Mtazamo wa Habari 2025/09/07
September 07, 2025

Mtazamo wa Habari 2025/09/07

Mtazamo wa Habari 2025/09/07

Ripoti: Google yatiliana saini mkataba wa dola milioni 45 na Netanyahu kuuza mauaji ya halaiki huko Gaza

Waarabu 48, 2025/9/6 - Kampuni ya Google ilifanya mkataba wa dola milioni 45 na ofisi ya waziri mkuu wa serikali ya Kiyahudi Netanyahu, kwa lengo la kukuza simulizi ya chombo cha Kiyahudi kuhusu vita dhidi ya Gaza na kukataa uhalifu uliofanywa dhidi ya Wapalestina, kama ilivyoripotiwa na tovuti ya Dropsite News, katika ripoti iliyochapishwa Jumatano iliyopita. Gazeti hilo liliripoti kuwa mkataba huo, uliotiwa saini mwishoni mwa Juni iliyopita, unaeleza Google kama "mhusika mkuu" katika kuunga mkono mkakati wa Netanyahu wa mahusiano ya umma.

Hii ilikuja sambamba na kuongezeka kwa shutuma za kimataifa dhidi ya serikali ya Kiyahudi kwa kulazimisha mzingiro kamili kwenye Ukanda wa Gaza na kufunga vivuko vyote vinavyoelekea Ukanda huo, kuzuia chakula, matibabu au misaada ya kibinadamu, ambayo ilisababisha Ukanda huo kuingia katika njaa licha ya malori ya misaada kuwa yamejaa kwenye mipaka yake. Hii ni pamoja na kifo cha kila siku ambacho Wayahudi wanalazimisha Gaza, ambayo inalia na haina msaidizi miongoni mwa Waislamu!

Maafisa wa chombo cha Kiyahudi wanajigamba kwamba hakuna njaa huko Gaza na serikali inaendelea kufanya kila aina ya mauaji bila kupata mtu wa kuizuia.

------------

Trump anashiriki vitisho vya chombo cha Kiyahudi kwa Gaza

CNN Kiarabu, 2025/9/6 - Rais wa Marekani Donald Trump, Ijumaa, alifichua kwamba utawala wake "unaendesha mazungumzo ya kina sana" na harakati ya Hamas kuhakikisha kuachiliwa kwa wafungwa Wayahudi waliosalia katika Ukanda wa Gaza.

Trump alionya, wakati wa matamshi kwa waandishi wa habari katika Ikulu ya White House, kwamba kushindwa kufikia makubaliano ya kuachiliwa mateka "kunaweza kusababisha hali ngumu," na akasema: "Hali itakuwa mbaya, hili ni maoni yangu, wanapaswa kuwaachilia." Hakutaja chochote kuhusu wafungwa Wapalestina wanaoteseka katika magereza ya Wayahudi kwa miongo kadhaa na wanakabiliwa na njaa na mateso, na hakutaja chochote kuhusu kusitisha vita dhidi ya Gaza, ambayo haijapita siku moja katika miaka miwili iliyopita bila idadi kubwa ya mashahidi na waliojeruhiwa, kana kwamba haoni chochote isipokuwa Wayahudi.

Aliwataka watu: "Lazima mkumbuke tarehe 7 Oktoba 2023," akimaanisha shambulio la Hamas dhidi ya serikali ya Kiyahudi, na akaendelea: "Kama mnavyojua, watu wanasahau tarehe 7 Oktoba, na si rahisi kuisahau, sivyo? Lakini watu wanasahau, au labda wanasahau tarehe 7 Oktoba 2023 kwa makusudi, kwa hivyo, kama mnavyojua, lazima mzingatie hilo kwa uzito mkubwa."

Anaona kwamba kuua chini ya Wayahudi 1200 ni uhalifu usiosameheka, wakati kuua makumi ya maelfu ya Wapalestina na kubomoa miji yao kwa miaka miwili na kwa msaada wa Amerika hakustahili kukumbukwa!

------------

Maduro atishia Amerika kuhamia kwenye mapambano ya silaha ikiwa Venezuela itashambuliwa

Shirika la Anadolu, 2025/9/6 - Rais wa Venezuela Nicolas Maduro, ametangaza kwamba nchi yake itaingia katika hatua ya mapambano ya silaha ikiwa itashambuliwa na Marekani. Hii ilikuja wakati wa mkutano wake na viongozi wa kijeshi katika mji mkuu Caracas kujadili tishio la Rais wa Marekani Donald Trump aliyeliambia Venezuela: "Tutadondosha ndege zenu." Maduro alisema: "Hivi sasa tuko katika hatua ya mapambano yasiyo ya silaha, ambayo ni hatua ya kisiasa, mawasiliano na taasisi. Lakini ikiwa Venezuela itashambuliwa, tutahamia kwenye hatua ya mapambano ya silaha." Aliongeza: "Sisi ni watengeneza amani, lakini pia sisi ni taifa la wapiganaji. Hakuna mtu anayeweza kututumikisha. Marekani lazima iache mipango yake ya kubadilisha mfumo nchini Venezuela kwa nguvu."

Hii inakuja huku kukiwa na vitisho vikubwa dhidi ya Venezuela kutoka kwa utawala wa Trump na hatua ya mwisho ya kuhamisha meli za kivita katika eneo hilo, na vitisho vinavyotolewa na Rais Trump, ambaye macho yake yako kwenye mafuta ya Venezuela, ambayo ina akiba kubwa ya mafuta duniani, na haiwezi kuuza mafuta kwa njia inayofaa kutokana na vikwazo vya Marekani.

Marekani inaona mafuta ya Venezuela kama akiba ya kimkakati kwake na inaweza wakati wowote kuikalia nchi hii na kuweka serikali ya vibaraka ndani yake kwa visingizio mbalimbali.

More from null

Habari za Abu Wadaha: Msimamo na hotuba ya kukwamisha njama ya kutenganisha Darfur na Port Sudan

أبو وضاحة شعار

14-11-2025

Habari za Abu Wadaha: Msimamo na hotuba ya kukwamisha njama ya kutenganisha Darfur na Port Sudan

Katika muktadha wa kampeni inayoendeshwa na Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Sudan kukwamisha njama ya Marekani ya kutenganisha Darfur, vijana wa Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Sudan waliandaa msimamo baada ya sala ya Ijumaa, 23 Jumada al-Ula 1447 Hijria, sawia na 2025/11/14 Miladia, mbele ya Msikiti wa Bashikh, katika mji wa Port Sudan, kitongoji cha Deim Medina.


Mwalimu Muhammad Jami' Abu Ayman - msaidizi wa msemaji rasmi wa Hizb ut-Tahrir katika Wilaya ya Sudan alitoa hotuba kwa umati wa waliohudhuria, akitoa wito wa kufanya kazi ili kukwamisha mpango unaoendelea wa kutenganisha Darfur, akisema: Kwamisheni mpango wa Marekani wa kutenganisha Darfur kama walivyotenganisha Kusini, ili kulinda umoja wa umma, na Uislamu umeharamisha kuutenganisha umma huu na kuuvunja, na umeifanya umoja wa umma na dola kuwa suala la hatima, ambalo hatua moja inachukuliwa dhidi yake, uhai au mauti, na pale suala hili lilipoanguka kutoka hadhi yake, makafiri waliweza, wakiongozwa na Marekani, na kwa msaada wa baadhi ya watoto wa Waislamu, kuuvunja nchi yetu, na kutenganisha Sudan Kusini ..Na baadhi yetu walinyamaza kimya juu ya dhambi hii kubwa, na walijishughulisha na upungufu na udhaifu, hivyo uhalifu huo ulipita! Na leo Marekani inarudi tena, kutekeleza mpango huo huo, na kwa mazingira hayo hayo, kuikata Darfur kutoka mwilini mwa Sudan, kwa kile walichokiita mpango wa mipaka ya damu. Wakitegemea wanamgambo wanaokalia Darfur nzima na wameanzisha dola yao bandia kwa kutangaza serikali sambamba katika mji wa Nyala; Je, mtairuhusu Marekani kufanya hivyo katika nchi yenu?!


Kisha alielekeza ujumbe kwa wanazuoni, na kwa watu wa Sudan, na kwa maafisa waaminifu katika vikosi vya jeshi kuchukua hatua ya kukomboa Darfur nzima na kuzuia kujitenga na kwamba fursa bado ipo ya kuzima mpango wa adui, na kukwamisha uovu huu, na kwamba tiba ya msingi ni kuanzisha Khilafah Rashidah kwa njia ya unabii, kwani ni hiyo pekee itakayo uhifadhi umma, na itatetea umoja wake, na itasimamisha sheria ya Mola wake.


Kisha alihitimisha hotuba yake akisema: Sisi ndugu zenu katika Hizb ut-Tahrir tumechagua kuwa pamoja na Mwenyezi Mungu Mtukufu, na tumsaidie Mungu, na tumuamini, na tutimize bishara ya Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ basi njooni pamoja nasi kwani Mwenyezi Mungu ni msaidizi wetu bila shaka. Amesema Mwenyezi Mungu: {Enyi mlio amini! Mkimnusuru Mwenyezi Mungu, naye atakunusuruni na atafanya imara nyayo zenu}.


Ofisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir katika Wilaya ya Sudan

Chanzo: Habari za Abu Wadaha

Rada: Babnusa Inaelekea Kufuata Mkondo wa Al-Fashir

الرادار شعار

13-11-2025

Rada: Babnusa Inaelekea Kufuata Mkondo wa Al-Fashir

Imeandikwa na Mhandisi/Hasbu Allah Al-Nur

Vikosi vya msaada wa haraka vilishambulia mji wa Babnusa siku ya Jumapili iliyopita, na kurudia shambulio lao asubuhi ya Jumanne.

Al-Fashir ilianguka kwa njia ya kusikitisha, na ilikuwa janga lililotikisa taifa la Sudan na kuumiza mioyo ya watu wake, ambapo damu safi ilimwagika, watoto walifiwa na baba, wanawake wakawa wajane, na mama zao waliomboleza.


Pamoja na majanga hayo yote, mazungumzo yanayoendelea Washington hayakuathirika hata kidogo, bali kinyume chake, mshauri wa Rais wa Marekani kuhusu masuala ya Afrika na Mashariki ya Kati, Musaad Bulus, aliliambia kituo cha Al Jazeera Mubasher tarehe 27/10/2025 kwamba kuanguka kwa Al-Fashir kunaimarisha mgawanyiko wa Sudan na kusaidia maendeleo ya mazungumzo!


Katika wakati huo muhimu, Wasudan wengi walitambua kwamba kinachotokea ni sura mpya tu ya mpango wa zamani ambao wazalendo wamekuwa wakionya dhidi yake, mpango wa kuitenga Darfur, ambao unataka kulazimishwa kwa njia ya vita, njaa na uharibifu.


Mzunguko wa kukataa kile kinachoitwa usitishaji wa mapigano wa miezi mitatu umeongezeka, na sauti za kupinga zimeongezeka, hasa baada ya habari kuvuja kuhusu uwezekano wa kuongezwa kwa miezi mingine tisa, ambayo kimsingi inamaanisha kuisomalia Sudan na kufanya mgawanyiko kuwa ukweli usioweza kuepukika kama ilivyo nchini Libya.


Na pale watengeneza vita waliposhindwa kunyamazisha sauti hizi kwa ushawishi, waliamua kuzinyamazisha kwa vitisho. Hivyo, dira ya mashambulizi ilielekezwa Babnusa, kuwa eneo la kurudia tukio la Al-Fashir; mzingiro mkali uliodumu kwa miaka miwili, na kuangusha ndege ya mizigo ili kuhalalisha kusimamishwa kwa usambazaji wa anga, na kulipua miji ya Sudan kwa wakati mmoja; Omdurman, Atbara, Damazin, Al-Abyad, Um Barmbita, Abu Jubaiha na Al-Abbasiya, kama ilivyotokea wakati wa shambulio la Al-Fashir.


Shambulio la Babnusa lilianza siku ya Jumapili, na liliongezeka tena asubuhi ya Jumanne, huku vikosi vya msaada wa haraka vikitumia mbinu na njia zilezile ambazo zilitumia huko Al-Fashir. Hadi wakati wa kuandika mistari hii, hakuna hatua yoyote halisi ya jeshi iliyorekodiwa kuwasaidia watu wa Babnusa, katika marudio ya kusikitisha ambayo karibu yanafanana na eneo la Al-Fashir kabla ya kuanguka kwake.


Ikiwa Babnusa itaanguka - Mungu apishie mbali - na sauti zinazopinga usitishaji wa mapigano hazitapungua, janga hilo litajirudia katika jiji lingine... Na kadhalika, hadi watu wa Sudan walazimishwe kukubali usitishaji wa mapigano wakiwa wanyonge.


Huo ndio mpango wa Amerika kwa Sudan kama unavyoonekana wazi; Kwa hivyo jihadharini, enyi watu wa Sudan, na fikirieni kile mnachofanya, kabla ya sura mpya yenye kichwa cha habari Mgawanyiko na Upotevu kuandikwa kwenye ramani ya nchi yenu.


Watu wa Babnusa wamehamishwa kabisa, ambao wanahesabu watu 177,000, kama ilivyoripotiwa katika kituo cha Al-Hadath tarehe 10/11/2025, na wanazurura bila mwelekeo.


Kupiga kelele, kulia, kupiga mashavu na kurarua mifuko ni tabia za wanawake, lakini hali hiyo inahitaji uanaume na ujasiri wa kukataa uovu, na kuchukua hatua dhidi ya mnyanyasaji, na kuinua neno la haki linalotaka kuachiliwa kwa minyororo ya majeshi ili kuchukua hatua ya kuokoa Babnusa, bali kurejesha Darfur yote.


Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ amesema: «Hakika watu wanapomuona dhalimu na hawamzuilii mkono wake, Mwenyezi Mungu yuko karibu kuwafunika kwa adhabu kutoka kwake.» Na akasema ﷺ: «Hakika watu wanapoona uovu na hawaubadilishi, Mwenyezi Mungu yuko karibu kuwafunika kwa adhabu.»


Na ni aina mbaya zaidi ya dhuluma, na miongoni mwa maovu makubwa, kuwakatisha tamaa watu wetu huko Babnusa kama watu wa Al-Fashir walivyokatishwa tamaa hapo awali.


Marekani ambayo inataka leo kuigawanya Sudan, ni ile ile iliyoigawanya kusini hapo awali, na inataka kuigawanya Iraq, Yemen, Syria na Libya, na kama watu wa Sham wanavyosema "na kamba iko kwenye mtungi", mpaka machafuko yataenea katika taifa lote la Kiislamu, na Mungu anatuita kwenye umoja.


Amesema Mwenyezi Mungu: ﴿NA HAKIKA HII DINI YENU NI DINI MOJA, NA MIMI NI MOLA WENU, BASI MCHENI﴾, na akasema ﷺ: «Akiapishwa Khalifa wawili, basi muueni yule mwingine miongoni mwao.» Na akasema: «Hakika yatakuwa majanga na majanga, na anayetaka kuutenganisha mambo ya umma huu na wao wote, mpigeni kwa upanga yeye yeyote anayekuwa.» Na pia alisema: «Anayekujieni na amri yenu nyote mkiwa juu ya mtu mmoja anayetaka kuigawanya fimbo yenu au kuitenganisha jamaa yenu, basi muueni.»


Je, nimefikisha? Ee Mwenyezi Mungu shuhudia, je, nimefikisha? Ee Mwenyezi Mungu shuhudia, je, nimefikisha? Ee Mwenyezi Mungu shuhudia.

Chanzo: Rada