Taarifa kwa Vyombo vya Habari
Enyi Waislamu: Waokoeni watu wa Gaza kabla hawajaangamia kabisa
na tahadharini asije Mwenyezi Mungu akakushukieni kwa ghadhabu na adhabu yake
Taasisi ya Kiyahudi inaendeleza vita vya mauaji ya halaiki dhidi ya Ukanda wa Gaza, ikilenga sehemu mbalimbali za Ukanda huo kwa mashambulizi ya anga na makombora makali, na kusababisha makumi ya watu kuuawa na kujeruhiwa kila siku. Kwa majuma kadhaa, imekuwa ikiongeza mashambulizi yake dhidi ya mji wa Gaza, ambao umejaa watu na wakimbizi kutoka kaskazini mwa Ukanda huo, ikiwa ni maandalizi ya kuuteka tena, ambapo inalenga shule na vituo vya makazi, na inafanya operesheni kubwa za ulipuaji wa vitalu kamili vya makazi, na kuharibu majengo ya makazi, ikiambatana na maonyo kwa watu kuhama kuelekea kusini mwa Ukanda huo.
Zaidi ya siku 700 za vita vya mauaji ya halaiki huko Gaza, ambapo taasisi ya Kiyahudi ilifanya uhalifu mbaya zaidi wa mauaji, uharibifu, uhamishaji na njaa dhidi ya watu wake, ambapo idadi ya mashahidi ilizidi elfu sitini na idadi ya majeruhi ilizidi laki moja kulingana na takwimu za Wizara ya Afya, na idadi ya vifo kutokana na njaa na utapiamlo ilizidi visa 400, wengi wao wakiwa watoto, na Shirika la UNICEF lilionya juu ya kuzorota kwa utapiamlo kwa watoto kwa viwango visivyokuwa vya kawaida, na likathibitisha kwamba vipimo vya hivi karibuni vilionyesha kuwa mtoto mmoja kati ya watano ana utapiamlo mkali. Siku ngumu ambazo watu wa Gaza wanaelezea ukatili na unyama waliokumbana nao wakisema "kana kwamba ni hofu ya Siku ya Kiyama", ambapo damu, vipande vya miili, miili iliyokonda, na sauti za makombora na ulipuaji haziachi mchana na usiku.
Zaidi ya siku 700 ambazo taasisi ya Kiyahudi ilizidi kila kitu kilichosemwa kuwa mistari mekundu, hakuna kinga kwa sheikh, wala kwa mwanamke, wala kwa mtoto, wala hata kwa kijusi tumboni mwa mama yake, na pia hakuna kinga kwa hospitali, wala kwa kituo cha makazi, wala kwa msikiti, wala kwa kanisa, kwa hivyo hakuna mahali salama huko Gaza, na kile ambacho jeshi la Kiyahudi liliamua kama maeneo salama lilishambulia na kufanya mauaji, kiasi kwamba wengi wa wale waliolazimika kuhama kutoka kaskazini mwa Ukanda huo na kutoka mji wa Gaza wamekuwa wakilala chini na kujifunika anga kwa sababu hawana nyumba au hema hata la kuwapa makazi. Pia ilitumia vita vya njaa kuwakandamiza watu na kuwaua katika mitego ya vituo vya misaada vya Marekani, na kauli mbiu zote za haki za binadamu, wanawake na watoto zilianguka na uongo wa wadai wake kutoka nchi na taasisi ulidhihirika.
Enyi Waislamu: Wayahudi wamepitiliza katika uovu wao na wanaendelea kutekeleza mipango yao ya kuua idadi kubwa ya watu wa Gaza na kuwahamisha waliobaki, ili waweze kuendelea kutimiza ndoto zao za Kiyahudi za kuanzisha dola yao kutoka Nile hadi Frati kama vile viongozi wao wanavyotangaza kwa ujasiri wote, na wanaunga mkono migongo yao katika hilo kwa Marekani na rais wake mhalifu jeuri Trump, bali jeuri yao na uhalifu wao umezidi ardhi iliyobarikiwa hadi kufikia Syria, Lebanon, Yemen, Iran na Qatar, na kamba iko juu ya mkokoteni, na katika uhalifu wao huu wanategemea usaliti na njama za watawala wenu, haswa watawala wa nchi zinazowazunguka ambao wanawalinda na kuwabana watu wa Gaza na kuzuia hatua yoyote ya kuwasaidia, kwa hivyo hadi lini kimya hiki juu ya watawala hawa wasaliti wahalifu?! Je, haijafika wakati wa wivu, ulinzi na uungwana kuhamasika katika mioyo na akili za wazalendo katika majeshi ya Waislamu?! Je, hamuwaokoi ndugu zenu kabla hawajaangamia kabisa?! Je, hamuwaokoi na kujiokoa wenyewe kabla ghadhabu na adhabu ya Mwenyezi Mungu haijawashukia kutokana na kimya na udhalilishaji huu?! Mwenyezi Mungu anasema: ﴿Na mkiacha, Atawaleta watu wengine badala yenu, kisha hawatakuwa mfano wenu﴾.
Sehemu ya Wanawake
katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut-Tahrir