Organization Logo

تونس - المكتب الإعلامي

ولاية تونس

Tel: 71345949

Fax: 71345950

http://www.ht-tunisia.info/ar/

Huko Gabes: Janga la kimazingira na kibinadamu... na adhabu ya pamoja dhidi ya vizazi
Press Release

Huko Gabes: Janga la kimazingira na kibinadamu... na adhabu ya pamoja dhidi ya vizazi

October 22, 2025
Location

Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Huko Gabes: Janga la kimazingira na kibinadamu... na adhabu ya pamoja dhidi ya vizazi

Mji wa Gabes unakumbwa na janga kubwa, ambalo linaua pumzi zake polepole kutokana na mzozo wa kimazingira unaotokana na utoaji wa hewa chafu kutoka kwa kiwanda cha kemikali.

Wakati wakazi bado wanamngoja gavana ambaye hajaja kukomesha madhara makubwa yaliyowapata, badala yake msafara wa vitengo vya usalama ulikuja kukandamiza maandamano ya amani ya watoto, wanawake na wazee, waliwakabili kwa mabomu ya machozi!

Pia, polisi iliwakamata zaidi ya watu 70 ndani ya saa za usiku wa Ijumaa, na idadi iliongezeka kufikia alfajiri, ambapo baadhi yao walichukuliwa kutoka majumbani mwao, kama ilivyoonyeshwa na Khair El-Din Debiya, mwanachama wa kampeni ya "Simamisheni Uchafuzi", ambapo baadhi yao walipelekwa mahakamani wakiwa wamewasilishwa na wengine walihamishiwa gerezani, na hivyo kubadilisha madai ya waandamanaji kutoka kusimamisha uchafuzi hadi kuachiliwa kwa wafungwa!

Kutokana na maendeleo haya, sisi katika ofisi ya habari ya Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Tunisia tunathibitisha yafuatayo:

1- Madai ya waandamanaji ya kuvunja na kufunga vitengo vya viwanda vinavyochafua, ni madai halali ambayo mamlaka lazima itii mara moja, na hali ni kwamba uamuzi wa kuvunja vitengo ulitolewa tangu 2017, na baraza la mitaa huko Gabes tayari limeonya kuwa vitengo hivi vinatishia maisha moja kwa moja.

2- Matumizi ya vurugu na ukamataji hayatazidisha hali isipokuwa mvutano, na yanafunua tena kushindwa kwa watawala wetu na kunyang'anywa kwao mamlaka mbele ya wajibu rahisi zaidi wa utunzaji, kwani wanakimbilia kutumia fimbo ya mamlaka na kukataa haki halali za watu za kuishi kwa heshima.

Enyi watu wetu katika Tunisia ya kijani kibichi:

Uchafu unaozunguka mazingira yetu ni matokeo ya asili ya mfumo wa kibepari wenye pupa ambao unajali faida na uzalishaji mwingi, na kinachotokea leo huko Gabes sio ubaguzi, lakini ni mfano wa uchafuzi unaotokana na gesi asilia huko Kairouan, taka za nyuklia huko Douz, tatizo la taka huko Sfax, na miradi ya hidrojeni ya kijani katika siku za usoni.

Tatizo la mazingira haliwezi kutatuliwa kabisa isipokuwa chini ya ukhalifa ulioongoka kwa mfumo wa unabii, dola ambayo ina uamuzi wake na inasimamia matendo yake na mizani ya sheria, hivyo kumcha Mungu katika nchi na watu na kukata mkono wa ukoloni kwa kufuta makubaliano ya kimataifa ambayo yanaimarisha utegemezi na kunyakua utajiri na unyonyaji wa rasilimali kwa gharama ya watoto wetu na mazingira yetu.

Kutoka kwa Abu Dharr, Mwenyezi Mungu amuwiye radhi, kwamba Nabii ﷺ alisema: «Umma wangu ulionyeshwa kwangu na matendo yake, mazuri yake na mabaya yake, nikaona katika uzuri wa matendo yake kile kinachoondoa uchafu njiani, na nikaona katika ubaya wa matendo yake makohozi msikitini ambayo hayazikwi».

Ofisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir

Katika Wilaya ya Tunisia

Official Statement

تونس - المكتب الإعلامي

ولاية تونس

تونس - المكتب الإعلامي

Media Contact

تونس - المكتب الإعلامي

Phone: 71345949

Fax: 71345950

Email:

تونس - المكتب الإعلامي

Tel: 71345949 |

Fax: 71345950

http://www.ht-tunisia.info/ar/

Reference: PR-019a0470-9758-7930-93a1-c7c68ddd759d