Organization Logo

بنغلادش مكتب

ولاية بنغلادش

Tel: 8801798367640

Fax: Skype: htmedia.bd

contact@ht-bangladesh.info

Watu wa Bangladesh wanaopenda Uislamu Wamekataa Mkataba wa Julai, Uliojengwa Juu ya Ulaikini wa Magharibi na Demokrasia Yake ya Uongo, na Wanadai Mkataba wa Madina Uliojengwa Juu ya Itikadi Yake Safi ya Kiislamu
Press Release

Watu wa Bangladesh wanaopenda Uislamu Wamekataa Mkataba wa Julai, Uliojengwa Juu ya Ulaikini wa Magharibi na Demokrasia Yake ya Uongo, na Wanadai Mkataba wa Madina Uliojengwa Juu ya Itikadi Yake Safi ya Kiislamu

October 22, 2025
Location

Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Watu wa Bangladesh wanaopenda Uislamu Wamekataa Mkataba wa Julai, Uliojengwa Juu ya Ulaikini wa Magharibi na Demokrasia Yake ya Uongo, na Wanadai Mkataba wa Madina Uliojengwa Juu ya Itikadi Yake Safi ya Kiislamu

Mnamo tarehe 17 Oktoba 2025, wasomi wa nchi wanaotamani madaraka walisaini Mkataba wa Julai (suluhu ya kisiasa iliyoandikwa kwa kuzingatia imani na mfumo wa kidemokrasia bandia wa kikoloni wa makafiri wa Magharibi, haswa Amerika na Uingereza) na kutoa mfano mwingine mbaya wa uhaini kwa Uislamu na Waislamu, na uaminifu kwa Magharibi. Mfumo huu wa kibinadamu wa kisekula wa kibepari umeshindwa katika nchi zote ulimwenguni, na hili ni wazi kama jua la utosi: Mfumo huu dhalimu unalinda maslahi ya tabaka tawala na wachache wa mabepari na wakoloni wa Magharibi, na unawanyanyasa watu kwa ujumla. Na tunaona jinsi kizazi Z katika nchi nyingi kinavyoasi dhidi ya tabaka tawala la kibepari na kuwaondoa watawala mmoja baada ya mwingine.

Baada ya uasi wa Julai 2024, matabaka ya kisiasa yenye tamaa ya madaraka hayakujali madai ya watu ya kutawala kwa sheria za Kiislamu au hisia zao na imani zao za Kiislamu; badala yake, walijitenga nao na kuwalazimisha kwa nguvu chini ya uongozi wa Wamarekani na wakasaini "Mkataba wa Julai". Mwenyezi Mungu amesema: ﴿Je, wanataka hukumu ya kijahiliya? Na nani aliye bora zaidi katika hukumu kuliko Mwenyezi Mungu kwa watu wenye yakini?﴾ Mbali na kubadilisha hali ya watu, suluhu hii ya kisiasa itaboresha tu kuendelea kwa mfumo dhalimu wa sasa. Kama matokeo, watu hawana imani na maigizo haya ya kidemokrasia, wala hawahitaji mambo haya.

Enyi watu: Lazima mmeshuhudia jinsi Arab Spring ilivyoanzisha wimbi la kuwaondoa watawala dhalimu, lakini chini ya kivuli cha mageuzi ya dola na makubaliano mapya ya kisiasa yanayoongozwa na Magharibi, mfumo wa kisekula wa kibepari ulioshindwa uliendelea kuwepo. Kama matokeo, mateso ya watu katika nchi hizi hayajabadilika, lakini ushawishi wa Magharibi juu yao umeongezeka. Katika nchi yetu pia, mnaona jinsi Amerika na Uingereza zinavyojaribu kudhibiti siasa zetu, uchumi wetu, na jeshi letu kupitia vibaraka wao. Je, mkataba kama huo unawezaje kuwaunganisha watu wakati hata haujaweza kuunganisha matabaka haya ya kisiasa ya vibaraka?!

Enyi watu: Mnapaswa kujua jinsi Mkataba wa Madina, uliowekwa kwa msingi wa itikadi ya Kiislamu, ulivyoweka misingi ya dola ya Kiislamu huko Madina. Katika mazingira yake, watu walifurahia utawala wa haki bila kujali dini au kabila na waliishi maisha ya ustawi. Baadaye, Ukhalifa ulieneza utawala huu wa haki kote ulimwenguni. Ama mfumo wa kidemokrasia wa Magharibi, umeeneza unyonyaji, dhuluma na vita kote ulimwenguni kwa muda mfupi. Kwa hivyo, ili kurejesha heshima yetu na utukufu wetu, lazima tudai suluhu ya kisiasa inayotegemea Mkataba wa Madina na tuungane ili kuanzisha Ukhalifa.

Enyi maafisa waaminifu katika jeshi: Katika hatua hii ya kisiasa ya nchi, tunawakumbusha Ahadi ya Pili ya Aqaba, wakati watu wa nguvu na kinga, wakiongozwa na Saad bin Muadh t, walimpa ushindi Mtume ﷺ, ili kuanzisha dola ya Kiislamu. Ibn Ishaq alisema: Wakati Ansar walipokusanyika kwa ajili ya kumtii Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ huko Aqaba ya pili, Abbas bin Obada bin Nadla al-Ansari aliwaambia: Enyi watu wa Khazraj, je, mnajua mnamtii mtu huyu kwa ajili ya nini? Mnamtii kwa ajili ya kupigana na watu wekundu na weusi. Ikiwa mnaona kwamba mtakapokuwa mmeishiwa na mali yenu na viongozi wenu wameuawa, mtamsaliti, basi ni kuanzia sasa, kwa hakika hiyo ni aibu ya dunia na akhera. Na ikiwa mnaona kwamba mtamtimizia alichowataka nacho kwa uharibifu wa mali na kuuliwa kwa viongozi, basi mchukue, kwani kwa hakika hiyo ni bora ya dunia na akhera. Wakasema: Tunamchukua kwa hayo. Wakamwambia Mtume ﷺ: Tuna nini kwa hilo, ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, ikiwa tutatimiza? Akasema ﷺ: Pepo. Basi jiungeni na Hizb ut-Tahrir ili kusimamisha Ukhalifa kwa njia ya Utume na mpeni ushindi bila hofu ya Amerika, Uingereza na India. Na tunasisitiza kwenu kwamba Umma wa Kiislamu wote unangojea kusimamishwa kwa Ukhalifa. Zaidi ya hayo, ikiwa mshikamano wa vibaraka wa kigeni utaondoka, basi nguvu hizi kubwa hazitakuwa na njia ya kuingilia nchi yetu.

﴿Mwenyezi Mungu amewaahidi wale walioamini miongoni mwenu na wakatenda mema kwamba atawafanya makhalifa katika ardhi kama alivyowafanya makhalifa wale waliokuwa kabla yao...

Ofisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir

Katika Wilaya ya Bangladesh

Official Statement

بنغلادش مكتب

ولاية بنغلادش

بنغلادش مكتب

Media Contact

بنغلادش مكتب

Phone: 8801798367640

Fax: Skype: htmedia.bd

Email: contact@ht-bangladesh.info

بنغلادش مكتب

Tel: 8801798367640 | contact@ht-bangladesh.info

Fax: Skype: htmedia.bd

Reference: PR-0199fa13-ce10-71ac-8fcf-12afef0390a6