Taarifa kwa Vyombo vya Habari
Taarifa ya rambirambi na pole kwa kifo cha Khalid Ahmed Ibrahim Tarad "Abu Muhammad"
﴿Miongoni mwa Waumini wapo watu waliosadiki yale waliyoahidi kwa Mwenyezi Mungu. Basi wengine wao wamekwisha timiza nadhiri zao,
na wengine wanangojea, wala hawakubadilisha (ahadi yao) hata kidogo.﴾
Ofisi ya habari ya Hizb ut-Tahrir huko Australia inatangaza kifo cha mmoja wa wabebaji wa Da'wah, ambaye ni miongoni mwa watu ambao upendo wao kwa Qur'an, kwa waumini, na kwa Da'wah uligusa mioyo ya wengi katika jamii, Mwenyezi Mungu amrehemu kwa rehema pana: Ndugu Khalid Ahmed Ibrahim Tarad "Abu Muhammad", ambaye amehamia katika rehema ya Mwenyezi Mungu leo, Jumapili 22 Rabi' al-Awwal 1447 Hijria, sawa na 14 Septemba 2025 AD.
Tunatoa pole zetu za dhati kwa familia ya marehemu na kwa wabebaji wote wa Da'wah. Tunamuomba Mwenyezi Mungu Mtukufu amfunike kwa rehema zake pana, amsamehe, na amuweke katika bustani zake pana pamoja na manabii, wasadikifu, mashahidi, na watu wema, na hao ni rafiki wema. Pia tunamuomba Mwenyezi Mungu Mtukufu aipe thawabu familia yake na jamaa zake na awape subira na faraja.
﴿Hakika sisi ni wa Mwenyezi Mungu, na hakika kwake tutarejea.﴾
Ofisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir
Australia