Mtazamo wa Habari 2025/07/24
July 25, 2025

Mtazamo wa Habari 2025/07/24

Mtazamo wa Habari 2025/07/24

Shirika la Afya Duniani: Ukanda wa Gaza unakabiliwa na njaa kubwa

Jengo la matibabu la Al-Shifa katika Ukanda wa Gaza lilitangaza mnamo 2025/7/22 kwamba njaa ilisababisha vifo vya watoto 21 katika masaa 72 yaliyopita. Habari ziliripoti kuwa njaa itasababisha vifo vya watu wengi katika ukanda uliozingirwa na taasisi ya Kiyahudi na serikali ya Misri.

Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani, Ghebreyesus, alisisitiza mnamo 2025/7/24 kwamba "Ukanda wa Gaza unakabiliwa na njaa kubwa inayosababishwa hasa na vizuizi vya kuingia kwa misaada katika ukanda huo" na akasema: "Sioni maelezo mengine zaidi ya njaa kubwa, ambayo imetengenezwa na mwanadamu waziwazi... Kuzingirwa ndio sababu".

Zaidi ya mashirika 100 ya misaada yalitoa onyo la "kuenea kwa njaa huko Gaza licha ya tani nyingi za chakula, maji safi na vifaa vya matibabu kuwekwa kwenye mipaka na Misri na hairuhusiwi kuingizwa".

Jeshi la taasisi ya Kiyahudi lilitangaza mnamo 2025/7/23 kwamba lilishambulia malengo 120 huko Gaza, ambapo linadai kuwa "linashambulia seli za wapiganaji, majengo ya kijeshi, vichuguu vya mapigano, vifaa vya kulipuka na miundombinu mingine". Ikumbukwe kwamba iliharibu karibu 80% ya Gaza na kuua na kujeruhi mamia ya maelfu ya watu wake, wengi wao wakiwa wanawake, watoto na wanaume wasio na ulinzi wanaoishi katika hema au mitaani.

Hivyo ndivyo taasisi ya Kiyahudi inavyobobea katika vita vya mauaji ya kimbari ambayo imekuwa ikifanya huko Gaza kwa zaidi ya miezi 21, ilipoona kwamba Waislamu, ambao idadi yao ni karibu bilioni 2, hawajatoa majibu makubwa, hivyo majeshi yao hayakusonga na kuwafunza somo wasilolisahau na kusafisha Palestina kutokana na uchafu wao, na mifumo yao inashirikiana nao, ikiwaunga mkono ama kwa ukimya au kwa kuendelea kurejesha uhusiano wa kawaida na kufanya biashara nao, na kuwapa wanachohitaji kutoka kwa chakula, mafuta, gesi na malighafi kwa ajili ya kutengeneza silaha. Pia inapata msaada kamili kutoka Amerika na nchi nyingi za Ulaya na inawapa silaha na vifaa.

----------

Bunge la Knesset latoa uamuzi wa kuunganisha Ukingo wa Magharibi na taasisi ya Kiyahudi

Bunge la Knesset katika taasisi ya Kiyahudi lilitangaza mnamo 2025/7/23 uamuzi unaoitaka serikali yake kuunganisha Ukingo wa Magharibi na Bonde la Jordan na kufuta mpango wowote wa kuanzisha taifa la Palestina kutoka kwenye ajenda. Hii inakiuka Mkataba wa Oslo uliotiwa saini na Shirika la Ukombozi la Palestina, ambalo Mamlaka ya Palestina iliundwa kutoka kwake, ambayo ilitosheka na kulaani uamuzi huo, na kusema kwamba ni "uamuzi wa kibaguzi wa kikoloni na tamko la vita vya mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina". Haikutangaza kufuta makubaliano haya mabaya au kufuta uratibu wa kiusalama na taasisi ya Kiyahudi, kwani inailinda na kupigana na watu wa Palestina ikidhani kwamba Wayahudi watawazawadia kwa taifa, hata kama ni kwa jina tu.

Uamuzi wa Knesset ulisema kwamba hii ni "haki ya asili, ya kihistoria na ya kisheria". Ikumbukwe kwamba hilo ni dai la uongo, kwani Waislamu walipoifungua Palestina wakati wa ukhalifa wa Rashidun wa pili, Omar, Mungu amridhie, hakukuwa na Wayahudi huko Palestina. Viongozi wa Kikristo ambao walikabidhi funguo za Yerusalemu kwa khalifa kwa amani iliyofanywa nao, walisema kwamba Wayahudi ambao walifukuzwa kutoka humo wakati wa Warumi hawapaswi kuingia.

Ilikumbana na uvamizi kutoka kwa Wasaliti, hivyo Waislamu waliikomboa na kuisafisha kutokana na uchafu wao. Hadi Uingereza ilipoweza kuiteka katika Vita vya Kwanza vya Dunia, wakati wakala wao Mustafa Kemal, kamanda wa jeshi la Ottoman huko Palestina, alipowakabidhi. Iligawanya na kuanzisha taifa la Wayahudi kwa msaada wa Amerika, nchi za Magharibi na Urusi. Iliongeza Ukingo wa Magharibi kama sehemu ya Palestina kwenda Jordan, lakini Mfalme Hussein wa Jordan alifanya usaliti mkubwa alipoipeleka kwa taasisi ya Kiyahudi mnamo 1967 kulingana na mpango wa mabwana zake wa Kiingereza na Wayahudi.

-----------

Erdogan amsifu Ahmed Al-Shara kwa kutekeleza mpango wa kuwahamisha Waislamu kutoka Al-Suwaida

Rais wa Uturuki Erdogan aliusifu mnamo 2025/7/21 msimamo wa Ahmed Al-Shara katika kushughulikia matukio ya Al-Suwaida. Alidai uongo kwamba "Rais Ahmed Al-Shara alichukua msimamo thabiti kuhusu matukio ya hivi karibuni katika Al-Suwaida, kusini mwa nchi, na hakutoa makubaliano yoyote, na alichukua hatua nzuri sana kwa kufikia maelewano na Wadrusi huko Al-Suwaida. Israeli inafanya kazi ya kuzuia mradi wa utulivu nchini Syria"

Ikumbukwe kwamba Ahmed Al-Shara hakufyatua risasi yoyote dhidi ya taasisi ya Kiyahudi ambayo ilihalalisha Syria hadi ikapiga mazingira ya ikulu ya rais, Wizara ya Ulinzi na Urais wa Wafanyakazi na kupiga maeneo 160 mnamo 2025/7/16, na kupiga mamia ya maeneo ya kijeshi tangu Al-Shara alipoingia madarakani mnamo 2024/12/8. Taasisi ya Kiyahudi iliteka ardhi mpya ya Syria hadi ikafikia umbali wa kilomita 25 kutoka mji mkuu, Damascus.

Katika matukio ya Al-Suwaida, Ahmed Al-Shara alifanya makubaliano na taasisi ya Kiyahudi na Amerika kwa kuondoa vikosi vya usalama vya Syria na kuwaacha watu wa nchi hiyo kutoka Bedouin wazi kwa mawakala wa taasisi ya Kiyahudi kutoka kwa Wadrusi, ambao wanawaua, wanawachinja na kuwanyang'anya pesa zao. Na alifanya makubaliano ya kuwahamisha Bedouin kutoka mkoa wa Al-Suwaida ili iwe chini ya udhibiti wa mawakala hawa.

Hizi zote ni hatua hasi na janga kwa watu wa Syria na kengele ya hatari kwa mfumo wa Ahmed Al-Shara mwenyewe, ambaye anaonekana kufanya makubaliano haraka na kufanya kazi dhidi ya watu wake na nchi yake ili kulinda kiti chake.

Na Erdogan alimsifu, na kabla ya hapo Trump alimsifu baada ya kukutana naye huko Riyadh mnamo 2025/5/13 akisema "Ahmed Al-Shara ni mzuri, kijana anayevutia na mwenye nguvu", yeye ni mzuri kwake hadi atakapofanya makubaliano zaidi, ambapo alitangaza kuwa anakubali kurejesha uhusiano wa kawaida na taasisi ya Kiyahudi. Na Erdogan, msimamizi wa Amerika, anamshinikiza Ahmed Al-Shara kwa niaba ya Amerika badala ya maslahi yake ya kubaki madarakani na kufikia maslahi kadhaa madogo kwa Uturuki badala ya kutoa maslahi makubwa kwa Amerika kwa kuhakikisha ushawishi wake nchini Syria, Libya, Azerbaijan na kwingineko.

More from null

Habari za Abu Wadaha: Msimamo na hotuba ya kukwamisha njama ya kutenganisha Darfur na Port Sudan

أبو وضاحة شعار

14-11-2025

Habari za Abu Wadaha: Msimamo na hotuba ya kukwamisha njama ya kutenganisha Darfur na Port Sudan

Katika muktadha wa kampeni inayoendeshwa na Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Sudan kukwamisha njama ya Marekani ya kutenganisha Darfur, vijana wa Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Sudan waliandaa msimamo baada ya sala ya Ijumaa, 23 Jumada al-Ula 1447 Hijria, sawia na 2025/11/14 Miladia, mbele ya Msikiti wa Bashikh, katika mji wa Port Sudan, kitongoji cha Deim Medina.


Mwalimu Muhammad Jami' Abu Ayman - msaidizi wa msemaji rasmi wa Hizb ut-Tahrir katika Wilaya ya Sudan alitoa hotuba kwa umati wa waliohudhuria, akitoa wito wa kufanya kazi ili kukwamisha mpango unaoendelea wa kutenganisha Darfur, akisema: Kwamisheni mpango wa Marekani wa kutenganisha Darfur kama walivyotenganisha Kusini, ili kulinda umoja wa umma, na Uislamu umeharamisha kuutenganisha umma huu na kuuvunja, na umeifanya umoja wa umma na dola kuwa suala la hatima, ambalo hatua moja inachukuliwa dhidi yake, uhai au mauti, na pale suala hili lilipoanguka kutoka hadhi yake, makafiri waliweza, wakiongozwa na Marekani, na kwa msaada wa baadhi ya watoto wa Waislamu, kuuvunja nchi yetu, na kutenganisha Sudan Kusini ..Na baadhi yetu walinyamaza kimya juu ya dhambi hii kubwa, na walijishughulisha na upungufu na udhaifu, hivyo uhalifu huo ulipita! Na leo Marekani inarudi tena, kutekeleza mpango huo huo, na kwa mazingira hayo hayo, kuikata Darfur kutoka mwilini mwa Sudan, kwa kile walichokiita mpango wa mipaka ya damu. Wakitegemea wanamgambo wanaokalia Darfur nzima na wameanzisha dola yao bandia kwa kutangaza serikali sambamba katika mji wa Nyala; Je, mtairuhusu Marekani kufanya hivyo katika nchi yenu?!


Kisha alielekeza ujumbe kwa wanazuoni, na kwa watu wa Sudan, na kwa maafisa waaminifu katika vikosi vya jeshi kuchukua hatua ya kukomboa Darfur nzima na kuzuia kujitenga na kwamba fursa bado ipo ya kuzima mpango wa adui, na kukwamisha uovu huu, na kwamba tiba ya msingi ni kuanzisha Khilafah Rashidah kwa njia ya unabii, kwani ni hiyo pekee itakayo uhifadhi umma, na itatetea umoja wake, na itasimamisha sheria ya Mola wake.


Kisha alihitimisha hotuba yake akisema: Sisi ndugu zenu katika Hizb ut-Tahrir tumechagua kuwa pamoja na Mwenyezi Mungu Mtukufu, na tumsaidie Mungu, na tumuamini, na tutimize bishara ya Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ basi njooni pamoja nasi kwani Mwenyezi Mungu ni msaidizi wetu bila shaka. Amesema Mwenyezi Mungu: {Enyi mlio amini! Mkimnusuru Mwenyezi Mungu, naye atakunusuruni na atafanya imara nyayo zenu}.


Ofisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir katika Wilaya ya Sudan

Chanzo: Habari za Abu Wadaha

Rada: Babnusa Inaelekea Kufuata Mkondo wa Al-Fashir

الرادار شعار

13-11-2025

Rada: Babnusa Inaelekea Kufuata Mkondo wa Al-Fashir

Imeandikwa na Mhandisi/Hasbu Allah Al-Nur

Vikosi vya msaada wa haraka vilishambulia mji wa Babnusa siku ya Jumapili iliyopita, na kurudia shambulio lao asubuhi ya Jumanne.

Al-Fashir ilianguka kwa njia ya kusikitisha, na ilikuwa janga lililotikisa taifa la Sudan na kuumiza mioyo ya watu wake, ambapo damu safi ilimwagika, watoto walifiwa na baba, wanawake wakawa wajane, na mama zao waliomboleza.


Pamoja na majanga hayo yote, mazungumzo yanayoendelea Washington hayakuathirika hata kidogo, bali kinyume chake, mshauri wa Rais wa Marekani kuhusu masuala ya Afrika na Mashariki ya Kati, Musaad Bulus, aliliambia kituo cha Al Jazeera Mubasher tarehe 27/10/2025 kwamba kuanguka kwa Al-Fashir kunaimarisha mgawanyiko wa Sudan na kusaidia maendeleo ya mazungumzo!


Katika wakati huo muhimu, Wasudan wengi walitambua kwamba kinachotokea ni sura mpya tu ya mpango wa zamani ambao wazalendo wamekuwa wakionya dhidi yake, mpango wa kuitenga Darfur, ambao unataka kulazimishwa kwa njia ya vita, njaa na uharibifu.


Mzunguko wa kukataa kile kinachoitwa usitishaji wa mapigano wa miezi mitatu umeongezeka, na sauti za kupinga zimeongezeka, hasa baada ya habari kuvuja kuhusu uwezekano wa kuongezwa kwa miezi mingine tisa, ambayo kimsingi inamaanisha kuisomalia Sudan na kufanya mgawanyiko kuwa ukweli usioweza kuepukika kama ilivyo nchini Libya.


Na pale watengeneza vita waliposhindwa kunyamazisha sauti hizi kwa ushawishi, waliamua kuzinyamazisha kwa vitisho. Hivyo, dira ya mashambulizi ilielekezwa Babnusa, kuwa eneo la kurudia tukio la Al-Fashir; mzingiro mkali uliodumu kwa miaka miwili, na kuangusha ndege ya mizigo ili kuhalalisha kusimamishwa kwa usambazaji wa anga, na kulipua miji ya Sudan kwa wakati mmoja; Omdurman, Atbara, Damazin, Al-Abyad, Um Barmbita, Abu Jubaiha na Al-Abbasiya, kama ilivyotokea wakati wa shambulio la Al-Fashir.


Shambulio la Babnusa lilianza siku ya Jumapili, na liliongezeka tena asubuhi ya Jumanne, huku vikosi vya msaada wa haraka vikitumia mbinu na njia zilezile ambazo zilitumia huko Al-Fashir. Hadi wakati wa kuandika mistari hii, hakuna hatua yoyote halisi ya jeshi iliyorekodiwa kuwasaidia watu wa Babnusa, katika marudio ya kusikitisha ambayo karibu yanafanana na eneo la Al-Fashir kabla ya kuanguka kwake.


Ikiwa Babnusa itaanguka - Mungu apishie mbali - na sauti zinazopinga usitishaji wa mapigano hazitapungua, janga hilo litajirudia katika jiji lingine... Na kadhalika, hadi watu wa Sudan walazimishwe kukubali usitishaji wa mapigano wakiwa wanyonge.


Huo ndio mpango wa Amerika kwa Sudan kama unavyoonekana wazi; Kwa hivyo jihadharini, enyi watu wa Sudan, na fikirieni kile mnachofanya, kabla ya sura mpya yenye kichwa cha habari Mgawanyiko na Upotevu kuandikwa kwenye ramani ya nchi yenu.


Watu wa Babnusa wamehamishwa kabisa, ambao wanahesabu watu 177,000, kama ilivyoripotiwa katika kituo cha Al-Hadath tarehe 10/11/2025, na wanazurura bila mwelekeo.


Kupiga kelele, kulia, kupiga mashavu na kurarua mifuko ni tabia za wanawake, lakini hali hiyo inahitaji uanaume na ujasiri wa kukataa uovu, na kuchukua hatua dhidi ya mnyanyasaji, na kuinua neno la haki linalotaka kuachiliwa kwa minyororo ya majeshi ili kuchukua hatua ya kuokoa Babnusa, bali kurejesha Darfur yote.


Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ amesema: «Hakika watu wanapomuona dhalimu na hawamzuilii mkono wake, Mwenyezi Mungu yuko karibu kuwafunika kwa adhabu kutoka kwake.» Na akasema ﷺ: «Hakika watu wanapoona uovu na hawaubadilishi, Mwenyezi Mungu yuko karibu kuwafunika kwa adhabu.»


Na ni aina mbaya zaidi ya dhuluma, na miongoni mwa maovu makubwa, kuwakatisha tamaa watu wetu huko Babnusa kama watu wa Al-Fashir walivyokatishwa tamaa hapo awali.


Marekani ambayo inataka leo kuigawanya Sudan, ni ile ile iliyoigawanya kusini hapo awali, na inataka kuigawanya Iraq, Yemen, Syria na Libya, na kama watu wa Sham wanavyosema "na kamba iko kwenye mtungi", mpaka machafuko yataenea katika taifa lote la Kiislamu, na Mungu anatuita kwenye umoja.


Amesema Mwenyezi Mungu: ﴿NA HAKIKA HII DINI YENU NI DINI MOJA, NA MIMI NI MOLA WENU, BASI MCHENI﴾, na akasema ﷺ: «Akiapishwa Khalifa wawili, basi muueni yule mwingine miongoni mwao.» Na akasema: «Hakika yatakuwa majanga na majanga, na anayetaka kuutenganisha mambo ya umma huu na wao wote, mpigeni kwa upanga yeye yeyote anayekuwa.» Na pia alisema: «Anayekujieni na amri yenu nyote mkiwa juu ya mtu mmoja anayetaka kuigawanya fimbo yenu au kuitenganisha jamaa yenu, basi muueni.»


Je, nimefikisha? Ee Mwenyezi Mungu shuhudia, je, nimefikisha? Ee Mwenyezi Mungu shuhudia, je, nimefikisha? Ee Mwenyezi Mungu shuhudia.

Chanzo: Rada