Habari kwa Vyombo vya Habari
Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Sudan
Waandaa Msimamo Mbele ya Msikiti wa Kale Katika Mji wa Port Sudan Kuinusuru Gaza
Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Sudan, leo Ijumaa 07 Safar 1447 Hijria, sawia na 2025/08/01 Miladia, wameandaa msimamo mbele ya Msikiti wa Kale katika mji wa Port Sudan baada ya Swala ya Ijumaa, ambapo vijana wa Hizb walibeba mabango yenye (hashtag: Angusheni viti vya enzi vinavyozuia harakati za majeshi kuinusuru Gaza), na yaliyoandikwa:
ـ ﴿Na wakiomba msaada kwenu katika dini, basi ni juu yenu kuwasaidia﴾.
ـ Mpaka lini mtaendelea kuwaangusha ndugu zenu huko Gaza na hali Mwenyezi Mungu atawauliza juu yao?!
ـ Lau tungekuwa na Khalifa, angetutangazia kwamba yeyote anayesikia na kutii, basi asisali Alasiri isipokuwa huko Palestina.
ـ Enyi Umma wa mabilioni mawili: Je, mnakubali vifo vya watu wa Gaza kwa mapipa, makombora na njaa huku mmezingirwa?!
ـ Je, kuna uhalifu mkuu kuliko kubaki kwa majeshi kwenye kambi na hali chombo cha Kiyahudi kinawachinja wanawake, watoto na wazee wetu?!
ـ Enyi Umma wa mabilioni mawili: Simamisheni Khilafah ili muweze kuikomboa Gaza na ardhi zote za Waislamu zilizokaliwa.
ـ Chombo cha Kiyahudi ni kivuli cha tawala zilizopo katika nchi za Waislamu, kikiondoka kitu, kivuli chake huondoka.
ـ Waislamu ni mkono mmoja dhidi ya wengine, vipi mnawakabidhi ndugu zenu huko Gaza kwa adui yenu?!
ـ Angusheni viti vya enzi vilivyochakaa vya vibaraka na simamisheni Khilafah ili muweze kuwanusuru ndugu zenu.
ـ Hakika Waumini ni ndugu, basi nendenikawanusuru ndugu zenu huko Gaza, ikiwa nyinyi ni Waumini.
Na msemaji rasmi wa Hizb ut-Tahrir katika wilaya ya Sudan, alihutubia makundi ya waumini, walipokuwa wakitoka msikitini, ambapo waliitikia msimamo huo, na hotuba kwa takbira na tahlili, na wakaonesha mshikamano wao na kadhia ya Waislamu huko Palestina, na wakangoja hadi mwisho wa msimamo licha ya joto kali la hali ya hewa.
Ibrahim Othman (Abu Khalil)
Msemaji Rasmi wa Hizb ut-Tahrir
Katika Wilaya ya Sudan
{gallery}2025_08_01_Sudan_OS_2_Pics.{/gallery}