Taarifa kwa Vyombo vya Habari
Wito kutoka Ofisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir nchini Uzbekistan
Kuhusu kukamatwa kwa Abdul Aziz Abdul Jalilov
Mnamo 2025/10/30, mwanachama wa Hizb ut-Tahrir, Abdul Aziz Abdul Jalilov, ambaye anatoka Uzbekistan, alikamatwa katika ofisi ya uhamiaji huko Stockholm.
Kwa kadiri tunavyojua, idara ya uhamiaji imeamua kumrudisha ndugu Abdul Aziz nchini Uzbekistan.
Katika suala hili, tungependa kuvutia mawazo ya idara ya uhamiaji ya Uswidi kwa yafuatayo:
Kwanza: Hizb ut-Tahrir ni chama cha kisiasa cha Kiislamu ambacho shughuli zake ni za kiakili na kisiasa pekee na huepuka aina yoyote ya vurugu.
Pili: Kupiga marufuku shughuli za Hizb ut-Tahrir na kuwafuata wanachama wake nchini Uzbekistan ni suala la kisiasa tu, kama ilivyotangazwa na wataalam wengi na watetezi wa haki za binadamu.
Tatu: Kwa miaka mingi nchini Uzbekistan, maelfu ya vijana wetu wamekamatwa na mamia yao wameuawa chini ya mateso. Wengi wao bado wako gerezani hadi sasa. Mwaka huu, kesi nyingi zimefanyika kwa vijana wetu ambapo wamehukumiwa tena kifungo cha miaka mingi.
Nne: Kumrudisha ndugu Abdul Aziz nchini Uzbekistan kunamaanisha kuwa atakabiliwa na: kifungo na mateso, angalau!
Kwa hivyo, tunakutaka ughairi kumrudisha Abdul Aziz na umuachilie mara moja.
Ofisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir
nchini Uzbekistan