Mtazamo wa Habari 2025/10/02
October 02, 2025

Mtazamo wa Habari 2025/10/02

Mtazamo wa Habari 2025/10/02

Mifumo iliyopo katika nchi za Kiislamu inathibitisha usaliti kwa kukaribisha mpango wa Trump

Mifumo iliyopo katika nchi za Waislamu imekaribisha mpango wa Trump wa kusimamisha vita huko Gaza. Qatar, kupitia msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje, Majid Al-Ansari, alitangaza mnamo 2025/9/30 kuunga mkono mpango huo na kuuelezea kama mfumo kamili wa kumaliza vita, na akasema kwamba Qatar na Misri zimewasilisha mpango huo kwa harakati ya Hamas na kwamba watakutana na Uturuki pamoja na ujumbe wa mazungumzo wa Hamas.

Mwanamfalme wa Saudia Mohammed bin Salman ameukubali, na vile vile Rais wa Uturuki Erdoğan, akisema "Ninaunga mkono juhudi za Rais wa Marekani Trump na uongozi wake unaolenga kukomesha umwagaji damu huko Gaza, na kufikia kusitisha mapigano". Jambo ambalo linafichua uwongo wake kwamba "huko Gaza na Palestina anawasaidia". Yote hayo yanafunua uovu wake, unyonge wake, na kujinyenyekeza kwake kwa Trump na uaminifu wake kwake kama watawala wengine wa Waislamu.

Inaonekana kwamba nchi hizi tatu, Qatar, Misri na Uturuki, zitafanya kazi ya kuishinikiza Hamas kukubali mpango huu unaojumuisha vipengele 21, na jambo muhimu zaidi lililotajwa ndani yake ni kuwakabidhi mateka wa Kiyahudi walio hai na waliokufa mara moja, na kuwapokonya silaha Hamas na mashirika mengine yenye silaha na kuharibu vifaa vya kutengeneza silaha, na kupeleka kikosi cha kimataifa. Trump alitangaza kwamba "ataanzisha Baraza la Amani chini ya uenyekiti wake na Tony Blair, Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza, na litajumuisha wanachama wengine kama chombo cha mpito cha kusimamia Gaza hadi Mamlaka ya Palestina itakapokamilisha programu yake ya mageuzi".

Trump ametishia harakati ya Hamas kwamba ikiwa haitakubali mpango huu, atampa chombo cha Kiyahudi ruhusa ya kufanya chochote kitakachotaka huko Gaza.

Mpango huo unasema kwamba chombo cha Kiyahudi kitaondoka polepole kutoka Ukanda bila ratiba. Hii inamaanisha kwamba inamsamehe kutoka kwa kuondoka mara moja na kwamba atacheza na suala la kujiondoa na kuchelewesha hadi atakapotimiza kile anachotaka.

Waziri Mkuu wa chombo cha Kiyahudi Netanyahu alikaribisha mpango huo kwa sababu yeye na Trump waliuandaa na kwa sababu unakidhi malengo yake. Alisema wakati wa ziara yake nchini Marekani na mkutano wake na Trump: "Hii ni ziara ya kihistoria nchini Marekani, na badala ya Hamas kutuzingira, tumegeuza mizani na kuizingira. Sasa ulimwengu mzima, ikiwa ni pamoja na ulimwengu wa Kiarabu na Kiislamu, unaishinikiza Hamas kukubali masharti ambayo tumeweka na Rais Trump. Nayo ni kuwaachilia huru mateka wetu wote wakiwa hai na wakiwa wamekufa huku vikosi vya jeshi la Israel vikiwa vimesalia katika eneo kubwa la Ukanda wa Gaza. Nani angeamini hili."

Kwa msingi wa haya, mpango huo unachukuliwa kuwa ushindi kwa chombo cha Kiyahudi, na unaikomboa kutokana na adhabu ya uhalifu wake kwa zaidi ya miaka miwili katika Ukanda wa Gaza, na unaiwezesha kudhibiti usalama wa Ukanda na inafanikisha kujisalimisha kwa wapiganaji kwa uvamizi wake na kuwanyang'anya silaha.

Pia inachukuliwa kuwa ushindi kwa Amerika kwani imehifadhi chombo chake cha Kiyahudi, kituo chake, na kuikomboa kutokana na uwajibikaji na adhabu. Ni aibu, fedheha, na lawama kwa watawala wa Waislamu na wale wanaowafuata na kuwaunga mkono, kwani wamekabidhi hatamu za mambo yao kwa Amerika na kukaribisha mipango yao mibaya na udhibiti wao juu ya nchi ya Kiislamu, na kwamba watawanyima silaha wapiganaji, na wasiwanyime silaha wavamizi wahalifu na kuadhibiwa vikali kwa kuangamiza uhai wao kutoka katika ardhi iliyobarikiwa ambayo ina Qibla ya kwanza na Haramu ya tatu, bali walinyamaza kimya juu ya uhalifu wake huko Gaza kwa zaidi ya miaka miwili, na kwamba nchi zinazoanzisha uhusiano wa kawaida na chombo cha Kiyahudi ziliendelea na uhusiano wao wa kidiplomasia na kibiashara, ambayo ni sawa na kuunga mkono kile ambacho chombo cha Kiyahudi kinafanya.

------------

Waziri wa Mambo ya Nje wa Syria kwa mfumo wa rais wake anathibitisha udhaifu na kuendelea na usaliti

Waziri wa Mambo ya Nje wa Syria, Asaad Al-Shaibani, alisema katika mahojiano na shirika la habari la CNN la Marekani mnamo 2025/9/28 "Kwamba mashambulizi ya Israel dhidi ya Syria baada ya kuanguka kwa Bashar al-Assad yalitushangaza... na kwamba Syria yenye nguvu na umoja itakuwa na manufaa kwa usalama wa kikanda, na hii itainufaisha Israeli, na kwamba Syria haileti tishio kwa mtu yeyote, ikiwa ni pamoja na Israeli, lakini sera hizi mpya za ushirikiano na amani zimepokelewa na vitisho na mashambulizi haya... na kwamba kuzungumzia uanzishwaji wa uhusiano wa kawaida na makubaliano ya Ibrahimu ni jambo gumu kidogo".

Waziri wa Mambo ya Nje wa Syria haachi kutoa matamko kama haya na kujihusisha katika mazungumzo na chombo cha Kiyahudi, na vivyo hivyo matamko ya rais wake Ahmed Al-Shara na matendo yake yanayohusiana na chombo cha Kiyahudi, kujisalimisha kwake, kujitolea kwa amani naye, na kujisalimisha kwa Amerika, kuonyesha kiwango cha akili iliyoanguka na nafsi duni iliyoanguka ambayo haijaonja utamu wa imani, wala heshima ya Muislamu ambaye hamwogopi ila Mungu, wala haitambui maana ya kumtegemea Mungu.

Hata waziri na rais wake wanaonyesha woga, kwa hivyo hawana matumizi ya lugha yoyote kali na hawataji neno lolote linalotishia chombo cha Kiyahudi na utayari wa kukabiliana nacho. Badala yake, yote ni kujisalimisha kwa kujisalimisha, kuonyesha unyenyekevu na kudharauliwa, na kujitolea kwa amani na chombo hiki cha uhalifu, ambacho hakiwapi amani na kitawanyonya kila wanaponyamaza na kujitoa na kuendelea na mashambulizi yao dhidi yao kwa sababu kama alivyosema Waziri Mkuu wa Kiyahudi Netanyahu kwamba mashambulizi ndiyo yanayofaulu mazungumzo. Hiyo ni kwamba yeye akiwa ameketi mezani anampiga adui na kumwambia akubali masharti yangu la sivyo nitakupiga na kweli anamchapa, na kila anapokubali masharti yake anamwekea masharti mengine na kadhalika ili asimwache na kinachofunika uchi wake.

-------------

Pakistan inatishia Afghanistan kwa kuzindua vita dhidi yake sambamba na vitisho vya Trump

Waziri wa Nchi wa Pakistan wa Mambo ya Nje, Talal Chaudhry, alitishia serikali ya Afghanistan katika mkutano na waandishi wa habari mnamo 2025/9/27 ikiwa mazungumzo yanayolenga kusitisha mashambulizi kwenye mpaka kati ya nchi hizo mbili yatashindikana, akisema: "Yeyote anayeelewa lugha ya risasi tutazungumza naye kwa lugha hiyo". Alidai kwamba "ugaidi ndio changamoto kubwa zaidi inayokabili Pakistan hivi sasa".

Gazeti la Dawn la Pakistan lilimnukuu akisema: "Asilimia 80 ya waliofanya mashambulizi ndani ya Pakistan wanatoka Afghanistan. Na Pakistan inachukua hatua kali za kuzuia uvukaji wa mpaka."

Vitisho vya Pakistan vinakuja kwa maelekezo ya Marekani ili kuongeza shinikizo kwa serikali ya Taliban ili iwe chini ya madai yake ya kikoloni ambapo rais wake hivi karibuni aliiomba serikali hii kukabidhi kambi ya Bagram kwake na alitoa vitisho dhidi yake. Hii inamaanisha kwamba Marekani itatumia utawala wa Pakistan unaoiunga mkono dhidi ya Afghanistan.

Kwa upande mwingine, waziri wa Pakistan alisahau changamoto kubwa zaidi inayokabili nchi yake kutoka India na uvamizi wake wa Kashmir na tishio lake la kutwaa maji ya mito ambayo walikubaliana kugawana kati yao mwaka 1960, ambapo India inafanya kazi ya kuanzisha miradi mikubwa ya kuzalisha umeme, ambayo ingeinyima Pakistan fursa ya kufaidika na maji haya, na pia juhudi za India za kuwahamisha mamilioni ya Waislamu kutoka nchini na kuwadhiki.

Waziri anamaanisha kwa ugaidi watu wa nchi hiyo Waislamu wanaodai kutekelezwa kwa Uislamu. Ambapo serikali ya Pakistan inapigana na kurejea kwa Uislamu madarakani, hata inachukulia makundi ya Kiislamu ya kisiasa kama vile Hizb ut-Tahrir ambayo haibebi silaha na inachukua njia ya Mtume ﷺ kama njia yake ya kuanzisha Khilafah, inachukulia kuwa makundi ya kigaidi ambapo ilipiga marufuku chama hicho mwaka 2003 kwa madai haya ya uongo na kumteka nyara msemaji rasmi wa chama hicho nchini Pakistan, Naveed Butt, na bado inamzuilia bila kesi tangu mwaka 2012, jambo linalothibitisha kiwango cha dhuluma na ukandamizaji unaofanywa na utawala wa Pakistan unaoiunga mkono Amerika.

More from null

Habari za Abu Wadaha: Msimamo na hotuba ya kukwamisha njama ya kutenganisha Darfur na Port Sudan

أبو وضاحة شعار

14-11-2025

Habari za Abu Wadaha: Msimamo na hotuba ya kukwamisha njama ya kutenganisha Darfur na Port Sudan

Katika muktadha wa kampeni inayoendeshwa na Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Sudan kukwamisha njama ya Marekani ya kutenganisha Darfur, vijana wa Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Sudan waliandaa msimamo baada ya sala ya Ijumaa, 23 Jumada al-Ula 1447 Hijria, sawia na 2025/11/14 Miladia, mbele ya Msikiti wa Bashikh, katika mji wa Port Sudan, kitongoji cha Deim Medina.


Mwalimu Muhammad Jami' Abu Ayman - msaidizi wa msemaji rasmi wa Hizb ut-Tahrir katika Wilaya ya Sudan alitoa hotuba kwa umati wa waliohudhuria, akitoa wito wa kufanya kazi ili kukwamisha mpango unaoendelea wa kutenganisha Darfur, akisema: Kwamisheni mpango wa Marekani wa kutenganisha Darfur kama walivyotenganisha Kusini, ili kulinda umoja wa umma, na Uislamu umeharamisha kuutenganisha umma huu na kuuvunja, na umeifanya umoja wa umma na dola kuwa suala la hatima, ambalo hatua moja inachukuliwa dhidi yake, uhai au mauti, na pale suala hili lilipoanguka kutoka hadhi yake, makafiri waliweza, wakiongozwa na Marekani, na kwa msaada wa baadhi ya watoto wa Waislamu, kuuvunja nchi yetu, na kutenganisha Sudan Kusini ..Na baadhi yetu walinyamaza kimya juu ya dhambi hii kubwa, na walijishughulisha na upungufu na udhaifu, hivyo uhalifu huo ulipita! Na leo Marekani inarudi tena, kutekeleza mpango huo huo, na kwa mazingira hayo hayo, kuikata Darfur kutoka mwilini mwa Sudan, kwa kile walichokiita mpango wa mipaka ya damu. Wakitegemea wanamgambo wanaokalia Darfur nzima na wameanzisha dola yao bandia kwa kutangaza serikali sambamba katika mji wa Nyala; Je, mtairuhusu Marekani kufanya hivyo katika nchi yenu?!


Kisha alielekeza ujumbe kwa wanazuoni, na kwa watu wa Sudan, na kwa maafisa waaminifu katika vikosi vya jeshi kuchukua hatua ya kukomboa Darfur nzima na kuzuia kujitenga na kwamba fursa bado ipo ya kuzima mpango wa adui, na kukwamisha uovu huu, na kwamba tiba ya msingi ni kuanzisha Khilafah Rashidah kwa njia ya unabii, kwani ni hiyo pekee itakayo uhifadhi umma, na itatetea umoja wake, na itasimamisha sheria ya Mola wake.


Kisha alihitimisha hotuba yake akisema: Sisi ndugu zenu katika Hizb ut-Tahrir tumechagua kuwa pamoja na Mwenyezi Mungu Mtukufu, na tumsaidie Mungu, na tumuamini, na tutimize bishara ya Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ basi njooni pamoja nasi kwani Mwenyezi Mungu ni msaidizi wetu bila shaka. Amesema Mwenyezi Mungu: {Enyi mlio amini! Mkimnusuru Mwenyezi Mungu, naye atakunusuruni na atafanya imara nyayo zenu}.


Ofisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir katika Wilaya ya Sudan

Chanzo: Habari za Abu Wadaha

Rada: Babnusa Inaelekea Kufuata Mkondo wa Al-Fashir

الرادار شعار

13-11-2025

Rada: Babnusa Inaelekea Kufuata Mkondo wa Al-Fashir

Imeandikwa na Mhandisi/Hasbu Allah Al-Nur

Vikosi vya msaada wa haraka vilishambulia mji wa Babnusa siku ya Jumapili iliyopita, na kurudia shambulio lao asubuhi ya Jumanne.

Al-Fashir ilianguka kwa njia ya kusikitisha, na ilikuwa janga lililotikisa taifa la Sudan na kuumiza mioyo ya watu wake, ambapo damu safi ilimwagika, watoto walifiwa na baba, wanawake wakawa wajane, na mama zao waliomboleza.


Pamoja na majanga hayo yote, mazungumzo yanayoendelea Washington hayakuathirika hata kidogo, bali kinyume chake, mshauri wa Rais wa Marekani kuhusu masuala ya Afrika na Mashariki ya Kati, Musaad Bulus, aliliambia kituo cha Al Jazeera Mubasher tarehe 27/10/2025 kwamba kuanguka kwa Al-Fashir kunaimarisha mgawanyiko wa Sudan na kusaidia maendeleo ya mazungumzo!


Katika wakati huo muhimu, Wasudan wengi walitambua kwamba kinachotokea ni sura mpya tu ya mpango wa zamani ambao wazalendo wamekuwa wakionya dhidi yake, mpango wa kuitenga Darfur, ambao unataka kulazimishwa kwa njia ya vita, njaa na uharibifu.


Mzunguko wa kukataa kile kinachoitwa usitishaji wa mapigano wa miezi mitatu umeongezeka, na sauti za kupinga zimeongezeka, hasa baada ya habari kuvuja kuhusu uwezekano wa kuongezwa kwa miezi mingine tisa, ambayo kimsingi inamaanisha kuisomalia Sudan na kufanya mgawanyiko kuwa ukweli usioweza kuepukika kama ilivyo nchini Libya.


Na pale watengeneza vita waliposhindwa kunyamazisha sauti hizi kwa ushawishi, waliamua kuzinyamazisha kwa vitisho. Hivyo, dira ya mashambulizi ilielekezwa Babnusa, kuwa eneo la kurudia tukio la Al-Fashir; mzingiro mkali uliodumu kwa miaka miwili, na kuangusha ndege ya mizigo ili kuhalalisha kusimamishwa kwa usambazaji wa anga, na kulipua miji ya Sudan kwa wakati mmoja; Omdurman, Atbara, Damazin, Al-Abyad, Um Barmbita, Abu Jubaiha na Al-Abbasiya, kama ilivyotokea wakati wa shambulio la Al-Fashir.


Shambulio la Babnusa lilianza siku ya Jumapili, na liliongezeka tena asubuhi ya Jumanne, huku vikosi vya msaada wa haraka vikitumia mbinu na njia zilezile ambazo zilitumia huko Al-Fashir. Hadi wakati wa kuandika mistari hii, hakuna hatua yoyote halisi ya jeshi iliyorekodiwa kuwasaidia watu wa Babnusa, katika marudio ya kusikitisha ambayo karibu yanafanana na eneo la Al-Fashir kabla ya kuanguka kwake.


Ikiwa Babnusa itaanguka - Mungu apishie mbali - na sauti zinazopinga usitishaji wa mapigano hazitapungua, janga hilo litajirudia katika jiji lingine... Na kadhalika, hadi watu wa Sudan walazimishwe kukubali usitishaji wa mapigano wakiwa wanyonge.


Huo ndio mpango wa Amerika kwa Sudan kama unavyoonekana wazi; Kwa hivyo jihadharini, enyi watu wa Sudan, na fikirieni kile mnachofanya, kabla ya sura mpya yenye kichwa cha habari Mgawanyiko na Upotevu kuandikwa kwenye ramani ya nchi yenu.


Watu wa Babnusa wamehamishwa kabisa, ambao wanahesabu watu 177,000, kama ilivyoripotiwa katika kituo cha Al-Hadath tarehe 10/11/2025, na wanazurura bila mwelekeo.


Kupiga kelele, kulia, kupiga mashavu na kurarua mifuko ni tabia za wanawake, lakini hali hiyo inahitaji uanaume na ujasiri wa kukataa uovu, na kuchukua hatua dhidi ya mnyanyasaji, na kuinua neno la haki linalotaka kuachiliwa kwa minyororo ya majeshi ili kuchukua hatua ya kuokoa Babnusa, bali kurejesha Darfur yote.


Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ amesema: «Hakika watu wanapomuona dhalimu na hawamzuilii mkono wake, Mwenyezi Mungu yuko karibu kuwafunika kwa adhabu kutoka kwake.» Na akasema ﷺ: «Hakika watu wanapoona uovu na hawaubadilishi, Mwenyezi Mungu yuko karibu kuwafunika kwa adhabu.»


Na ni aina mbaya zaidi ya dhuluma, na miongoni mwa maovu makubwa, kuwakatisha tamaa watu wetu huko Babnusa kama watu wa Al-Fashir walivyokatishwa tamaa hapo awali.


Marekani ambayo inataka leo kuigawanya Sudan, ni ile ile iliyoigawanya kusini hapo awali, na inataka kuigawanya Iraq, Yemen, Syria na Libya, na kama watu wa Sham wanavyosema "na kamba iko kwenye mtungi", mpaka machafuko yataenea katika taifa lote la Kiislamu, na Mungu anatuita kwenye umoja.


Amesema Mwenyezi Mungu: ﴿NA HAKIKA HII DINI YENU NI DINI MOJA, NA MIMI NI MOLA WENU, BASI MCHENI﴾, na akasema ﷺ: «Akiapishwa Khalifa wawili, basi muueni yule mwingine miongoni mwao.» Na akasema: «Hakika yatakuwa majanga na majanga, na anayetaka kuutenganisha mambo ya umma huu na wao wote, mpigeni kwa upanga yeye yeyote anayekuwa.» Na pia alisema: «Anayekujieni na amri yenu nyote mkiwa juu ya mtu mmoja anayetaka kuigawanya fimbo yenu au kuitenganisha jamaa yenu, basi muueni.»


Je, nimefikisha? Ee Mwenyezi Mungu shuhudia, je, nimefikisha? Ee Mwenyezi Mungu shuhudia, je, nimefikisha? Ee Mwenyezi Mungu shuhudia.

Chanzo: Rada