Organization Logo

القسم النسائي في المكتب الإعلامي المركزي

المركزي

Tel: 0096171724043

Fax: 009611307594

ws-cmo@hizb-ut-tahrir.info

http://www.hizb-ut-tahrir.info/

"Vita ya Kiitikadi ya Hijabu" Ni Mwangwi wa Kisasa wa Ukoloni wa Ulaya Unatumika Kupuuza Mauaji ya Kimbari huko Gaza na Kuwanyima Wanawake Waislamu Utambulisho wao wa Kiislamu
Press Release

"Vita ya Kiitikadi ya Hijabu" Ni Mwangwi wa Kisasa wa Ukoloni wa Ulaya Unatumika Kupuuza Mauaji ya Kimbari huko Gaza na Kuwanyima Wanawake Waislamu Utambulisho wao wa Kiislamu

October 25, 2025
Location

Taarifa kwa Vyombo vya Habari

"Vita ya Kiitikadi ya Hijabu" Ni Mwangwi wa Kisasa wa Ukoloni wa Ulaya

Inatumika Kupuuza Mauaji ya Kimbari huko Gaza na Kuwanyima Wanawake Waislamu Utambulisho wao wa Kiislamu

(Imetafsiriwa)

Leo, uwanja wa kisiasa unashuhudia vita mpya vya kiitikadi vinavyoendeshwa na vyama vya siasa za mrengo wa kulia na serikali za kidemokrasia zinazotoa wito wa kupigwa marufuku kwa hijabu, na Australia, Italia na Ureno zimejiunga na wimbi hili. Nchi hizi ni sehemu ya kundi pana la nchi za Ulaya ambazo tayari zimepiga marufuku hijabu, huku Ufaransa, Ubelgiji, Denmark na Uswizi zikiwa tayari zimeweka marufuku kamili ya hijabu katika maeneo yote ya umma, wakati Uholanzi na Ujerumani zina marufuku ya sehemu katika maeneo maalum kama vile taasisi za elimu na idara za serikali. Huko Uingereza, mjadala unazingatia mahali pa kazi na wafanyikazi, ambapo vyama vya mrengo wa kulia kama vile Chama cha Mageuzi cha Uingereza vinadai kuwa hijabu inazuia ujumuishaji, mawasiliano na usalama, na kuielezea kama ishara ya mgawanyiko.

Vita hivi dhidi ya hijabu si jambo la kisasa, bali ni sura mpya katika historia ndefu ya uadui wa Magharibi usio wa kidini dhidi ya Uislamu na Waislamu. Uadui huu wa kihistoria uliokita mizizi unatumiwa kama chombo cha kukengeusha umakini kutoka kwa mzozo mkubwa wa kiuchumi unaoikumba jamii za Magharibi zisizo za kidini kutokana na kushindwa kwa mfumo wa kibepari wa kimataifa.

Vyama vya mrengo wa kulia kama vile Chama cha One Nation kinachoongozwa na Pauline Hanson huko Australia, Chama cha Brothers of Italy kinachoongozwa na Giorgia Meloni, na Chama cha Chega kinachoongozwa na André Ventura huko Ureno, vinatumia hijabu kama ishara ya kuwadharau wanawake Waislamu, kulazimisha ujumuishaji wao wa kulazimishwa katika jamii, na kugeuza umakini wa umma kutoka kwa migogoro halisi inayotokana na kushindwa kwa serikali.

Mjadala huu wa karne nyingi kuhusu mavazi ya mwanamke Mwislamu unakumbusha kile kilichojulikana kama "misheni ya ustaarabu" ya kikoloni ya Ulaya na mgongano wa ustaarabu, lakini kwa toleo la kisasa linalolenga hadhira ya karne ya ishirini na moja ambayo imechoshwa na mifumo ya kibepari iliyofilisika na yenye upendeleo. Hii ni mkakati uliopangwa unaolenga kugeuza mateso halisi ya kiuchumi kuwa vita bandia dhidi ya Uislamu na Waislamu.

Pia, kile kinachojulikana kama "utetezi wa wanawake wa kitaifa," ambacho ni matumizi ya wanasiasa ya hotuba ya haki za wanawake kuhalalisha sera za chuki dhidi ya Uislamu kama vile kupiga marufuku hijabu, inazalisha upya hotuba ya kikoloni ya kimashariki ambayo iliwaonyesha nchi za Kiislamu na wanawake Waislamu kama wameachwa nyuma, wanatishia, na wanahitaji kuokolewa.

Mapendekezo ya kupiga marufuku hijabu nchini Italia na Australia yanalenga haswa wanawake Waislamu, ambao tayari ni waathiriwa wakuu wa mashambulizi ya chuki dhidi ya Uislamu.

Huko Australia, data kutoka kwa rekodi ya chuki dhidi ya Uislamu ya Australia, ripoti ya kila mwaka ya 2024, inaonyesha kuwa 75% ya mashambulizi ya chuki dhidi ya Uislamu yanalenga wanawake na wasichana. Vile vile, data kutoka kwa Shirika la Haki za Msingi la Umoja wa Ulaya inaonyesha kuwa 65% ya Waislamu nchini Italia wanabaguliwa, na wanawake ndio wanaolengwa zaidi.

Wakati huo huo, nchini Ureno, uzushi wa chuki dhidi ya Uislamu unaongezeka kwa kiasi kikubwa, na unahusiana moja kwa moja na kupanda kwa chama cha mrengo wa kulia cha Chega kinachoongozwa na André Ventura, ambaye anaonyesha Uislamu kama tishio kwa utambulisho wa Ureno na Magharibi ya Kikristo. Kuweka marufuku kwa hijabu katika nchi hizi kutahalalisha kisheria chuki zile zile ambazo wanawake Waislamu tayari wanateseka nazo.

Zaidi ya hayo, unafiki wa kisiasa wa vyama vya mrengo wa kulia hauwezi kupuuzwa, ambavyo vinazungumzia kuhusu mavazi ya wanawake Waislamu wakati nchi zao zinashuhudia mzozo mbaya wa vurugu za kiume dhidi ya wanawake:

  • Huko Australia, mwanamke anauawa na mpenzi wake karibu kila wiki (Taasisi ya Australia ya Uhalifu, 2023-2024).
  • Nchini Italia, mwanamke anauawa kila baada ya siku tatu, kuashiria mzozo wa aibu (Wizara ya Mambo ya Ndani ya Italia, 2024).
  • Nchini Ureno, unyanyasaji wa nyumbani unachukuliwa kuwa uhalifu uliripotiwa zaidi, huku wanawake wakiwa ni 85% ya wahasiriwa.

Kupuuza migogoro hii ya kibinadamu, huku hatari ya kipande cha nguo ikikuzwa na kuchukuliwa kuwa tishio la usalama, kunaonyesha unafiki mbaya wa wale wanaodai kuwalinda wanawake.

Kupiga marufuku hijabu ni chaguo la makusudi kutoka kwa tabaka la kisiasa kupuuza masuala halisi ya kibinadamu ambayo yanashughulisha maoni ya umma. Wakati mamia ya maelfu ya watu waliandamana - kwenye Daraja la Sydney Harbour huko Australia, katika viwanja vya Italia, na mitaa ya Lisbon - kupinga mauaji ya kimbari dhidi ya Waislamu huko Gaza, yaliyofanywa na taasisi haramu na ya uhalifu ya Kiyahudi, wanasiasa walichagua badala yake kupigana vita vya kitamaduni kulingana na dichotomy "sisi dhidi yao."

Shambulio hili la moja kwa moja dhidi ya mavazi ya mwanamke Mwislamu, ambalo linatumia hotuba ya usalama wa taifa kuonyesha hijabu kama tishio la kiuwepo kwa usalama, utambulisho wa kitaifa na maadili ya kilimwengu, husababisha uhalalishaji wa mradi wa kulazimishwa wa ujumuishaji wa kulazimishwa, na kuwalazimisha wanawake Waislamu kuachana na utambulisho wao wa Kiislamu na kuzingatia utambulisho wa kitaifa wa kilimwengu.

Sisi Waislamu, lazima tushikamane na imani yetu ya Kiislamu, na tukumbuke ahadi ya Mwenyezi Mungu ya malipo makubwa kwa wenye subira wanaosimama imara katika dini yao wakati wa dhiki na majaribu. Mwenyezi Mungu amesema: ﴿Hakika wale walio sema: Mola wetu ni Mwenyezi Mungu, kisha wakasimama sawa sawa, basi hawana khofu wala hawatahuzunika. Hao ndio watu wa Peponi, watadumu humo, ni malipo ya yale waliyo kuwa wakiyatenda.﴾.

Sehemu ya Wanawake

Katika Afisi Kuu ya Habari

ya Hizb ut-Tahrir

Official Statement

القسم النسائي في المكتب الإعلامي المركزي

المركزي

القسم النسائي في المكتب الإعلامي المركزي

Media Contact

القسم النسائي في المكتب الإعلامي المركزي

Phone: 0096171724043

Fax: 009611307594

Email: ws-cmo@hizb-ut-tahrir.info

القسم النسائي في المكتب الإعلامي المركزي

Tel: 0096171724043 | ws-cmo@hizb-ut-tahrir.info

Fax: 009611307594

http://www.hizb-ut-tahrir.info/

Reference: PR-019a1646-a580-7a14-984f-cda566f0f268