Mtazamo wa Habari 2025/08/31
August 31, 2025

Mtazamo wa Habari 2025/08/31

 Mtazamo wa Habari 2025/08/31

Vance: Mazungumzo ya Witkov na Urusi yamepunguza tofauti kuhusu suluhu nchini Ukraine hadi masuala mawili muhimu

RT, 2025/8/29 - Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance alithibitisha kwamba juhudi za mjumbe Steve Witkov katika mazungumzo na Urusi zimepunguza tofauti kuhusu faili ya Ukraine na kubaki na masuala mawili tu ya dhamana za kiusalama na makubaliano ya kikanda.

Vance aliandika kwenye akaunti yake kwenye jukwaa la X: "Matokeo ya msingi ya mazungumzo ya Witkov yalikuwa kupunguza mzunguko wa masuala yaliyosalia yanayohusiana na vita kati ya Urusi na Ukraine, na kubaki na idadi ya faili zilizobainishwa wazi, ambazo ni dhamana za kiusalama na makubaliano ya kikanda."

Makamu wa Rais wa Marekani alimtaja Witkov kama "mwanachama muhimu sana" katika timu ya utawala wa Marekani, akijibu makala iliyochapishwa na gazeti la Politico, ambayo ilinukuu maafisa ambao hawakutajwa majina, wakitoa ukosoaji mkali kwa mjumbe huyo maalum, wakiamini kwamba hana uwezo wa kutosha kushiriki katika mchakato wa mazungumzo.

Vance alibainisha kuwa ripoti ya gazeti hilo inawakilisha ushahidi wa kupuuzwa kwa uandishi wa habari na inaonyesha uwepo wa chombo cha ushawishi wa kigeni kinacholenga kuudhuru utawala wa Marekani. Aliongeza: "Witkov hakumpotosha mtu yeyote kuhusu kile Warusi walimwambia au kile walionyesha kuwa tayari kukubali."

Makamu wa Rais wa Marekani alisisitiza kwamba "kufikia makubaliano ya amani nchini Ukraine bado hakujahitimishwa", lakini alieleza imani yake kwamba "ikiwa usitishaji mapigano utafikiwa, basi sifa ya hilo itakwenda kwa juhudi za Witkov na Rais Donald Trump."

Hii inaashiria ukali wa ukosoaji ambao Witkov anakabiliwa nao kwa sababu ya mazungumzo yake na Urusi na ukosefu wake wa uzoefu wa kidiplomasia na labda Warusi wanamshawishi kwa uwekezaji fulani wa kibinafsi.

------------

Washington yafuta visa za Rais wa Mamlaka ya Palestina na maafisa wengine kabla ya mkutano wa Baraza Kuu

Arab 48, 2025/8/30 - Marekani ilitangaza Ijumaa kwamba haitatoa visa kwa Rais wa Palestina, Mahmoud Abbas, na maafisa wengine 80 katika Mamlaka ya Palestina kuhudhuria Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mwezi ujao, ambapo Ufaransa na nchi nyingine kadhaa zinakusudia kuitambua nchi ya Palestina. Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani ilisema katika taarifa, "Waziri wa Mambo ya Nje Marco Rubio anakataa na kufuta visa za wanachama wa Shirika la Ukombozi la Palestina na Mamlaka ya Palestina kabla ya mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa." Iliongeza kuwa "Utawala wa Trump uko wazi: ni kwa manufaa yetu ya kiusalama wa kitaifa kuwawajibisha Shirika la Ukombozi la Palestina na Mamlaka ya Palestina kwa kushindwa kutimiza ahadi zao, na kudhoofisha matarajio ya amani."

Wizara ya Mambo ya Nje pia iliishutumu Palestina kwa kuzindua "vita vya kisheria" kwa kukimbilia Mahakama ya Kimataifa ya Jinai na Mahakama ya Kimataifa ya Haki kuishitaki huluki ya Kiyahudi. Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani ilisema Mamlaka ya Palestina inapaswa kusitisha "majaribio ya kukwepa mazungumzo kupitia kampeni za vita vya kisheria vya kimataifa" na "juhudi za kuhakikisha utambuzi wa upande mmoja wa nchi dhahania ya Palestina."

Chini ya makubaliano yaliyofikiwa kati ya Marekani na Umoja wa Mataifa kama nchi mwenyeji wa shirika la kimataifa huko New York, Washington haifai kukataa kutoa visa kwa maafisa wanaoelekea kwenye shirika hilo.

Hatua hii ya Marekani inakuja kuthibitisha mambo muhimu, ikiwa ni pamoja na kwamba Marekani na huluki ya Kiyahudi ni washirika wasiotenganishwa, na kwamba nchi ya Palestina, na kukimbilia Mahakama ya Kimataifa, yote hayaruhusiwi kwa mawakala na wanachotakiwa kufanya ni kujisalimisha kikamilifu, na kwamba Palestina haitatatuliwa tatizo lake na Umoja wa Mataifa au mfumo wa kimataifa, lakini majeshi yataikomboa na kuiosha kutoka kwa Wayahudi.

-----------

Umiraji wa kikabila huko Al-Khalil.. Mpango wa huluki ya Kiyahudi kujibu wino wa Magharibi kwenye karatasi ya Mamlaka ya Abbas

Euro News, 2025/8/29 - Vyombo vya habari katika huluki ya Kiyahudi viliripoti kwamba Waziri Mkuu Netanyahu anajiandaa kujadili mpango wa kuanzisha kile ambacho ripoti zingine zimeeleza kama "umiraji tofauti" katika mji wa Al-Khalil kusini mwa Ukingo wa Magharibi, na kuutenganisha na Mamlaka ya Ramallah.

Hatua hii inakuja kujibu tangazo la baadhi ya nchi za Magharibi, ikiwa ni pamoja na Ufaransa na Uingereza, nia yao ya kuitambua nchi ya Palestina wakati wa mikutano ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mnamo Septemba ijayo kama wino kwenye karatasi ambayo haibadilishi chochote katika hali halisi ya uvamizi.

Kulingana na ripoti, mpango huo unajumuisha uwezekano wa kuchukua nafasi ya makabila ya wenyeji na viongozi wa Mamlaka ya Palestina katika Al-Khalil, na kuanzisha huluki tofauti ambayo inatambua huluki ya Kiyahudi kama nchi ya Kiyahudi, na kujiunga na makubaliano ya Abraham ya kurejesha uhusiano wa kawaida na nchi za Kiarabu.

Lakini kituo hicho kilionyesha kuwa shirika la usalama la umma (Shabak) lilionyesha upinzani wake kwa mpango huo kutokana na huduma kubwa za kiusalama ambazo Mamlaka inatoa kwa huluki ya Kiyahudi, ikizingatia kwamba inachukua jukumu muhimu katika kupambana na shughuli za silaha, na kwamba utekelezaji wa mpango huo unaweza kudhoofisha fursa za kuanzisha nchi ya Palestina chini ya udhibiti wa Mamlaka.

Makabila ya Palestina hapo awali yalikuwa yamejitenga na pendekezo ambalo linategemea mawakala wa huluki ya Kiyahudi.

More from null

Habari za Abu Wadaha: Msimamo na hotuba ya kukwamisha njama ya kutenganisha Darfur na Port Sudan

أبو وضاحة شعار

14-11-2025

Habari za Abu Wadaha: Msimamo na hotuba ya kukwamisha njama ya kutenganisha Darfur na Port Sudan

Katika muktadha wa kampeni inayoendeshwa na Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Sudan kukwamisha njama ya Marekani ya kutenganisha Darfur, vijana wa Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Sudan waliandaa msimamo baada ya sala ya Ijumaa, 23 Jumada al-Ula 1447 Hijria, sawia na 2025/11/14 Miladia, mbele ya Msikiti wa Bashikh, katika mji wa Port Sudan, kitongoji cha Deim Medina.


Mwalimu Muhammad Jami' Abu Ayman - msaidizi wa msemaji rasmi wa Hizb ut-Tahrir katika Wilaya ya Sudan alitoa hotuba kwa umati wa waliohudhuria, akitoa wito wa kufanya kazi ili kukwamisha mpango unaoendelea wa kutenganisha Darfur, akisema: Kwamisheni mpango wa Marekani wa kutenganisha Darfur kama walivyotenganisha Kusini, ili kulinda umoja wa umma, na Uislamu umeharamisha kuutenganisha umma huu na kuuvunja, na umeifanya umoja wa umma na dola kuwa suala la hatima, ambalo hatua moja inachukuliwa dhidi yake, uhai au mauti, na pale suala hili lilipoanguka kutoka hadhi yake, makafiri waliweza, wakiongozwa na Marekani, na kwa msaada wa baadhi ya watoto wa Waislamu, kuuvunja nchi yetu, na kutenganisha Sudan Kusini ..Na baadhi yetu walinyamaza kimya juu ya dhambi hii kubwa, na walijishughulisha na upungufu na udhaifu, hivyo uhalifu huo ulipita! Na leo Marekani inarudi tena, kutekeleza mpango huo huo, na kwa mazingira hayo hayo, kuikata Darfur kutoka mwilini mwa Sudan, kwa kile walichokiita mpango wa mipaka ya damu. Wakitegemea wanamgambo wanaokalia Darfur nzima na wameanzisha dola yao bandia kwa kutangaza serikali sambamba katika mji wa Nyala; Je, mtairuhusu Marekani kufanya hivyo katika nchi yenu?!


Kisha alielekeza ujumbe kwa wanazuoni, na kwa watu wa Sudan, na kwa maafisa waaminifu katika vikosi vya jeshi kuchukua hatua ya kukomboa Darfur nzima na kuzuia kujitenga na kwamba fursa bado ipo ya kuzima mpango wa adui, na kukwamisha uovu huu, na kwamba tiba ya msingi ni kuanzisha Khilafah Rashidah kwa njia ya unabii, kwani ni hiyo pekee itakayo uhifadhi umma, na itatetea umoja wake, na itasimamisha sheria ya Mola wake.


Kisha alihitimisha hotuba yake akisema: Sisi ndugu zenu katika Hizb ut-Tahrir tumechagua kuwa pamoja na Mwenyezi Mungu Mtukufu, na tumsaidie Mungu, na tumuamini, na tutimize bishara ya Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ basi njooni pamoja nasi kwani Mwenyezi Mungu ni msaidizi wetu bila shaka. Amesema Mwenyezi Mungu: {Enyi mlio amini! Mkimnusuru Mwenyezi Mungu, naye atakunusuruni na atafanya imara nyayo zenu}.


Ofisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir katika Wilaya ya Sudan

Chanzo: Habari za Abu Wadaha

Rada: Babnusa Inaelekea Kufuata Mkondo wa Al-Fashir

الرادار شعار

13-11-2025

Rada: Babnusa Inaelekea Kufuata Mkondo wa Al-Fashir

Imeandikwa na Mhandisi/Hasbu Allah Al-Nur

Vikosi vya msaada wa haraka vilishambulia mji wa Babnusa siku ya Jumapili iliyopita, na kurudia shambulio lao asubuhi ya Jumanne.

Al-Fashir ilianguka kwa njia ya kusikitisha, na ilikuwa janga lililotikisa taifa la Sudan na kuumiza mioyo ya watu wake, ambapo damu safi ilimwagika, watoto walifiwa na baba, wanawake wakawa wajane, na mama zao waliomboleza.


Pamoja na majanga hayo yote, mazungumzo yanayoendelea Washington hayakuathirika hata kidogo, bali kinyume chake, mshauri wa Rais wa Marekani kuhusu masuala ya Afrika na Mashariki ya Kati, Musaad Bulus, aliliambia kituo cha Al Jazeera Mubasher tarehe 27/10/2025 kwamba kuanguka kwa Al-Fashir kunaimarisha mgawanyiko wa Sudan na kusaidia maendeleo ya mazungumzo!


Katika wakati huo muhimu, Wasudan wengi walitambua kwamba kinachotokea ni sura mpya tu ya mpango wa zamani ambao wazalendo wamekuwa wakionya dhidi yake, mpango wa kuitenga Darfur, ambao unataka kulazimishwa kwa njia ya vita, njaa na uharibifu.


Mzunguko wa kukataa kile kinachoitwa usitishaji wa mapigano wa miezi mitatu umeongezeka, na sauti za kupinga zimeongezeka, hasa baada ya habari kuvuja kuhusu uwezekano wa kuongezwa kwa miezi mingine tisa, ambayo kimsingi inamaanisha kuisomalia Sudan na kufanya mgawanyiko kuwa ukweli usioweza kuepukika kama ilivyo nchini Libya.


Na pale watengeneza vita waliposhindwa kunyamazisha sauti hizi kwa ushawishi, waliamua kuzinyamazisha kwa vitisho. Hivyo, dira ya mashambulizi ilielekezwa Babnusa, kuwa eneo la kurudia tukio la Al-Fashir; mzingiro mkali uliodumu kwa miaka miwili, na kuangusha ndege ya mizigo ili kuhalalisha kusimamishwa kwa usambazaji wa anga, na kulipua miji ya Sudan kwa wakati mmoja; Omdurman, Atbara, Damazin, Al-Abyad, Um Barmbita, Abu Jubaiha na Al-Abbasiya, kama ilivyotokea wakati wa shambulio la Al-Fashir.


Shambulio la Babnusa lilianza siku ya Jumapili, na liliongezeka tena asubuhi ya Jumanne, huku vikosi vya msaada wa haraka vikitumia mbinu na njia zilezile ambazo zilitumia huko Al-Fashir. Hadi wakati wa kuandika mistari hii, hakuna hatua yoyote halisi ya jeshi iliyorekodiwa kuwasaidia watu wa Babnusa, katika marudio ya kusikitisha ambayo karibu yanafanana na eneo la Al-Fashir kabla ya kuanguka kwake.


Ikiwa Babnusa itaanguka - Mungu apishie mbali - na sauti zinazopinga usitishaji wa mapigano hazitapungua, janga hilo litajirudia katika jiji lingine... Na kadhalika, hadi watu wa Sudan walazimishwe kukubali usitishaji wa mapigano wakiwa wanyonge.


Huo ndio mpango wa Amerika kwa Sudan kama unavyoonekana wazi; Kwa hivyo jihadharini, enyi watu wa Sudan, na fikirieni kile mnachofanya, kabla ya sura mpya yenye kichwa cha habari Mgawanyiko na Upotevu kuandikwa kwenye ramani ya nchi yenu.


Watu wa Babnusa wamehamishwa kabisa, ambao wanahesabu watu 177,000, kama ilivyoripotiwa katika kituo cha Al-Hadath tarehe 10/11/2025, na wanazurura bila mwelekeo.


Kupiga kelele, kulia, kupiga mashavu na kurarua mifuko ni tabia za wanawake, lakini hali hiyo inahitaji uanaume na ujasiri wa kukataa uovu, na kuchukua hatua dhidi ya mnyanyasaji, na kuinua neno la haki linalotaka kuachiliwa kwa minyororo ya majeshi ili kuchukua hatua ya kuokoa Babnusa, bali kurejesha Darfur yote.


Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ amesema: «Hakika watu wanapomuona dhalimu na hawamzuilii mkono wake, Mwenyezi Mungu yuko karibu kuwafunika kwa adhabu kutoka kwake.» Na akasema ﷺ: «Hakika watu wanapoona uovu na hawaubadilishi, Mwenyezi Mungu yuko karibu kuwafunika kwa adhabu.»


Na ni aina mbaya zaidi ya dhuluma, na miongoni mwa maovu makubwa, kuwakatisha tamaa watu wetu huko Babnusa kama watu wa Al-Fashir walivyokatishwa tamaa hapo awali.


Marekani ambayo inataka leo kuigawanya Sudan, ni ile ile iliyoigawanya kusini hapo awali, na inataka kuigawanya Iraq, Yemen, Syria na Libya, na kama watu wa Sham wanavyosema "na kamba iko kwenye mtungi", mpaka machafuko yataenea katika taifa lote la Kiislamu, na Mungu anatuita kwenye umoja.


Amesema Mwenyezi Mungu: ﴿NA HAKIKA HII DINI YENU NI DINI MOJA, NA MIMI NI MOLA WENU, BASI MCHENI﴾, na akasema ﷺ: «Akiapishwa Khalifa wawili, basi muueni yule mwingine miongoni mwao.» Na akasema: «Hakika yatakuwa majanga na majanga, na anayetaka kuutenganisha mambo ya umma huu na wao wote, mpigeni kwa upanga yeye yeyote anayekuwa.» Na pia alisema: «Anayekujieni na amri yenu nyote mkiwa juu ya mtu mmoja anayetaka kuigawanya fimbo yenu au kuitenganisha jamaa yenu, basi muueni.»


Je, nimefikisha? Ee Mwenyezi Mungu shuhudia, je, nimefikisha? Ee Mwenyezi Mungu shuhudia, je, nimefikisha? Ee Mwenyezi Mungu shuhudia.

Chanzo: Rada