Organization Logo

المكتب الإعلامي المركزي

المركزي

Tel: 0096171724043

Fax: 009611307594

media@hizb-ut-tahrir.info

www.hizb-ut-tahrir.info

Kongamano la Islamabad Kati ya Usaliti wa Viongozi na Wajibu wa Kunusuru
Press Release

Kongamano la Islamabad Kati ya Usaliti wa Viongozi na Wajibu wa Kunusuru

July 30, 2025
Location

Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Kongamano la Islamabad Kati ya Usaliti wa Viongozi na Wajibu wa Kunusuru

Wakati taasisi ya Kiyahudi inaendelea kufanya mauaji huko Gaza, na kuwafanya watu wake kuwa na njaa, na wakati umma umepoteza tumaini kwa viongozi wao kuwanusuru, tamaa kubwa ilitoka moyoni mwa Islamabad, ambapo mnamo Jumamosi, 2025/7/26, mkutano wa wakuu wa majeshi ya ulinzi wa kikanda ulifanyika kwa ushiriki wa Amerika na nchi za Asia ya Kati, chini ya usimamizi wa Jeshi la Pakistani, ambapo mkutano huo uliwakutanisha viongozi wakuu wa kijeshi kutoka Amerika, Kazakhstan, Kyrgyzstan, Tajikistan, na Uzbekistan.

Idara ya habari ya kijeshi ilitangaza kuwa mkutano huo ulijadili kuimarisha ushirikiano wa kiusalama na kupambana na (ugaidi na itikadi kali), kulingana na ajenda ya kawaida ya Amerika ambayo inalenga Uislamu na Waislamu na kila mtu anayefanya kazi kwa ajili ya maendeleo yao. Na kwa kweli, hakukuwa na majadiliano juu ya suala la Palestina, au juu ya uhalifu ambao watoto wachanga huota kwa hofu yao, na taarifa ya mwisho haikujumuisha kutaja mateso ya watu wa Gaza, au kutaja uhalifu unaoendelea dhidi yao, achilia mbali kuwa na wito wa jihadi au taarifa ya msimamo wa kisheria kuhusu uvamizi, ambao ni msimamo ambao Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ alihukumu katika bishara yake: «Mayahudi watapigana nanyi, na mtawashinda, hata jiwe litasema: Ewe Muislamu, huyu ni Myahudi yuko nyuma yangu, basi muue» Imesimuliwa na Bukhari na Muslim.

Katika tukio ambalo roho nzuri na maumbile safi huchukizwa nalo, kamanda wa Kamandi Kuu ya Marekani alihudhuria mkutano huo, kama kiongozi, mwelekezi, na anayeamuru ajenda ya Amerika na maono yake kwa mkutano na eneo hilo, na alitunukiwa Nishani ya Ubora katika sherehe rasmi tofauti, licha ya kuwa mmoja wa wapangaji na wafadhili wakuu wa uchokozi wa taasisi ya Kiyahudi dhidi ya Gaza, na msimamizi wa moja kwa moja wa operesheni za Amerika zinazoiunga mkono. Mkutano huo uliishia kwenye ajenda ya Washington "kupambana na ugaidi na itikadi kali", ambayo ni itikadi ambazo zinalenga kukandamiza makundi ya Kiislamu yanayofanya kazi kwa ajili ya maendeleo ya umma na kupinga uvamizi wa Kiyahudi na Kihindi, na sio kukabiliana na adui halisi wa ubinadamu, taasisi ya Kiyahudi na wale wanaomuunga mkono.

Hakika, kuhudhuria kwa viongozi wa Amerika, na kushughulika nao kama washirika katika usalama, sio tu usaliti wa wazi kwa Uislamu na Waislamu, na kujiunga kikamilifu na kambi ya uovu inayoongozwa na taasisi ya Kiyahudi na kambi ya usaliti inayoongozwa na Sisi na watawala wa Al Saud, wakati damu ya watoto wa Gaza inamwagika usiku na mchana, lakini pia ni kuendelea kwa njia ya uajiri kwa Amerika na utekelezaji wa ajenda yake na maono yake kwa eneo hilo, huku mzozo kati ya Amerika na Uchina ukizidi.

Tunawahutubia viongozi waaminifu katika jeshi la Pakistani na majeshi ya umma, na tunawaambia kuwa Amerika ni adui mkubwa wa umma, na kwamba Wayahudi ni wauaji, na yeyote anayeshirikiana nao katika wakati huu mgumu hauwakilishi umma au Uislamu. Wanapaswa kutambua kuwa viongozi wao wa kijeshi ndio sababu ya kudorora tunakoishi, na ndio sababu ya unyonge tunaopokea kutoka kwa Wayahudi, Wahindu, na Amerika nyuma yao. Kwa hivyo, lazima muondoe mawakala hawa, na mkipe ushindi Hizb ut-Tahrir ili kusimamisha Khilafah Rashidah ya pili kwa njia ya Utume, kwani ndiyo pekee itakayonusuru Gaza, kulipiza kisasi kwa watoto wake, na kukomboa Msikiti wa Al-Aqsa. Na jueni kwamba umma kutoka Jakarta hadi Rabat, unawasubiri mfanye uamuzi wa kihistoria na wa heshima ambao utatikisa ardhi chini ya miguu ya Wayahudi, Wahindu, na wale wanaowaunga mkono.

Hakika, Pakistan, kwa nguvu zake za nyuklia, jeshi lake la waumini na wanamgambo, na watu wake wanaopenda Uislamu, inaweza kusimamisha vita vya mauaji ya kimbari huko Gaza katika masaa, lakini inaweza kubadilisha mizani ya nguvu za kimataifa, ikiwa uongozi mwaminifu utachukua uamuzi. Kwa jina la watoto wa Gaza, damu ya mashahidi wake, na majeraha ya wajane na wanyonge, tunawasihi: msikae kimya juu ya usaliti wa uongozi wenu, msiwashike mikono wale waliowashika mikono wauaji, na msiwaheshimu wale waliowaua watoto wetu. Tunawakumbusha maneno ya Mwenyezi Mungu: ﴿Enyi mlio amini! Mmekuwaje, mkiambiwa: Nendeni kupigana katika njia ya Mwenyezi Mungu, mnazidi kushikamana na nchi? Je! Mmeridhia uhai wa dunia kuliko Akhera? Basi starehe ya uhai wa dunia ni chache ukilinganisha na Akhera﴾.

Enyi maafisa wa jeshi la Pakistani, enyi maafisa wa majeshi ya Waislamu, na kila mwenye chembe ya imani moyoni mwake: Nani kati yenu atakuwa na heshima ya kukomboa Msikiti wa Al-Aqsa? Nani kati yenu atakumbukwa katika vitabu vya historia kama mkombozi wa ardhi iliyobarikiwa kama alivyokomboa Salahuddin, Mungu amrehemu?!

Hiyo ndiyo siku ambayo waumini watafurahi kwa ushindi wa Mwenyezi Mungu, na hiyo ndiyo siku ambayo milango ya Pepo itafunguliwa kwa wale waliopigana na kushinda ﴿Enyi mlio amini! Mkimnusuru Mwenyezi Mungu, naye atakunusuruni na atathibitisha nyayo zenu﴾.

Ofisi Kuu ya Habari

kwa Hizb ut-Tahrir

Official Statement

المكتب الإعلامي المركزي

المركزي

المكتب الإعلامي المركزي

Media Contact

المكتب الإعلامي المركزي

Phone: 0096171724043

Fax: 009611307594

Email: media@hizb-ut-tahrir.info

المكتب الإعلامي المركزي

Tel: 0096171724043 | media@hizb-ut-tahrir.info

Fax: 009611307594

www.hizb-ut-tahrir.info

Reference: PR-019850f4-5e68-7aa0-a779-3ad09d0c3b62