Organization Logo

مصر - المكتب

ولاية مصر

Tel:

info@hizb.net

www.hizb.net

Mkataba wa Gesi na Taasisi ya Kiyahudi ni Ununuzi wa Utajiri Wetu Ulioibwa na Msaada kwa Adui Yetu Mtekaji
Press Release

Mkataba wa Gesi na Taasisi ya Kiyahudi ni Ununuzi wa Utajiri Wetu Ulioibwa na Msaada kwa Adui Yetu Mtekaji

August 08, 2025
Location

Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Mkataba wa Gesi na Taasisi ya Kiyahudi

Ununuzi wa Utajiri Wetu Ulioibwa na Msaada kwa Adui Yetu Mtekaji

Katika tukio jipya linaloonyesha kiwango cha uozo na utegemezi ambao utawala wa Misri umefikia, imetangazwa kutiwa saini kwa mkataba mkubwa na taasisi ya Kiyahudi kuagiza gesi asilia kutoka uwanja wa Leviathan katika ardhi za Palestina zilizochukuliwa kwa nguvu, kwa thamani ya karibu dola bilioni 35 za Kimarekani zinazoendelea hadi mwaka 2040, ambapo taasisi ya Kiyahudi inasafirisha takriban mita za ujazo bilioni 130 za gesi kwenda Misri, inayotumika kukidhi mahitaji ya soko la ndani na usafirishaji kupitia vituo vya ukwasi vya Misri. Mkataba huu umeuzwa kama "kuimarisha usalama wa nishati", wakati ukweli wake ni usaliti kwa taifa, kupoteza utajiri wake, uaminifu kwa adui yake na msaada kwa uchumi wake ulioathirika.

Katika mazingira ya migogoro ya kiuchumi na kisiasa inayokabili taasisi ya Kiyahudi, mkataba huu ni njia ya uokoaji kifedha na kimkakati kwake, kwani huizalishia mabilioni ya dola kila mwaka, huipa mshirika wa kuaminika katika usafirishaji, na kuiwezesha kujitangaza kama mchezaji mkuu katika soko la nishati la kikanda. Kwa upande mwingine, watu wa Misri wanapelekwa kwenye tegemezi zaidi, unyonge na umaskini, kwani mkataba huu hauwarejeshei chochote isipokuwa deni, kodi na kupanda kwa bei, wakati wanakabiliwa na uhaba wa umeme, gesi na gharama kubwa ya maisha.

Mtu anayeangalia mkataba huu haitaji uchunguzi mwingi ili kutambua utata hatari: Misri, nchi ya Kiislamu, inanunua gesi kutoka kwa taasisi iliyonyakua ardhi takatifu! Na la kushangaza zaidi, uwanja wa Leviathan na maeneo mengine hayakuwa na haki yoyote kwa Wayahudi, lakini walipewa ndani ya makubaliano batili ya kuweka mipaka ya baharini iliyoingiwa na utawala wa Misri mwaka 2018, ambayo ilikabidhi haki ya taifa katika maji yake ya kiuchumi, ili kuthibitisha ushirikiano wake kamili katika uhalifu.

Utawala wa Misri unaweka mkataba huu kama mafanikio ya kiuchumi, wakati kwa kweli ni unyenyekevu, kujisalimisha na uhusiano wa kiuchumi na adui mtekaji. Mkataba huu ni matokeo ya moja kwa moja ya makubaliano ya kuweka mipaka ya baharini ambayo utawala ulisaini na taasisi ya Kiyahudi, Cyprus na Ugiriki, ambayo ilisababisha kukabidhi maeneo makubwa ya maji yake ya kiuchumi kwa faida ya Wayahudi. Makubaliano haya ni batili kisheria, kwa sababu yanawakilisha kukabidhi ardhi, maji na utajiri kwa Wayahudi, na utambuzi wa wazi wa taasisi yao.

Mkataba huu wa gesi ni uhalifu mpya ulioongezwa kwenye rekodi ya utawala katika kupoteza ardhi takatifu na watu wake na ushirikiano wake na taasisi mtekaji.

Enyi askari wa Kinana: amkeni kabla historia haijaandika kwamba mlikuwa mashahidi wa uongo kwa usaliti mkubwa zaidi ambao taifa limejua katika enzi yake ya kisasa. Amkeni kwa kuwa Mungu atakuulizeni mmoja mmoja, kuhusu silaha ambayo haikuinuliwa, na kuhusu sauti ambayo haikusikika, na kuhusu taifa linalochinjwa mbele ya macho yenu, na hamkulisaidia. Na jueni kwamba saa ya hesabu inakuja, na kwamba Mungu hadanganywi na itikadi, wala hatishwa na majina. Kwa hivyo msiwe povu kama povu la mafuriko, wala walinzi wa upuuzi ambao huchoma dini yenu kutoka nyuma, kisha huinua bendera za uongo juu yenu... Tunamuomba Mungu awaongoze kwenye ukweli na awaruzuku kuufuata.

﴿Enyi mlio amini! Msiwafanye Mayahudi na Wakristo kuwa marafiki. Wao ni marafiki wao kwa wao. Na miongoni mwenu atakayewafanya marafiki, basi huyo ni katika wao

Ofisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilaya ya Misri

Official Statement

مصر - المكتب

ولاية مصر

مصر - المكتب

Media Contact

مصر - المكتب

Phone:

Email: info@hizb.net

مصر - المكتب

Tel: | info@hizb.net

www.hizb.net

Reference: PR-019884dd-1c60-73fc-8d10-634a2a42823a