Mtazamo wa Habari 22-06-2025
Erdogan anafunika uchi wake kwa makelele na kusema: Netanyahu na serikali yake ni kama Hitler
Al Jazeera Net, 2025/6/20 - Wakati Waislamu wanasubiri matendo badala ya maneno mbele ya shambulio la Wayahudi na Magharibi linaloendelea dhidi ya nchi za Kiislamu, rais wa Uturuki, ambaye anajulikana kwa makelele, anaendelea nayo na anashambulia chombo cha Kiyahudi kwa maneno tu! Alisema kuwa Waziri Mkuu wa chombo cha Kiyahudi Netanyahu na serikali yake wameandika majina yao pamoja na madikteta kama vile Hitler, akishutumu ukiukwaji wa chombo cha Kiyahudi huko Gaza na shambulio dhidi ya Iran, ambayo alionya kuwa inakaribia "hatua ya kutorejea".
Erdogan alisisitiza kuwa nchi za Kiislamu kwa sasa zinapitia kipindi kigumu, na akasema kuwa "vita, migogoro, machafuko na mawingu ya ukosefu wa utulivu yamefunika jiografia ya ustaarabu wetu. Tangu miaka miwili iliyopita, popote tunapoelekeza macho yetu, tunashtushwa na uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya ubinadamu."
Erdogan hakutaja chochote kuhusu matendo, kwani biashara ya Uturuki na chombo cha Kiyahudi inaendelea kupitia pande za tatu baada ya kutangaza kusitisha kwake baada ya miezi kadhaa ya vita dhidi ya Gaza, na kisha mafuta ya Azerbaijani yanaendelea kupita kutoka ardhi ya Uturuki hadi bandari ya Ceyhan ya Uturuki ambapo meli hubeba mafuta hadi chombo cha Kiyahudi kusafishwa na kusafirishwa na ndege zinazoshambulia Gaza, Lebanoni, Syria na Iran, kisha ndege za chombo cha Kiyahudi ambazo zinashambulia leo nchini Iran zimepenya anga ya Uturuki kutoka upande wa mashariki na Uturuki haikuziangusha, lakini ilisema kwamba iliingilia kati na kuzitaka kutoka nje ya anga yake na kushambulia Iran kutoka upande wa Iraqi.
Hali hii mbaya ya Erdogan imeunda tamaa na mshtuko kwa wafuasi wa mrengo wa wastani katika eneo hilo ambao walimtangaza kama "Sultan wa Umma" na msaidizi wa wanyonge, na hatujui ikiwa wamegundua ukweli wake leo au bado wanamwona kuwa mwema!
-----------
Putin: Ikiwa mfumo wa Kiev utatumia bomu chafu, jibu letu litakuwa kali sana na la maafa kwa mfumo mpya wa Nazi
RT, 2025/6/20 - Rais wa Urusi Vladimir Putin alisisitiza Ijumaa kwamba uamuzi wowote unaowezekana wa Ukraine kutumia bomu chafu dhidi ya Urusi utakuwa kosa la mwisho la serikali ya Kiev. Bomu chafu ni mlipuko ambao hutoa mionzi ya nyuklia na sio mlipuko wa nyuklia na ni rahisi kwa nchi kumiliki. Rais wa Urusi alisisitiza kuwa Urusi daima hujibu vitisho kwa usawa, kama inavyoelezwa katika mafundisho ya nyuklia ya nchi.
Akijibu swali kuhusu uwezekano wa Ukraine kuangusha bomu chafu kwenye ardhi ya Urusi, Putin alisema: "Katika mafundisho yetu ya nyuklia, pamoja na mantiki timamu na mazoezi ya matendo yetu, daima yanaonyesha kwamba tunajibu vitisho vyote tunavyokabiliana navyo kwa usawa. Daima tunajibu na kwa usawa daima." Aliendelea: "Kwa hiyo, jibu letu litakuwa kali sana, na uwezekano mkubwa litakuwa la maafa kwa mfumo mpya wa Nazi, na kwa bahati mbaya kwa Ukraine yenyewe. Natumaini haitafikia hatua hiyo kamwe."
Rais wa Urusi alieleza kuwa majeshi ya Ukraine yalifanya mfululizo wa uhalifu katika mkoa wa Kursk, ikiwa ni pamoja na dhidi ya raia.
----------
Marekani na mzozo wa kushiriki katika vita vya chombo cha Kiyahudi dhidi ya Iran, na naibu wa Trump anasema kwamba Marekani inazingatia maslahi yake kabla ya uamuzi kuhusu Iran
Al-Arabiya, 21/6/2025 - Wakati ulimwengu mzima ulikuwa ukisubiri uamuzi wa Rais wa Marekani Donald Trump kuhusu uwezekano wa kuingia katika vita vya chombo cha Kiyahudi dhidi ya Iran, baada ya kuipa Tehran muda wa wiki mbili kujibu pendekezo alilotoa kuhusu mpango wake wa nyuklia, naibu wake, JD Vance, alisisitiza kwamba rais atazingatia katika uamuzi wake maslahi ya kitaifa ya nchi.
Vance aliongeza katika mahojiano na Fox News kwamba Trump atatoa fursa kwa diplomasia, na wakati anaamua kwamba "diplomasia imemaliza madhumuni yake, na kwamba hatapata chochote kutoka kwa mazungumzo na upande wa Iran, basi atafanya uamuzi unaofaa." Aliongeza pia, "Wakati diplomasia imechoka, nadhani rais atafanya kile anachopaswa kufanya." Hata hivyo, alionya wakati huo huo kwamba wakati unakwisha.
Matamshi hayo yalitolewa baada ya rais wa Marekani kutangaza kwamba Iran ina muda wa wiki mbili "kiwango cha juu" kuepuka kukabiliwa na mashambulizi yanayoweza kutokea ya Marekani, akionyesha kwamba anaweza kufanya uamuzi kabla ya tarehe hii ya mwisho aliyoiweka. Hili ndilo lililotokea, kwani ndege za Marekani zilishambulia maeneo ya nyuklia ya Iran alfajiri ya Jumapili hii, 2025/06/22.
Kinacholeta changamoto zaidi kwa uamuzi wa Marekani ni kwamba Iran imetangaza kuwa haitafanya mazungumzo kabla ya kusitishwa kwa shambulio la chombo cha Kiyahudi dhidi yake, na pia nguzo za chama cha Republican zimegawanyika sana kuhusu ushiriki wa Marekani, na nguzo tatu kati ya hizi zimetoa wito wa kuacha chombo cha Kiyahudi kipigane vita vyake peke yake bila uingiliaji wa moja kwa moja wa Marekani na kwamba Marekani inatosha kushiriki kwa kulinda chombo hicho na sio kushambulia Iran.

