Taarifa kwa Vyombo vya Habari
Haki na uhalifu wa taasisi ya Kiyahudi katika Gaza na Yemen hautaweza kusimamishwa
ila na Ukhalifa Rashidah wa Pili kwa msingi wa Utume, mlinzi wa Waislamu
Jana Jumatatu, 2025/09/01M, miili ya Waziri Mkuu na Mkuu wa Serikali ya Mabadiliko na Ujenzi huko Sana'a, Ahmed Ghaleb Nasser Al-Rahwi, ilisafirishwa pamoja na kundi la mawaziri, ambao ni Jaji Mujahid Ahmed Abdullah Ali - Waziri wa Sheria na Haki za Binadamu, Moin Hashem Ahmed Al-Mahaqari - Waziri wa Uchumi, Viwanda na Uwekezaji, Radwan Ali Ali Al-Rubaie - Waziri wa Kilimo, Uvuvi na Rasilimali za Maji, Jamal Ahmed Ali Amer - Waziri wa Mambo ya Nje na Wahamiaji, Ali Saif Mohammed Hassan - Waziri wa Umeme, Nishati na Maji, Ali Qassem Hussein Al-Yafie - Waziri wa Utamaduni na Utalii, Samir Mohammed Ahmed Bajaalah - Waziri wa Masuala ya Kijamii na Kazi, Hashem Ahmed Abdul Rahman Sharaf Al-Din - Waziri wa Habari, Mohammed Ali Ahmed Al-Mawlid - Waziri wa Vijana na Michezo, Mohammed Qassem Al-Kabsi - Mkurugenzi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Zahed Mohammed Al-Amadi, Katibu wa Baraza la Mawaziri, huku hatima ya mawaziri wengine waliokuwa kwenye mkutano haikutajwa; baada ya kulengwa alasiri ya Alhamisi iliyopita, 2025/08/28M, na uchokozi wa taasisi ya Kiyahudi dhidi yao katika mji mkuu, Sana'a, wakati wa mkutano wao siku nne baada ya kulenga kampuni ya mafuta, na kituo cha umeme cha Hazir.
Haiwezekani kwa wale ambao Mwenyezi Mungu amewadhalilisha kuweza kuvamia nchi zetu isipokuwa wanapokuwa na uhakika wa kuwepo kwa watawala vibaraka ambao wanawafungulia njia, na ndege zao zinaondoka juu ya Bahari Nyekundu kwenye ufuo wake wa kulia, Salman bin Abdulaziz, na kwenye ufuo wake wa kushoto, Sisi na Al-Burhan, bali zinaondoka kutoka visiwa vyake na kutoka visiwa vya Yemen ambavyo wanashirikiana navyo katika vituo vyake, Imarati za Mohammed bin Zayed, na wengine kutoka kwa watawala wa Waislamu, na wale wanaowaunga mkono, na kufanya kile walichokifanya cha uchokozi dhidi ya nchi za Waislamu, lau si ushirikiano wa watawala hawa na kuegemea kwao kwenye dunia katika kukabiliana na taasisi hii iliyoporwa ya Palestina tangu 1948, na uvivu wao katika kukabiliana nayo, na ujasiri wao dhidi ya watu wao wanapopinga uchafu wa matendo yao maovu.
Kulengwa kwa Yemen na taasisi ya Kiyahudi hakungeweza kufanyika isipokuwa katika kivuli cha kukosekana kwa hukumu kwa Uislamu, na kuchukua Sheria ya Kimataifa inayowakilishwa na Umoja wa Mataifa, na wale wanaoiunga mkono, kama Qibla kwao, na thawabu kwa wale wanaokataa hukumu kwa Uislamu, ni matokeo ya asili, mpaka wanasiasa wa Yemen warudi kwenye akili zao, na kuweka Uislamu mahali pa utekelezaji katika kivuli cha dola ya Ukhalifa Rashidah wa Pili kwa msingi wa Utume, Mwenyezi Mungu alisema: ﴿Hakika tutawasaidia Mitume wetu na wale walioamini katika uhai wa dunia na siku itakayosimama ushahidi﴾, na Mtume ﷺ alisema: «Kisha kutakuwa na Ukhalifa kwa msingi wa Utume» Ukhalifa unaohukumu kwa Uislamu, na unaunganisha nchi za Waislamu, na unaangamiza taasisi ya Kiyahudi kutoka mizizi yake, kwa msafara wa majeshi ya Waislamu, baada ya uovu wake kwa karibu miaka themanini, na si kuilenga tu kwa makombora kutoka mbali! Na bila ya haya, taasisi hiyo ya uhalifu itaendelea na vitendo hivi vya uhalifu.
Hakika Mwenyezi Mungu ametutukuza kwa Uislamu na akatuheshimu nao na akatuteremshia sheria inayotatua matatizo yote ya dunia na kuieleza njia ya uongofu, basi tunawezaje kuibadilisha na sheria ya kibinadamu dhalimu (Sheria ya Umoja wa Mataifa) ambayo kanuni zake zimeundwa na makafiri wakoloni?! Hakika dunia leo inatushambulia kwa upinde mmoja, basi tunapaswa kuzingatia kile ambacho Mola wetu amesema na kutumia Uislamu kikamilifu bila kupunguzwa na kuongoza makundi ya umma kuelekea ukombozi wa nchi za Waislamu na ubinadamu wote kutoka kwa dhuluma ya ubepari. Na sisi katika Hizb ut Tahrir tunaendelea na kazi yetu ya kuhamasisha umma na kutafuta nusra kutoka kwa watu wa nguvu na ulinzi na kubeba mradi safi wa Kiislamu mpaka Mwenyezi Mungu atutukuze kwa ushindi na ufunguzi kwa kusimamisha Ukhalifa Rashidah wa Pili kwa msingi wa Utume, na tunawaalika kufanya kazi nasi ili kusimamisha faradhi hii kubwa.
Mwenyezi Mungu alisema: ﴿Enyi mlio amini! Muitikieni Mwenyezi Mungu na Mtume anapo kuwaiteni kwenye lile linalo kuhuisheni. Na jueni kwamba Mwenyezi Mungu huingilia baina ya mtu na moyo wake, na kwamba kwake Yeye mtakusanywa﴾.
Ofisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilaya ya Yemen