Organization Logo

مصر - المكتب

ولاية مصر

Tel:

info@hizb.net

www.hizb.net

Mkutano wa Sharm El-Sheikh Kutangaza Ushindi Dhidi ya Umma, Kudhibitisha Utiifu na Kuimarisha Ukaliaji
Press Release

Mkutano wa Sharm El-Sheikh Kutangaza Ushindi Dhidi ya Umma, Kudhibitisha Utiifu na Kuimarisha Ukaliaji

October 14, 2025
Location

Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Mkutano wa Sharm El-Sheikh Kutangaza Ushindi Dhidi ya Umma, Kudhibitisha Utiifu na Kuimarisha Ukaliaji

Baada ya tangazo la Trump kuhusu ushindi ambao alisema yeye na mwanafunzi wake, taasisi ya Kiyahudi, walipata katika hotuba yake mbele ya Knesset, ushindi huo ulikuwa dhidi ya raia wasio na hatia, wanawake, watoto, wazee, na dhidi ya miti na mawe, mchinjaji wa Gaza alielekea kwenye mkutano uliopangwa na Sisi, wakala wake nchini Misri, na akawaalika wote waliopanga njama dhidi ya ardhi iliyobarikiwa. Mkutano huo ulifanyika katika jiji la Sharm El-Sheikh mnamo 2025/10/13, chini ya kichwa "Mkutano wa Amani wa Sharm El-Sheikh", ulihudhuriwa na zaidi ya nchi ishirini na mashirika ya kimataifa, ukiongozwa na Rais wa Marekani Trump na Rais wa Misri Sisi, na ushiriki mpana wa viongozi wa Kiarabu na Magharibi, akiwemo Mfalme wa Jordan, Amir wa Qatar, Rais wa Ufaransa, Rais wa Uturuki, Waziri Mkuu wa Pakistan, na Waziri Mkuu wa Indonesia, pamoja na ujumbe wa Ulaya na Asia. Mkutano huu ulikuja siku chache baada ya kutangazwa kwa makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya ukaliaji na Hamas, yaliyojumuisha kubadilishana wafungwa, kusitisha mapigano, na kufungua njia ya mazungumzo ya kusimamia Ukanda wa Gaza na kuijenga upya.

Licha ya kichwa kinachovutia cha mkutano huo, ambacho kinadai amani, utulivu na ujenzi mpya, ukweli wake haupingani kabisa na kichwa chake. Yaliyomo halisi ya mkutano huo yalikuwa sherehe ya Trump ya ushindi uliodaiwa na taasisi ya Kiyahudi, na kuionyesha kama mafanikio makubwa ambayo yanastahili Tuzo ya Nobel ya Amani - tuzo ambayo haijawahi kutolewa kwa mtu anayewakilisha maadili na kanuni tukufu au kwa mafanikio yanayohudumia ubinadamu kwa haki - pia alitafuta kupitia hiyo kujitambulisha kama bwana na mtengenezaji pekee wa uamuzi katika suala la Mashariki ya Kati na uundaji wake. Kwa kuongezea, Trump aliwazungumzia waziwazi watu dhaifu wa nchi za Waislamu kufuata makubaliano ya Abraham, ambayo ni, kumtawaza serikali ya ukaliaji kama mfalme wa Mashariki ya Kati mpya ambayo anataka.

Misri ilichukua jukumu muhimu katika kuandaa mkutano huo na kutoa kifuniko cha Kiarabu kwa mipango ya Amerika, kama ilivyofanya katika makubaliano ya kusitisha mapigano ya hapo awali. Serikali ya Misri imejitolea kwa Mkataba wa Camp David ambao ulizuia harakati zake za kijeshi na kuibadilisha kuwa mlinzi wa mipaka ya taasisi ya Kiyahudi, na leo inajionyesha kama mpatanishi "asiyeegemea upande wowote", wakati jukumu lake halisi ni kutengeneza njia ya nchi zingine za Waislamu kuanzisha uhusiano wa kawaida na Wayahudi kwa utekelezaji wa matakwa ya Amerika, na kuhakikisha usalama wa Wayahudi kutokana na tishio lolote kutoka kwa umma.

Hawa washiriki wa njama waovu huko Sharm El-Sheikh hawawakilishi suala la Palestina, wala sio wa umma wa Kiislamu ambao unamiliki suala hilo. Jukumu la ukombozi wa Palestina na kulipiza kisasi kwa mashahidi wake ni amana nzito ambayo haitekelezwi ila na wanaume halisi ambao ﴿WAMETIMIZA WALICHOAHIDI KWA ALLAH﴾; na sio hawa watu dhaifu. Kila makubaliano au mkutano unaotegemea kukiri taasisi ya Kiyahudi na kuishi nayo, na kudhibitisha uwepo wake kwenye inchi yoyote ya ardhi ya Palestina ni batili bila ubishi; kwa sababu inapingana na hukumu ya kisheria ya uhakika ya ulazima wa kukomboa ardhi iliyobarikiwa kikamilifu, na uharamu wa kukabidhi sehemu yoyote yake, Mwenyezi Mungu alisema: ﴿NA PIGANENI NAO HATA KUSIWE FITNA NA DINI IWE YOTE YA ALLAH﴾, na Aliyetukuka alisema: ﴿NA NINI KWENU HAMWAPIGANI KATIKA NJIA YA ALLAH NA WANYONGE﴾.

Mkutano huu ni sehemu ya mradi wa Amerika wa kupanga upya eneo hilo na kuunganisha taasisi ya Kiyahudi ndani yake, na kumaliza suala la Palestina kupitia njia za kisiasa za uwongo baada ya kuwachosha watu wa Gaza kwa vita na kuzingirwa. Njia hizi zinatafuta kuingiza nguvu ya usimamizi wa kimataifa inayosimamia mipango ya kiusalama na kuhakikisha usalama wa Wayahudi, kwa msaada wa serikali za Kiarabu, haswa serikali ya Misri, na kucheza jukumu hili ni uhalifu wa usaliti, kwa sababu haujengwa kwa maslahi ya umma, lakini kwa utiifu kwa bwana wa Amerika na utekelezaji wa mipango yake.

Wajibu kuelekea Gaza sio kuandaa mikutano wala kusubiri maamuzi ya kimataifa, lakini kuhamasisha majeshi ya Waislamu kukomboa ardhi iliyobarikiwa kutoka baharini hadi mtoni, na wana uwezo wa kuponda taasisi ya Kiyahudi kwa saa moja ya mchana. Ama watawala, ndio kikwazo kikubwa mbele ya harakati za majeshi haya, kwa sababu wao ni wasaliti waliofungamana na makubaliano ya unyonge na vizuizi vya kijeshi (Camp David, Wadi Araba, Oslo, na Abraham). Na hapa ndipo kazi halisi ya ukombozi wa Palestina inaanza na kung'oa serikali hizi na kuanzisha Ukhalifa ulioongoka kwa misingi ya unabii, ambao unahamasisha majeshi na kuwasukuma kuelekea kile ambacho Mungu amewalazimu na kupitisha jihad kukomboa ardhi na kuunganisha umma.

Enyi askari wa Kinana: Nyinyi sio askari wa Amerika wala zana za kutekeleza mipango yake, lakini nyinyi ni sehemu ya umma wa Muhammad ﷺ, mliokabidhiwa kisheria kusaidia wanyonge na kuinua neno la Mungu, na kinachoendelea huko Sharm El-Sheikh chini ya usikilizaji wenu, maono yenu na ulinzi wenu, sio ushindi kwa Gaza lakini ni uthibitisho wa kuzingirwa kwake na uimarishaji wa utawala wa adui juu ya hatima yake, na kuwapa Wayahudi kile wasichoweza kupata licha ya yote waliyoyafanya kwa Gaza na watu wake. Jibu halali la lazima ni kukataa mikutano kama hiyo, kufichua malengo yake, na kusonga mbele kuelekea ukombozi wa kweli sio "amani ya uwongo".

﴿NA NINI KWENU HAMWAPIGANI KATIKA NJIA YA ALLAH NA WANYONGE MIONGONI MWA WANAUME NA WANAWAKE NA WATOTO

Ofisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir

Katika Wilaya ya Misri

Official Statement

مصر - المكتب

ولاية مصر

مصر - المكتب

Media Contact

مصر - المكتب

Phone:

Email: info@hizb.net

مصر - المكتب

Tel: | info@hizb.net

www.hizb.net

Reference: PR-0199ddb9-dae8-78c2-9f75-d76ce55733e1