Mtazamo wa Habari 2025/10/02
Mifumo iliyopo katika nchi za Kiislamu inathibitisha usaliti kwa kukaribisha mpango wa Trump
Mifumo iliyopo katika nchi za Waislamu imekaribisha mpango wa Trump wa kusimamisha vita huko Gaza. Qatar, kupitia msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje, Majid Al-Ansari, alitangaza mnamo 2025/9/30 kuunga mkono mpango huo na kuuelezea kama mfumo kamili wa kumaliza vita, na akasema kwamba Qatar na Misri zimewasilisha mpango huo kwa harakati ya Hamas na kwamba watakutana na Uturuki pamoja na ujumbe wa mazungumzo wa Hamas.
Mwanamfalme wa Saudia Mohammed bin Salman ameukubali, na vile vile Rais wa Uturuki Erdoğan, akisema "Ninaunga mkono juhudi za Rais wa Marekani Trump na uongozi wake unaolenga kukomesha umwagaji damu huko Gaza, na kufikia kusitisha mapigano". Jambo ambalo linafichua uwongo wake kwamba "huko Gaza na Palestina anawasaidia". Yote hayo yanafunua uovu wake, unyonge wake, na kujinyenyekeza kwake kwa Trump na uaminifu wake kwake kama watawala wengine wa Waislamu.
Inaonekana kwamba nchi hizi tatu, Qatar, Misri na Uturuki, zitafanya kazi ya kuishinikiza Hamas kukubali mpango huu unaojumuisha vipengele 21, na jambo muhimu zaidi lililotajwa ndani yake ni kuwakabidhi mateka wa Kiyahudi walio hai na waliokufa mara moja, na kuwapokonya silaha Hamas na mashirika mengine yenye silaha na kuharibu vifaa vya kutengeneza silaha, na kupeleka kikosi cha kimataifa. Trump alitangaza kwamba "ataanzisha Baraza la Amani chini ya uenyekiti wake na Tony Blair, Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza, na litajumuisha wanachama wengine kama chombo cha mpito cha kusimamia Gaza hadi Mamlaka ya Palestina itakapokamilisha programu yake ya mageuzi".
Trump ametishia harakati ya Hamas kwamba ikiwa haitakubali mpango huu, atampa chombo cha Kiyahudi ruhusa ya kufanya chochote kitakachotaka huko Gaza.
Mpango huo unasema kwamba chombo cha Kiyahudi kitaondoka polepole kutoka Ukanda bila ratiba. Hii inamaanisha kwamba inamsamehe kutoka kwa kuondoka mara moja na kwamba atacheza na suala la kujiondoa na kuchelewesha hadi atakapotimiza kile anachotaka.
Waziri Mkuu wa chombo cha Kiyahudi Netanyahu alikaribisha mpango huo kwa sababu yeye na Trump waliuandaa na kwa sababu unakidhi malengo yake. Alisema wakati wa ziara yake nchini Marekani na mkutano wake na Trump: "Hii ni ziara ya kihistoria nchini Marekani, na badala ya Hamas kutuzingira, tumegeuza mizani na kuizingira. Sasa ulimwengu mzima, ikiwa ni pamoja na ulimwengu wa Kiarabu na Kiislamu, unaishinikiza Hamas kukubali masharti ambayo tumeweka na Rais Trump. Nayo ni kuwaachilia huru mateka wetu wote wakiwa hai na wakiwa wamekufa huku vikosi vya jeshi la Israel vikiwa vimesalia katika eneo kubwa la Ukanda wa Gaza. Nani angeamini hili."
Kwa msingi wa haya, mpango huo unachukuliwa kuwa ushindi kwa chombo cha Kiyahudi, na unaikomboa kutokana na adhabu ya uhalifu wake kwa zaidi ya miaka miwili katika Ukanda wa Gaza, na unaiwezesha kudhibiti usalama wa Ukanda na inafanikisha kujisalimisha kwa wapiganaji kwa uvamizi wake na kuwanyang'anya silaha.
Pia inachukuliwa kuwa ushindi kwa Amerika kwani imehifadhi chombo chake cha Kiyahudi, kituo chake, na kuikomboa kutokana na uwajibikaji na adhabu. Ni aibu, fedheha, na lawama kwa watawala wa Waislamu na wale wanaowafuata na kuwaunga mkono, kwani wamekabidhi hatamu za mambo yao kwa Amerika na kukaribisha mipango yao mibaya na udhibiti wao juu ya nchi ya Kiislamu, na kwamba watawanyima silaha wapiganaji, na wasiwanyime silaha wavamizi wahalifu na kuadhibiwa vikali kwa kuangamiza uhai wao kutoka katika ardhi iliyobarikiwa ambayo ina Qibla ya kwanza na Haramu ya tatu, bali walinyamaza kimya juu ya uhalifu wake huko Gaza kwa zaidi ya miaka miwili, na kwamba nchi zinazoanzisha uhusiano wa kawaida na chombo cha Kiyahudi ziliendelea na uhusiano wao wa kidiplomasia na kibiashara, ambayo ni sawa na kuunga mkono kile ambacho chombo cha Kiyahudi kinafanya.
------------
Waziri wa Mambo ya Nje wa Syria kwa mfumo wa rais wake anathibitisha udhaifu na kuendelea na usaliti
Waziri wa Mambo ya Nje wa Syria, Asaad Al-Shaibani, alisema katika mahojiano na shirika la habari la CNN la Marekani mnamo 2025/9/28 "Kwamba mashambulizi ya Israel dhidi ya Syria baada ya kuanguka kwa Bashar al-Assad yalitushangaza... na kwamba Syria yenye nguvu na umoja itakuwa na manufaa kwa usalama wa kikanda, na hii itainufaisha Israeli, na kwamba Syria haileti tishio kwa mtu yeyote, ikiwa ni pamoja na Israeli, lakini sera hizi mpya za ushirikiano na amani zimepokelewa na vitisho na mashambulizi haya... na kwamba kuzungumzia uanzishwaji wa uhusiano wa kawaida na makubaliano ya Ibrahimu ni jambo gumu kidogo".
Waziri wa Mambo ya Nje wa Syria haachi kutoa matamko kama haya na kujihusisha katika mazungumzo na chombo cha Kiyahudi, na vivyo hivyo matamko ya rais wake Ahmed Al-Shara na matendo yake yanayohusiana na chombo cha Kiyahudi, kujisalimisha kwake, kujitolea kwa amani naye, na kujisalimisha kwa Amerika, kuonyesha kiwango cha akili iliyoanguka na nafsi duni iliyoanguka ambayo haijaonja utamu wa imani, wala heshima ya Muislamu ambaye hamwogopi ila Mungu, wala haitambui maana ya kumtegemea Mungu.
Hata waziri na rais wake wanaonyesha woga, kwa hivyo hawana matumizi ya lugha yoyote kali na hawataji neno lolote linalotishia chombo cha Kiyahudi na utayari wa kukabiliana nacho. Badala yake, yote ni kujisalimisha kwa kujisalimisha, kuonyesha unyenyekevu na kudharauliwa, na kujitolea kwa amani na chombo hiki cha uhalifu, ambacho hakiwapi amani na kitawanyonya kila wanaponyamaza na kujitoa na kuendelea na mashambulizi yao dhidi yao kwa sababu kama alivyosema Waziri Mkuu wa Kiyahudi Netanyahu kwamba mashambulizi ndiyo yanayofaulu mazungumzo. Hiyo ni kwamba yeye akiwa ameketi mezani anampiga adui na kumwambia akubali masharti yangu la sivyo nitakupiga na kweli anamchapa, na kila anapokubali masharti yake anamwekea masharti mengine na kadhalika ili asimwache na kinachofunika uchi wake.
-------------
Pakistan inatishia Afghanistan kwa kuzindua vita dhidi yake sambamba na vitisho vya Trump
Waziri wa Nchi wa Pakistan wa Mambo ya Nje, Talal Chaudhry, alitishia serikali ya Afghanistan katika mkutano na waandishi wa habari mnamo 2025/9/27 ikiwa mazungumzo yanayolenga kusitisha mashambulizi kwenye mpaka kati ya nchi hizo mbili yatashindikana, akisema: "Yeyote anayeelewa lugha ya risasi tutazungumza naye kwa lugha hiyo". Alidai kwamba "ugaidi ndio changamoto kubwa zaidi inayokabili Pakistan hivi sasa".
Gazeti la Dawn la Pakistan lilimnukuu akisema: "Asilimia 80 ya waliofanya mashambulizi ndani ya Pakistan wanatoka Afghanistan. Na Pakistan inachukua hatua kali za kuzuia uvukaji wa mpaka."
Vitisho vya Pakistan vinakuja kwa maelekezo ya Marekani ili kuongeza shinikizo kwa serikali ya Taliban ili iwe chini ya madai yake ya kikoloni ambapo rais wake hivi karibuni aliiomba serikali hii kukabidhi kambi ya Bagram kwake na alitoa vitisho dhidi yake. Hii inamaanisha kwamba Marekani itatumia utawala wa Pakistan unaoiunga mkono dhidi ya Afghanistan.
Kwa upande mwingine, waziri wa Pakistan alisahau changamoto kubwa zaidi inayokabili nchi yake kutoka India na uvamizi wake wa Kashmir na tishio lake la kutwaa maji ya mito ambayo walikubaliana kugawana kati yao mwaka 1960, ambapo India inafanya kazi ya kuanzisha miradi mikubwa ya kuzalisha umeme, ambayo ingeinyima Pakistan fursa ya kufaidika na maji haya, na pia juhudi za India za kuwahamisha mamilioni ya Waislamu kutoka nchini na kuwadhiki.
Waziri anamaanisha kwa ugaidi watu wa nchi hiyo Waislamu wanaodai kutekelezwa kwa Uislamu. Ambapo serikali ya Pakistan inapigana na kurejea kwa Uislamu madarakani, hata inachukulia makundi ya Kiislamu ya kisiasa kama vile Hizb ut-Tahrir ambayo haibebi silaha na inachukua njia ya Mtume ﷺ kama njia yake ya kuanzisha Khilafah, inachukulia kuwa makundi ya kigaidi ambapo ilipiga marufuku chama hicho mwaka 2003 kwa madai haya ya uongo na kumteka nyara msemaji rasmi wa chama hicho nchini Pakistan, Naveed Butt, na bado inamzuilia bila kesi tangu mwaka 2012, jambo linalothibitisha kiwango cha dhuluma na ukandamizaji unaofanywa na utawala wa Pakistan unaoiunga mkono Amerika.

