Taarifa kwa Vyombo vya Habari
Kupiga Marufuku Hizb ut-Tahrir ni Ufilisi wa Kidemokrasia
(Imetafsiriwa)
Baada ya kampeni mbaya ya kumharibia sifa mmoja wa vijana wetu, iliyoanzishwa na vyombo vya habari na wanasiasa - ikitegemea tu itikadi zake na maadili ya Kiislamu - vyama vitatu katika serikali ya Denmark vilifanya upya wito wao wa kisiasa wa kupiga marufuku Hizb ut-Tahrir nchini Denmark. Hii si mara ya kwanza kwa wanasiasa wa Denmark kutumia "karatasi ya marufuku" kwa msukumo wa kukata tamaa. Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma, katika matukio matatu tofauti, alihitimisha kuwa hakuna msingi wa kikatiba kwa marufuku kama hiyo.
Hizb ut-Tahrir inajulikana ulimwenguni kote kwa kutotumia vurugu, bali inategemea kazi ya kisiasa na kiakili tu. Ukweli huu haubadilishi hukumu za kisiasa dhidi ya idadi ya vijana wetu kwa wito wao wa wazi wa ukombozi wa Palestina. Kinyume chake! Kila wakati hamu ya kisiasa ya kutupiga marufuku inapozuka, serikali mfululizo za Denmark zinakaribia marafiki na washirika wao katika nchi za mateso, ambapo wapinzani wa kisiasa na watu wenye maadili tofauti wanateswa kwa sababu ya imani na misemo yao. Ni serikali hizi haswa za kidikteta katika nchi za Kiislamu ambazo Hizb ut-Tahrir inataka kuziangusha ili kuanzisha Dola ya Kiislamu; Ukhalifa, kulingana na itikadi na historia ya watu wa Kiislamu katika nchi za Kiislamu pia.
Uongo kwamba tunafanya kazi ya kuangusha jamii ya Denmark umekanushwa mara nyingi sana, na mikanusho hii haihitaji juhudi nyingi kugundua na kuthibitisha. Tafsiri pekee inayowezekana ni kwamba wanasiasa hawa, kinyume na kile wanachokijua vizuri, huchochea kwa makusudi chuki na hofu ili kuwakandamiza Waislamu wanaoshiriki katika jamii ambao wanakataa kujisalimisha kwa ulimwengu, kupitia marufuku na kulazimisha.
Hii inaweka wazi unafiki mkubwa wa vyombo vile vile vya kisiasa ambavyo, kwa vizazi, vimekuwa vikiwaonya Waislamu kuvumilia kila aina ya uchochezi na sheria za kibaguzi kwa jina la "uhuru wa kujieleza". Wakati huo huo, hii inaangazia ubatili na udhaifu wa maadili ya Magharibi ya kilimwengu ambayo hayasimami changamoto ya maoni na mawazo ya Kiislamu. Inaonekana kwamba katiba, mgawanyo wa madaraka, na kanuni ya uhuru wa kujieleza, zote ni vikwazo vya kusumbua kwa wanasiasa hawa ambao hawana jibu kwa maadili ya Uislamu isipokuwa majaribio ya vitisho.
Na hivyo, demokrasia ya kilimwengu ya kiliberali inatia saini tamko lake la kufilisika. Ambapo nguvu kamili ya mamlaka ya serikali, wala propaganda na uwongo wa mashine za vyombo vya habari, hazijafaulu kuwashawishi Waislamu kuacha maadili yao kwa ajili ya yale yanayokuzwa na watawala wa Christiansborg na Berlingske Media.
Lakini hili halishangazi. Ni mtu gani mwadilifu angetaka kushikamana na maadili ambayo yanahalalisha utakaso wa kikabila, njaa ya pamoja ya raia, na mauaji ya kimbari?!
Hakuna mtu atakayetuweka chini ya adhabu au marufuku na hakika sio wanafiki hawa wasio na thamani, wanaounga mkono mauaji ya kimbari. Kazi yetu inaendelea kwa mafanikio, kwa sifa zote ni za Mwenyezi Mungu.
Elias Lamrabet
Mwakilishi wa Vyombo vya Habari wa Hizb ut-Tahrir nchini Denmark