Organization Logo

السودان - مكتب - ناطق

ولاية السودان

الخرطوم شرق- عمارة الوقف الطابق الأرضي -شارع 21 اكتوبر- غرب شارع المك نمر

Tel: 0912240143- 0912377707

spokman_sd@dbzmail.com

www.hizb-ut-tahrir.info

Tutaacha Lini Kuingilia Kati kwa Mataifa ya Magharibi Makafiri na Mashirika Yake ya Kikoloni Katika Maisha Yetu, na Tuuelekeze Uso Wetu Kwa Mungu Mmoja Mwenye Haki?
Press Release

Tutaacha Lini Kuingilia Kati kwa Mataifa ya Magharibi Makafiri na Mashirika Yake ya Kikoloni Katika Maisha Yetu, na Tuuelekeze Uso Wetu Kwa Mungu Mmoja Mwenye Haki?

October 10, 2025
Location

Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Tutaacha Lini Kuingilia Kati kwa Mataifa ya Magharibi Makafiri na Mashirika Yake ya Kikoloni Katika Maisha Yetu, na Tuuelekeze Uso Wetu Kwa Mungu Mmoja Mwenye Haki?

Chini ya udhamini wa shirika la Ufaransa la Promediation, vyama vya Sudan viliandaa warsha huko Port Sudan, kama ilivyoonyeshwa kwenye tovuti ya Sudan Tribune mnamo 2025/10/5: (Msemaji wa kambi ya Kidemokrasia, Mohamed Zakaria, alisema kwamba warsha hiyo "inajadili jinsi ya kufanya mazungumzo ya Sudan na Sudan, pande zake, mahali pa mkutano, jukumu la upatanishi, na maswala ya ufadhili." Alieleza kuwa warsha hiyo itafuatwa na hatua zingine kwa lengo la kufikia makubaliano kati ya idadi kubwa ya nguvu za kisiasa nchini, kufikia utulivu, kuepuka migogoro na mivutano hasi).

Sisi katika Hizb ut-Tahrir / Wilaya ya Sudan, kuhusiana na hali halisi hii, tunaeleza ukweli ufuatao:

Kwanza: Uislamu umeamua suala la chanzo cha matibabu ya matatizo ya maisha kwa uamuzi wa mwisho, na umeifanya mamlaka kuwa ya sheria pekee, hivyo haijuzu kwa Mwislamu kuchukua tiba kwa tatizo lolote la matatizo ya maisha ila kutoka kwa sheria, bali ameifanya hiyo kuwa sawa na imani, Mwenyezi Mungu Mtukufu alisema: ﴿La, naapa kwa Mola wako Mlezi! Hawataamini mpaka wakufanye wewe hakimu katika yale wanayo khitalifiana, kisha wasione dhiki nyoyoni mwao kwa hukumu yako, na wanyenyekee kabisa.﴾; kwa hiyo, chanzo cha tiba ni Uislamu pekee, na si matamanio ya wanasiasa wanaoshindana kwa viti vya utawala.

Pili: Uislamu umewataka Waislamu, panapotokea mzozo katika jambo lolote, wairudishe kwenye Kitabu cha Mwenyezi Mungu na Sunna za Mtume wake ﷺ, si kwa nchi za kikoloni, wala mashirika yake ya uhalifu, kwani kulirudisha jambo hilo kwenye Uislamu ni miongoni mwa mambo muhimu ya imani, Mwenyezi Mungu alisema: ﴿Na mkizozana katika jambo lolote, basi lirudisheni kwa Mwenyezi Mungu na Mtume, ikiwa mnamuamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho. Hiyo ndiyo bora na ndiyo nzuri zaidi kwa matokeo.﴾.

Tatu: Kutegemea nchi za kikoloni makafiri wenye chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu, kama vile Ufaransa, Marekani, Uingereza na Urusi, na kutegemea uingiliaji wa mashirika yao ya uhalifu, kama vile Promediation, Taasisi ya Amani ya Marekani, Chatham House, na mengineyo, ni kujiharibu kisiasa, na usaliti kwa umma, Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: ﴿Enyi mlio amini! Msiwafanye siri zenu watu wasio kuwa wenu. Hawataacha kukufanyieni ubaya. Wanapenda mtaabike. Uadui umekwisha dhihirika katika vinywa vyao, na yale yanayo ficha vifua vyao ni makubwa zaidi. Tumekwisha kubainishieni Ishara ikiwa nyinyi ni wenye akili.﴾.

Nne: Sheria ya Kiislamu imefanya uhusiano na nchi za kigeni na mashirika yake kuwa mdogo kwa dola, na imemzuia mtu yeyote au kikundi kuwa na uhusiano na nchi ya kigeni, au shirika lolote la kigeni kabisa, kwa kuwa kuna hatari kubwa kwa chombo cha dola na umma.

Tano: Uislamu unatosha kwa hukumu zake na matibabu yake kwa matatizo yote ya maisha, kwani siasa katika Uislamu ni kuwahudumia watu, ndani na nje, na dola inazifanya kivitendo, na ni kazi tukufu zaidi, bali ni kazi ya manabii, kama ilivyoelezwa na Nabii ﷺ aliposema: "Wana wa Israili walikuwa wakiongozwa na manabii, kila nabii alipokufa, nabii alimfuata, na hakuna nabii baada yangu, na watakuwepo makhalifa na wataongezeka." Wakasema: Unatuamrisha nini? Akasema: "Timizeni ahadi ya wa kwanza, na wa kwanza, na muwape haki zao, kwani Mungu atawauliza kuhusu yale aliyowakabidhi." Imepokewa na Muslim.

Hitimisho: Hakika umma leo unahitaji mfumo wa Uislamu; Ukhalifa ulioongoka kwa njia ya unabii, ambao unasimamisha dini, unatekeleza sheria, unaondoa ushawishi wa magharibi kafiri mkoloni kutoka nchi yetu, unawafuatilia watu wa mashaka wanaoshirikiana na balozi za magharibi na mashirika yake, na unafanya maisha kuwa ya Mungu mmoja Mwenye Haki. Na kwa ajili ya haya, wafanyakazi wafanye kazi, Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: ﴿Enyi mlio amini! Muitikieni Mwenyezi Mungu na Mtume anapo kuombeni kwenye litakalo kuuhisha.﴾.

Ibrahim Othman (Abu Khalil)

Msemaji Rasmi wa Hizb ut-Tahrir katika Wilaya ya Sudan

Official Statement

السودان - مكتب - ناطق

ولاية السودان

السودان - مكتب - ناطق

Media Contact

السودان - مكتب - ناطق

Phone: 0912240143- 0912377707

Email: spokman_sd@dbzmail.com

السودان - مكتب - ناطق

الخرطوم شرق- عمارة الوقف الطابق الأرضي -شارع 21 اكتوبر- غرب شارع المك نمر

Tel: 0912240143- 0912377707 | spokman_sd@dbzmail.com

www.hizb-ut-tahrir.info

Reference: PR-0199c793-8958-7967-996b-69e51a520728