Organization Logo

السودان - مكتب - ناطق

ولاية السودان

الخرطوم شرق- عمارة الوقف الطابق الأرضي -شارع 21 اكتوبر- غرب شارع المك نمر

Tel: 0912240143- 0912377707

spokman_sd@dbzmail.com

www.hizb-ut-tahrir.info

Serikali ya Muungano wa Uanzilishi ni hatua ya juu katika kuharakisha mpango wa Marekani wa kuitenga Darfur
Press Release

Serikali ya Muungano wa Uanzilishi ni hatua ya juu katika kuharakisha mpango wa Marekani wa kuitenga Darfur

July 29, 2025
Location

Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Serikali ya Muungano wa Uanzilishi ni hatua ya juu katika kuharakisha mpango wa Marekani wa kuitenga Darfur

Kikosi cha Msaada wa Haraka, kupitia muungano wake unaoitwa Muungano wa Uanzilishi wa Sudan "Uanzilishi," Jumamosi, 2025/7/26 BK, kilitangaza uteuzi wa rais na makamu wa rais wa baraza la urais, na waziri mkuu, ambayo inamaanisha kuunda serikali sambamba na mamlaka inayoendeshwa na jeshi kutoka Port Sudan, mashariki mwa nchi.

Muungano huo una mashirika ya kijeshi, kisiasa na kiraia, muhimu zaidi kati yao ni Kikosi cha Msaada wa Haraka, na Vuguvugu la Wananchi - Kaskazini, ambapo mkataba wake wa msingi ulisainiwa mwezi Februari uliopita, katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi.

Sisi katika Hizb ut-Tahrir / Wilaya ya Sudan tumekuwa tukifichua mpango wa Marekani kila wakati, na tunawaonya watu wa Sudan kwamba vita nchini Sudan vina ajenda ya kikoloni ya kuirarua Sudan, ikisimamiwa na kichwa cha uovu, Amerika, kupitia vibaraka wake kutoka kwa viongozi wa jeshi, na viongozi wa Kikosi cha Msaada wa Haraka. Kama vile serikali ya al-Bashir ilivyotenganisha kusini mwa Sudan, kwa kushirikiana na Vuguvugu la Wananchi, lililoongozwa na marehemu John Garang, ndivyo serikali ya al-Burhan leo na Kikosi cha Msaada wa Haraka, wanavyoendesha suala la Darfur kwa mpango huo huo, kupitia uondoaji wa kutiliwa shaka, na kukabidhi kambi za jeshi na miji kwa Kikosi cha Msaada wa Haraka, na kutochukua hatua kwa majeshi, wala ndege kukomesha uasi wake! Huku tukijua kuwa jeshi nchini Sudan lina uwezo wa kukomesha vita, na kukomboa nchi na watu, ikiwa hatamu itafunguliwa kutoka kwa yule anayeishikilia.

Al-Bashir alikiri hapo awali kwamba alipitisha kulirarua eneo la kusini kwa shinikizo la Marekani, akisema: "Kujitenga kwa kusini kulikuwa kwa shinikizo la Marekani, na kwamba mpango wa Marekani ni kuigawa Sudan katika nchi tano." (Tovuti ya Sputnik ya Urusi).

Na baada ya hapo kukaja kukiri kwa nguzo za utawala wake, na mawaziri wake wa mambo ya nje, ambayo inamaanisha kwamba walikuwa wanajua mpango huo, na wanautekeleza, na leo hali hiyo inajirudia huko Darfur, kwa kupanga kuitenga kupitia Kikosi cha Msaada wa Haraka, ambacho kilisimamiwa kuimarishwa na kamanda wa jeshi, al-Burhan.

Kwa hakika inasikitisha sana, kwamba kichwa cha uovu, Amerika kafiri mkoloni, kinaweza kusimamia mapigano yanayovuna roho nchini Sudan, kupitia vibaraka wake; ambao wanatekeleza mpango huo hadharani sio kwa siri, na kwa uwazi sio kwa kificho, wakisaidiwa na vyombo vya habari vinavyoshirikiana, vinavyopotosha, na wanasiasa mamluki ambao hawana lengo lingine isipokuwa viti vilivyochakaa, wanakaa juu yao, na kafiri mkoloni anaviendesha.

Kuirarua nchi za Waislamu ni uhalifu mkubwa, ambao kila anayeshiriki ndani yake atachukua dhambi yake, Nabii ﷺ anasema kumhusu Arfaja bin Asad: «Yeyote anayekujieni hali yenu ikiwa imekusanyika juu ya mtu mmoja, akitaka kuigawa fimbo yenu, au kueneza kundi lenu, basi muuweni» Imesimuliwa na Muslim. Na Muslim amesimulia kutoka kwa Abu Saeed al-Khudri akisema kwamba Nabii ﷺ alisema: «Pindi khalifa wawili wanapochaguliwa, basi muuweni yule wa mwisho kati yao», jambo ambalo linasisitiza ulazima wa kuhifadhi umoja wa umma, na kutotawanyika kwake.

Kwa msingi huo, sisi katika Hizb ut-Tahrir / Wilaya ya Sudan, tunawahimiza watu waaminifu kutoka kwa maafisa wa jeshi, na watu wa nguvu na ulinzi, kusimamisha uhalifu huu mbaya, na kuizuia Amerika, na nchi zote za kikoloni na zana zake, kutekeleza mipango yake mibaya katika nchi yetu, na kuunga mkono mradi mkuu wa umma, kwa kusimamisha Khilafah Rashidah kwa njia ya Utume; ndio njia pekee ya kutoka na ukombozi.

Nabii ﷺ anasema: «... Kwani yeyote atakayeishi miongoni mwenu ataona tofauti nyingi, hivyo basi shikamaneni na Sunnah zangu na Sunnah za Makhalifa Waongofu walioongoka, zishikilieni kwa nguvu na ziumeni kwa magego».

Ibrahim Othman (Abu Khalil)

Msemaji Rasmi wa Hizb ut-Tahrir katika Wilaya ya Sudan

Official Statement

السودان - مكتب - ناطق

ولاية السودان

السودان - مكتب - ناطق

Media Contact

السودان - مكتب - ناطق

Phone: 0912240143- 0912377707

Email: spokman_sd@dbzmail.com

السودان - مكتب - ناطق

الخرطوم شرق- عمارة الوقف الطابق الأرضي -شارع 21 اكتوبر- غرب شارع المك نمر

Tel: 0912240143- 0912377707 | spokman_sd@dbzmail.com

www.hizb-ut-tahrir.info

Reference: PR-01984df3-3040-7397-85de-29c00b2d13a2