Organization Logo

المكتب الإعلامي ماليزيا

ماليزيا

Khilafah Centre, 47-1, Jalan 7/7A, Seksyen 7, 43650 Bandar Baru Bangi, Selangor

Tel: 03-89201614

htm@mykhilafah.com

www.mykhilafah.com

Majanga Mawili Yanayoikumba Umma wa Kiislamu: Watawala Wabaya na Mfumo Mbaya, na Lazima Yabadilishwe Mara Moja
Press Release

Majanga Mawili Yanayoikumba Umma wa Kiislamu: Watawala Wabaya na Mfumo Mbaya, na Lazima Yabadilishwe Mara Moja

August 02, 2025
Location

Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Majanga Mawili Yanayoikumba Umma wa Kiislamu: Watawala Wabaya na Mfumo Mbaya, na Lazima Yabadilishwe Mara Moja

(Imetafsiriwa)

Mnamo Julai 26, 2025, jiji la Kuala Lumpur lishuhudia maandamano ya wananchi ambayo hayajawahi kushuhudiwa, yakidai kujiuzulu kwa Waziri Mkuu wa Malaysia, Datuk Seri Anwar Ibrahim. Maandamano haya yalionyesha hasira ya watu na kuchanganyikiwa kunakoongezeka dhidi ya uongozi ambao haukushindwa tu kutimiza ahadi zake za mageuzi, lakini ulizidisha mateso ya watu kwa kuongeza kodi, kuongeza ushuru wa umeme, na kupanda kwa bei za bidhaa muhimu.

Hasira za watu zinaendelea kuongezeka kwa sababu ya kile kinachoonekana sana kama unafiki wa Anwar. Ahadi yake ya kukomesha ufisadi inapingana kabisa na kuendelea kwake kuwalinda na kuwakuza wafisadi. Zaidi ya hayo, ziara zake za mara kwa mara na za gharama kubwa za nje - ambazo mara nyingi huzihalalisha na ahadi za mabilioni ya dola za uwekezaji wa kigeni - zimekuwa kauli mbiu tupu bila matokeo yoyote halisi.

Ingawa upinzani umefanikiwa kuchochea hasira hii ya umma kwa kuandaa maandamano, umeshindwa kutoa mbadala halisi kwa mtawala. Haijatolewa wazi nani atamrithi Anwar ikiwa ata jiuzulu kweli. Mtazamo bado ni finyu, ukilenga tu kumwondoa Waziri Mkuu, bila kutoa njia ya kuaminika ya kusonga mbele, na kwa bahati mbaya watu bado wanakusanywa kwa kuzingatia hisia badala ya kufikiri kisiasa timamu na suluhisho bora. Simulizi hili la juu juu - kwamba tatizo liko kwa Anwar Ibrahim - ndilo linalowapotosha watu. Wameshindwa kutambua kuwa tatizo la kweli haliko kwa mtawala tu, bali katika mfumo mzima unaotumika nchini tangu wakati huo.

Tangu uhuru wake mwaka 1957, Malaysia imetawaliwa na mawaziri wakuu kumi, na vyama tofauti vya kisiasa; Baraza la Kitaifa, Muungano wa Matumaini, Muungano wa Kitaifa, na sasa serikali ya Madani. Ingawa asilimia ndogo ya watu wanaishi maisha ya raha, wengi bado wanakabiliwa na changamoto za kiuchumi zinazoongezeka. Masuala ya kijamii yanazidi kutia wasiwasi. Vile vile, sekta ya elimu bado inakabiliwa na matatizo yanayoendelea. Viwango vya uhalifu havionyeshi dalili zozote za kupungua, lakini vimekuwa vya kutisha sana, ikiwa ni pamoja na kile kinachotokea ndani ya jeshi la polisi lenyewe. Mandhari ya kisiasa inabaki kuwa chafu kila mara na kashfa, rushwa, usaliti wa uaminifu, mapambano ya madaraka, na aina mbalimbali za utovu wa nidhamu, ambazo watu huathirika kila mara.

Kwa kifupi, licha ya mabadiliko ya watawala kwa miaka mingi, watu hawajaonja raha au ustawi wa kweli. Katika kila enzi ya utawala, watu wameendelea kuasi dhidi ya dhuluma ya serikali na kudai haki zao. Tangu enzi ya Dk. Mahathir Muhammad (wa kwanza), mawaziri wakuu wamekuwa wakishinikizwa kujiuzulu, kutoka ndani ya vyama vyao na kutoka kwa nguvu za nje. Hata hivyo, kila wakati waziri mkuu mpya anapoteuliwa, mabadiliko ambayo watu wanatarajia hayatokei. Kinachobaki kuwa mara kwa mara bila kubadilika ni mfumo wa demokrasia yenyewe, ambayo ililazimishwa na nguvu za kikoloni kama sharti la uhuru wa nchi.

Je, mfumo ulioundwa na makafiri, kinyume kabisa na hukumu za Uislamu, unawezaje kutoa suluhisho la kweli kwa Umma wa Kiislamu?! Ni muhimu kwa Waislamu kutambua ukweli huu muhimu; kwamba kubadilisha waziri mkuu bila kubadilisha mfumo hakutawahi kutatua matatizo ya msingi yanayokabili umma huu.

Hali hii halisi haihusu Malaysia pekee, kwa sababu katika nchi za Kiislamu, tunaona mtindo uleule: Tunisia, Misri, Yemen na Libya zote zilishuhudia uasi wakati wa Arab Spring ambao ulisababisha kuondolewa kwa watawala, lakini mifumo ya utawala ilibaki kama ilivyo, na mateso ya watu yaliendelea. Vile vile nchini Sudan, Uturuki, Pakistan, Bangladesh, Indonesia, na nchi nyingine nyingi za Kiislamu, watawala wamebadilika mara kwa mara, lakini mifumo ya kidunia iliyorithiwa kutoka kwa ukoloni ilibaki bila kuguswa. Matokeo yake ni kwamba hali ya umma haijabadilika kimsingi.

Umma lazima uamke na kutambua ukweli kwamba haupaswi kuumwa na shimo lilelile mara mbili. Lakini nchini Malaysia, kwa bahati mbaya, haujaumwa mara moja au mara mbili tu, lakini mara nyingi. Imedhibitika mara kwa mara kwamba wale wanaofika madarakani chini ya mfumo wa demokrasia hawashindwi tu kutekeleza Uislamu - suluhisho la kweli kwa migogoro yetu - lakini kimsingi hawataki kufanya hivyo. Pia imethibitika kuwa demokrasia, kama urithi wa kikoloni, haipingani tu na Uislamu, bali imeundwa kimakusudi kuutenganisha na maisha. Kwa maneno mengine, iliwekwa mahsusi kuzuia utekelezaji wa Uislamu wenyewe.

Hili ndilo janga maradufu linaloikumba Umma wa Kiislamu leo: watawala wafisadi na mfumo fisadi, na yote mawili yameonekana kuwa maovu bila shaka.

Mifumo mibaya haitoi ila watawala wabaya, na watawala hao kwa upande wao wanaendeleza mwendelezo wa mifumo hiyo mibaya. Kama vile Ukomunisti unavyotoa watawala wa Kikomunisti ambao wanadumisha Ukomunisti, na Ubepari unavyotoa watawala wa Kibepari ambao wanadumisha mfumo wa Kibepari, ndivyo demokrasia inavyofanya; inajiimarisha yenyewe kwa kutoa watawala ambao wanaitumikia na kuilinda. Mtawala na mfumo ni pande mbili za sarafu moja ambazo haziwezi kutenganishwa, na kila moja huimarisha nyingine.

Kwa hivyo, njia pekee ya Umma ya kutoka katika majanga haya ni kubadili watawala na mfumo kwa wakati mmoja. Katika Uislamu, mtawala halali ni Khalifa, na mfumo na dola halali ni Ukhalifa. Hili ndilo Hizb ut-Tahrir inajitahidi kulitimiza ulimwenguni kote, na huu ndio wito wetu kwa Umma wote; kufanya kazi nasi bega kwa bega kuanzisha dola ya Khilafah Rashidah kwa misingi ya Utume.

Abdul Hakim Othman

Msemaji Rasmi wa Hizb ut-Tahrir

Nchini Malaysia

Official Statement

المكتب الإعلامي ماليزيا

ماليزيا

المكتب الإعلامي ماليزيا

Media Contact

المكتب الإعلامي ماليزيا

Phone: 03-89201614

Email: htm@mykhilafah.com

المكتب الإعلامي ماليزيا

Khilafah Centre, 47-1, Jalan 7/7A, Seksyen 7, 43650 Bandar Baru Bangi, Selangor

Tel: 03-89201614 | htm@mykhilafah.com

www.mykhilafah.com

Reference: PR-01985ae5-7d30-7115-bb63-ee74d7584be2