Taarifa kwa Vyombo vya Habari
Licha ya mfumo wa Jordan kuwaangusha watu wa Gaza na kukubali mpango wa Trump
Vyombo vyake vya usalama vinamkamata mmoja wa vijana wa Hizb ut-Tahrir
Mfumo wa Jordan bado unaendelea na kiburi chake cha dhambi na uadui, licha ya kuwaangusha watu wa Gaza, bali na kushirikiana na taasisi ya Kiyahudi katika vita vya mauaji ya halaiki iliyoanzisha dhidi ya Ukanda wa Gaza, na kuipatia sababu za uwezeshaji na kuishi, kisha haukusita kumbariki Trump mhalifu katika kumaliza suala la Palestina kwa kuhudhuria kile kinachoitwa (Baraza la Amani) ili kuwa shahidi wa uwongo juu ya mpango wa Trump wa kutawala nchi za Waislamu na kupoteza ardhi iliyobarikiwa ya Palestina.
Badala ya kuficha usaliti na udhaifu wake, vyombo vyake vya usalama tarehe 2025/10/8 vinamkamata kinyama Ustadh Khaled Al-Ashqar (Abu Al-Mu'taz), mmoja wa vijana wa Hizb ut-Tahrir, kutoka mlangoni mwa msikiti alipokuwa akitoka kusali (pamoja na shemeji yake, kaka wa mkewe, kwa wakati mmoja kutoka sehemu nyingine); kwa sababu tu ya kuzungumza na imamu wa msikiti hapo awali kuhusu hali ya Gaza na ulazima wa kuisaidia, na kile ambacho umma unapaswa kufanya kisheria ili kuisaidia, wakizuia neno la haki ambalo vijana wa Hizb ut-Tahrir wanatangaza kwa kutekeleza wajibu wa kuamrisha mema na kukataza maovu, wakati miji ya ulimwengu inachafuka juu ya uhalifu wa mauaji ya halaiki yanayofanywa na Wayahudi huko Gaza.
Kuongezeka kwa kampeni ya ukandamizaji wa mfumo dhidi ya neno la haki linalotangazwa wakati wa kufichua upungufu wake na ulinganifu wake na taasisi ya Kiyahudi na Amerika na kushindwa kwake kutekeleza wajibu wake wa kuwasaidia watu wa Gaza kwa kuendesha majeshi, kunaonyesha msimamo wake wa kuendelea na utegemezi wake kwa Magharibi kafiri mkoloni na dhuluma yake kwa watu wa Jordan na watu wa Palestina, na kuendelea kwake kuunga mkono maadui wa umma na kutegemea kwao, wakati neno la haki linamtikisa mbele ya dhuluma yake.
Kama mnavyomjua Hizb ut-Tahrir, haitachoka na haitazuiliwa na kukamatwa huku na ukandamizaji ambao mfumo unafanya dhidi ya vijana wake na kukandamiza vyombo vya habari unavyofanya, haitazuiliwa kueleza misimamo yake na lengo ambalo inafanya kazi kwa ajili yake kwa mapambano ya kiitikadi na mapambano ya kisiasa, ambayo ni kuanzisha upya maisha ya Kiislamu kwa kuanzisha Khilafah kwa njia ya Utume, ambayo itaendesha majeshi kukomesha taasisi ya Kiyahudi na mikono ya Amerika na mipango yake kwa eneo hilo na kurudisha kwa umma heshima na hadhi yake.
﴿Wale ambao watu waliwaambia: Hakika watu wamekusanyika kwa ajili yenu, basi waogopeni. Lakini hilo liliwazidisha Imani, wakasema: Mwenyezi Mungu anatutosha, naye ni Mbora wa kutegemewa﴾
Ofisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir
Katika Wilaya ya Jordan