Mtazamo wa Habari 03-07-2025
Trump: Taasisi ya Kiyahudi imekubali kusitisha mapigano kwa siku 60 huko Gaza
Rais wa Marekani Trump alisema kwenye jukwaa lake la Truth Social mnamo 2025/7/2 baada ya kukutana na maafisa wa Marekani na Wayahudi huko Washington kwamba taasisi ya Kiyahudi imekubali masharti muhimu ili kukamilisha usitishaji wa mapigano kwa siku 60 na akaongeza "Tutafanya kazi katika kipindi hiki na pande zote kukomesha vita. Watu wa Qatar na Misri ambao wamefanya kazi kwa bidii kuleta amani watatoa pendekezo hili la mwisho. Ninatumai kwa manufaa ya Mashariki ya Kati kwamba Hamas itakubali makubaliano haya kwa sababu hali haitaboreka, lakini itazidi kuwa mbaya zaidi."
Hii inamaanisha kuwa taasisi ya Kiyahudi, baada ya kuwapata mateka, inaweza kuanza tena uchokozi wake na vita vya mauaji ya halaiki huko Gaza baada ya kuwachukua kama ilivyofanya katika usitishaji mapigano uliopita, kwa sababu ilibainisha lengo lake la kuondoa nguvu zote za kijeshi huko Gaza na kukabidhi silaha zake, na kutimiza lengo la Trump la kuwahamisha watu wake na kuifanya kuwa mapumziko ya Amerika. Watawala wa Misri na Qatar wanafanya kazi kama wasimamizi wa Amerika na taasisi ya Kiyahudi, kwani walishinikiza Hamas hapo awali kukabidhi mateka na sasa wanafanya jukumu lile lile. Hawafanyi uungwaji mkono wowote kwa watu wa Gaza, si kwa kuingiza chakula au kinywaji, wala kwa kukabiliana na uchokozi wa Wayahudi.
-----------
Amerika inatilia maanani uwekaji mipaka kati ya Lebanoni na Syria
Ripoti katika Mashariki ya Kati mnamo 2025/7/2 ilisema kwamba Balozi wa Amerika nchini Uturuki na Mjumbe Maalum wa Amerika kwa Syria Tom Barak anazingatia umuhimu maalum wa uwekaji mipaka ya Lebanoni na Syria wakati wa mikutano yake mnamo Julai 7 na 8 na Rais wa Lebanon Aoun, Spika wa Bunge Nabih Berri, Waziri Mkuu Nawaf Salam, na uongozi wa jeshi.
Ripoti hiyo ilisema kuwa kile ambacho serikali iliyopita ilikuwa ikifanya cha ulanguzi wa kupitisha dawa za kulevya kama utangulizi wa kuzifikisha kwa nchi za Kiarabu, kiliongeza ushawishi wa Washington kujiunga na juhudi zake kwa kumwomba Barak kujumuisha uwekaji mipaka kama moja ya mawazo ya kusaidia Lebanoni.
Kwa hivyo Amerika inachukua matendo ya serikali iliyopita kama kisingizio cha kudhibitisha mgawanyiko kati ya Syria na Lebanoni, nchi moja iliyogawanywa na ukoloni na kuanzisha serikali mbili tegemezi kwake na kufikisha makundi ya rushwa kuzisimamia.
Hii inathibitisha kuwa Balozi na Mjumbe wa Amerika Barak anafanya sera ya kikoloni ya hila na kile alichokisema baada ya kukutana na Rais wa Syria Ahmed Al-Shara mnamo 2025/06/24 ni upotoshaji na udanganyifu, kwani aliandika kwenye jukwaa la X akisema: "Karne moja iliyopita, Magharibi iliweka ramani, mipaka iliyochorwa, ulinzi na utawala wa kigeni. Mkataba wa Sykes-Picot uligawanya Syria na eneo pana zaidi ili kufikia maslahi ya kikoloni, si kwa ajili ya amani. Kosa hili limegharimu vizazi vyote. Hatutaruhusu lirudiwe tena." Alisema: "Enzi ya uingiliaji wa Magharibi imekwisha, mustakabali ni wa suluhisho za kikanda zinazojengwa juu ya ushirikiano na diplomasia inayotegemea heshima. Kama Rais Trump alivyosisitiza katika hotuba yake huko Riyadh mnamo Mei 13: Zimepita siku ambazo waingiliaji wa Magharibi walikuwa wakiruka kwenda Mashariki ya Kati kutoa mihadhara kuhusu maisha na jinsi ya kuendesha mambo yenu wenyewe" na akasema: "Janga la Syria limezaliwa kutokana na mgawanyiko".
Na hapa anathibitisha kuwa Amerika ni mwendelezo wa ukoloni wa zamani wa Magharibi na inafanya kazi ya kudhibitisha kile ilichokifanya. Hatutarajii kutoka kwake, wakati anawakilisha nchi kubwa ya kikoloni, kufanya kazi ya kuondoa mipaka hii na kuunganisha nchi na kuirejesha ilivyokuwa kabla ya Sykes-Picot, sehemu katika nchi moja.
----------
Taasisi ya Kiyahudi inafanya mawasiliano ya moja kwa moja na serikali ya Syria ili kuanzisha uhusiano wa kawaida
Ukurasa wa Televisheni ya Syria 2025/6/28 uliripoti kile Waziri wa Mambo ya Nje wa Taasisi ya Kiyahudi Gideon Saar alisema kwamba taasisi yake haipingi "kimsingi kuingia katika mchakato wa mazungumzo na Syria. Lakini makubaliano yoyote ya amani au kuanzisha uhusiano wa kawaida ya baadaye lazima yafanyike wakati Golan iko mikononi mwetu. Ninasisitiza jambo hili, hakuna kuachia jambo hili. Na ikiwa Syria itatambua mamlaka ya Israeli juu ya milima ya Golan, itakuwa msingi wa makubaliano yanayokubalika. Lakini hatuko katika hatua hii bado, na bado tunafuatilia matukio." (Kituo cha Habari cha Kiyahudi 24, 2025/6/28)
Kituo hiki kiliripoti kutoka kwa vyanzo vya habari vya Syria vilivyoarifiwa kwamba Syria na taasisi ya Kiyahudi zinaelekea kusaini makubaliano ya amani kabla ya mwisho wa mwaka huu 2025. Chini ya makubaliano hayo, inatarajiwa kwamba taasisi ya Kiyahudi itajiondoa hatua kwa hatua kutoka kwa ardhi yote ya Syria iliyodhibitiwa baada ya uvamizi wa eneo la bafa mnamo Desemba 8 iliyopita, pamoja na kilele cha Mlima Sheikh. Na kwamba makubaliano ya kihistoria yataleta uhusiano wa kawaida kabisa kati yao, na kwamba Milima ya Golan itakuwa bustani ya amani. Na kwamba Syria haiondoi uwezekano wa amani na taasisi ya Kiyahudi kabla ya mwisho wa muhula wa Trump, na kwamba mazungumzo ya moja kwa moja yanafanyika kila siku naye katika siku za hivi karibuni.
Mkuu wa Baraza la Usalama la Taifa linaloitwa la Wayahudi, Tzachi Hanegbi, alifichua kuwepo kwa mawasiliano ya moja kwa moja na endelevu kati ya taasisi yake na serikali ya Syria na kwamba pande hizo mbili zinajadili uwezekano wa kuanzisha uhusiano wa kawaida. Alisema, "Mazungumzo na Syria hayazuiliwi tena kwa njia za nyuma au wasuluhishi, lakini yamekuwa mawasiliano ya moja kwa moja na ya kila siku ambayo yanajumuisha ngazi mbalimbali za serikali," na akasema kuwa Syria na Lebanoni zinachukuliwa kuwa miongoni mwa nchi zinazoweza kufanya makubaliano ya kuanzisha uhusiano wa kawaida na taasisi yake kama vile makubaliano ya Abraham ambayo ilisaini na nchi nyingine za Kiarabu.
Inaonekana kwamba watawala wapya wa Syria wamekataa isipokuwa kujisalimisha kwa taasisi ya Kiyahudi na Amerika nyuma yake, kama Mamlaka ya Palestina ilivyofanya, ambayo imekuwa mlinzi wa taasisi ya Kiyahudi. Inaonekana kwamba hawadai tena Milima ya Golan na kujiondoa kwa taasisi ya Kiyahudi hadi mipaka ya Juni 4, 1967, lakini kujiondoa kwake hadi mipaka ya Desemba 8, 2024. Na yote hayo yanatokana na kuacha utekelezaji wa Uislamu, ikiwa ni pamoja na kuweka wajibu wa Jihadi.
----------
India inafanya uhamisho wa Waislamu kwa ukatili na bila uamuzi wa mahakama
Habari ziliripoti mnamo 2025/6/30 kwamba India ilihamisha mamia ya Waislamu kwenda Bangladesh bila uamuzi wa mahakama, na India inadai kwamba waliohamishwa ni wahamiaji haramu, na inafuata sera ya kiholela ya dhuluma dhidi ya Waislamu kote India, ambao wanazidi watu milioni 200.
Wanaharakati nchini India walisema kwamba Waislamu, haswa katika eneo la mashariki mwa nchi, wameogopa sana. "Mamilioni wametupwa katika hofu hii ya kuwepo."
Shirika la habari la Ufaransa AFP liliripoti kutoka kwa Rahima Begum, mmoja wa wanawake Waislamu waliohamishwa, akielezea mateso yao: "Polisi walimzuilia kwa siku kadhaa mwishoni mwa Mei iliyopita kabla ya kumpeleka kwenye mpaka na Bangladesh, ingawa wanafamilia wake wote walizaliwa India na wameishi humo kwa vizazi.. Sijui kwa nini walinifanyia hivyo. Polisi wa India walimpeleka pamoja na watu 5, wote Waislamu, kwenye mpaka, na kuwalazimisha kushuka ndani ya bwawa gizani. Walionyesha kijiji cha mbali na kutuomba tukitambae kuelekea huko na wakasema tusithubutu kusimama au kutembea vinginevyo tutawapiga risasi," na akasema "Wakazi wa Kibengali ambao walitupata walitukabidhi kwa polisi wa mpaka wa Kibengali ambao askari wao walitupiga sana na kutuamuru turudi India."
Bangladesh ilisema kwamba India imesukuma zaidi ya watu 1,600 kuvuka mpaka wake tangu Mei, na vyombo vya habari vya India vilisema kwamba idadi hiyo inaweza kufikia 2,500. Haya yote yanatokea kwa sababu nchi za Kiislamu jirani kama Pakistan, Bangladesh na Afghanistan hazipingi sera za kiholela za India na kuishinikiza kuzizuia, na kisha kufanya kazi ya kuikomboa India kutoka kwa utawala wa Wahindu wenye chuki.
Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir ilitoa taarifa mnamo 2025/6/25 ikisema kwamba "Wakala wa Kitaifa wa Upelelezi wa India ulifanya uvamizi ulioratibiwa katika maeneo matatu katika jiji la Bhopal katika jimbo la Madhya Pradesh na maeneo mengine mawili huko Jawalor katika jimbo la Rajasthan ndani ya kile kinachoitwa kesi ya Hizb ut-Tahrir na kudai kwamba operesheni hii ililenga kukusanya ushahidi zaidi dhidi ya chama.. Ilikuwa imewakamata watu wawili kuhusiana na kesi hii.. Na serikali ya India ilitoa uamuzi wa kiholela wa kupiga marufuku Hizb ut-Tahrir mnamo 2024/10/10 kwa madai kwamba inafanya kazi ya kuanzisha Ukhalifa wa ulimwengu kupitia kile wanachoelezea kwa uwongo kama ugaidi na itikadi kali."

