Organization Logo

القسم النسائي في المكتب الإعلامي المركزي

المركزي

Tel: 0096171724043

Fax: 009611307594

ws-cmo@hizb-ut-tahrir.info

http://www.hizb-ut-tahrir.info/

Damu itachemka lini kwenye mishipa na uwekwe kikomo kwa uchokozi wowote na mikono ya maadui ikatwe?!
Press Release

Damu itachemka lini kwenye mishipa na uwekwe kikomo kwa uchokozi wowote na mikono ya maadui ikatwe?!

July 26, 2025
Location

Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Damu itachemka lini kwenye mishipa na uwekwe kikomo kwa uchokozi wowote na mikono ya maadui ikatwe?!

Wizara ya Afya ilitoa katika ripoti yake ya takwimu ya kila siku ya idadi ya mashahidi na majeruhi kutokana na uchokozi wa Wayahudi dhidi ya Ukanda wa Gaza tarehe 2025/07/23 kwamba hospitali za ukanda zilipokea mashahidi 113 na majeruhi 534 katika saa 24 zilizopita. Idadi ya mashahidi na majeruhi tangu Machi 18, 2025 hadi tarehe ya taarifa ilifikia mashahidi 8,363 na majeruhi 31,004, na hivyo idadi ya waathirika wa uchokozi imeongezeka hadi mashahidi 59,219 na majeruhi 143,045 tangu Oktoba 7, 2023.

Wizara ya Afya ya Palestina ilitangaza Jumatano, 2025/07/24, kurekodi vifo vipya 10 kutokana na njaa na utapiamlo katika saa ishirini na nne zilizopita, na kufanya jumla ya vifo kufikia visa 111 tangu kuanza kwa mzozo huo. Katika hali ya kusikitisha, vyanzo vya matibabu vilifichua vifo vya watoto 21 kutokana na njaa na utapiamlo katika siku tatu zilizopita pekee, ikijulikana kuwa baadhi ya watoto "wanakufa katika mahema na nyumba zao bila kufika hospitali au mtu yeyote kujua kuhusu hilo." Katika muktadha huo huo, Rick Peeperkorn, mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani katika maeneo yanayokaliwa ya Palestina, alieleza kuwa mwezi wa Julai pekee ulishuhudia watoto 5,100 wakilazwa katika programu za matibabu ya utapiamlo, wakiwemo watoto 800 wanaougua udhaifu mkubwa.

Mashambulizi ya kikatili ya chombo cha Kiyahudi dhidi ya watu wetu huko Gaza yanaendelea kwa njia na mbinu zote; kwa makombora, mauaji, mzingiro na njaa, kwa lengo la kuwaangamiza na kuwaondoa, bila kuwatenga wanawake au watoto, lakini kinyume chake, wanalenga kwa makusudi kuwalenga hawa kudhoofisha ari ya watu wa Gaza na kuwalazimisha kujisalimisha, kunyenyekea na kuwa wanyonge.

Mkurugenzi Mtendaji wa UNICEF alitoa taarifa za kutisha kuhusu kuuawa kwa watoto 7 walipokuwa wakingoja kupata maji katika eneo la usambazaji, na aliongeza kuwa tukio hilo linakuja siku chache baada ya watoto na wanawake kuuawa walipokuwa wakingoja misaada ya chakula. Hii ndiyo hali ambayo watoto wetu huko Gaza wamefikia, wanauawa na kuangamizwa kwa damu baridi na adui mkuu, na damu imeganda kwenye mishipa ya watu wa umma, kwa hiyo hakuna harakati wala msaada!

Enyi watu wa umma wa Kiislamu: Kuna nini kwenu mko kama wafu hamuendeshwi?! Ndugu zenu wanatafuta msaada, wanaomba msaada, basi mnafanya nini? Au mmeridhika na kuwaombea tu?! Je, mmeshindwa au mmekamatana na maisha na mnaogopa kifo?! Wapi mapenzi yenu kwa dini yenu na hamu yenu ya kuwa shahidi au mmeacha kushinda mojawapo ya mazuri mawili?! Enyi watu wa umma bora ambao Mungu amewatoa kwa ajili ya watu: Je, mmezoea matukio ya mateso na mauaji na mmebaki bila kufanya lolote, mmeshindwa kusaidia?! Je, hamna msukumo wa wakweli na wanyofu ndani yenu ambao utawasababisha kuamka kwa pamoja, kukata mizizi ya wahalifu na kuwasaidia walio dhaifu?!

Sisi katika Idara ya Wanawake katika Ofisi Kuu ya Habari ya Hizb ut-Tahrir tunatoa wito kwa watu wote wa umma kufanya kazi ya kuwashawishi wale walio na uwezo wa kusitisha mauaji haya kuchukua hatua na kukomesha sera ya njaa ambayo inawaangamiza watu wetu huko Gaza na kusimamisha maporomoko ya damu ambayo yamewazama na kukata mikono ya maadui ambayo imefika kwa uovu kwa watu wao. Tunawaomba kila mtu kufanya kazi ya kumsimika Khalifa ambaye atawalinda raia wake, kuwapatia usalama na utulivu na kuwasha hofu na uoga katika nafsi za maadui ili wasifikirie kwa muda mfupi kuwashambulia mtu yeyote kati yao.

Idara ya Wanawake

Katika Ofisi Kuu ya Habari

ya Hizb ut-Tahrir

Official Statement

القسم النسائي في المكتب الإعلامي المركزي

المركزي

القسم النسائي في المكتب الإعلامي المركزي

Media Contact

القسم النسائي في المكتب الإعلامي المركزي

Phone: 0096171724043

Fax: 009611307594

Email: ws-cmo@hizb-ut-tahrir.info

القسم النسائي في المكتب الإعلامي المركزي

Tel: 0096171724043 | ws-cmo@hizb-ut-tahrir.info

Fax: 009611307594

http://www.hizb-ut-tahrir.info/

Reference: PR-0198461e-f250-78ef-9766-4b629217d119