishia kujuta, mkapoteza utukufu wa dunia na neema za akhera. ﴿MWITIKIE MOLA WENU KABLA HAKI HAIJAFIKA AMBAYO HAIREJESHWI NA ALLAH, HAMTakuwa NA MAHALI PA KUKIMBILIA SIKU HIYO, WALA HAMTAKUWA NA WA KUKATAA﴾.

Ofisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir

Katika Wilaya ya Pakistani

Official Statement

الباكستان مكتب

ولاية باكستان

الباكستان مكتب

Media Contact

الباكستان مكتب

Phone:

Email: HTmediaPAK@gmail.com

الباكستان مكتب

Twitter: http://twitter.com/HTmediaPAK

Tel: | HTmediaPAK@gmail.com

http://www.hizb-pakistan.com/

Reference: PR-0198b2d8-f620-7b48-b494-07706723f9d6