Habari kwa Vyombo vya Habari
Vijana wa Hizb ut-Tahrir katika Al-Abbasiya Taqli Watoa Wito wa Dhati kwa Waislamu
Kuhusu Kushindwa kwa Mpango wa Marekani wa Kuitenga Darfur
Katika muktadha wa kampeni inayoandaliwa na Hizb ut-Tahrir / Wilaya ya Sudan, kushindwa mpango wa kuivunja Sudan kwa kuitenga eneo la Darfur, na kwa kuzingatia kwamba umoja wa Umma ni suala la hatima, ambalo linachukuliwa hatua ya uhai au mauti, vijana wa Hizb ut-Tahrir katika Al-Abbasiya Taqli siku ya Ijumaa, 6 Rabi' al-Awwal 1447 Hijria, sawia na 2025/8/29 Miladia, baada ya swala ya Ijumaa, katika Msikiti wa Sheikh Yahya wa kuhifadhisha Qur'ani Tukufu, walitoa wito wa dhati kwa Waislamu wa makundi mbalimbali; kutoka kwa wanasiasa, wanahabari, wanachuoni, maafisa na askari, na wengineo, wakiwataka kutekeleza wajibu wao wa kisheria kuzuia kujitenga kwa Darfur.
Wito huo ulisomwa, mbele ya umati mkubwa wa waumini, na Ustadhi Abdul Rahim Abdullah, mwanachama wa Hizb ut-Tahrir, na amesimama upande wake wa kulia, na upande wake wa kushoto, baadhi ya vijana wa chama, wakiwa wamebeba mabango yanayotoa wito wa kukataa kujitenga, na mengine yanayotoa wito wa kushikamana na kamba ya Mwenyezi Mungu.
Waliohudhuria walishirikiana na wito huo kwa nguvu, huku wakimuomba Mwenyezi Mungu awalipe vijana wa chama thawabu zao na aubariki juhudi zao.
Ibrahim Othman (Abu Khalil)
Msemaji Rasmi wa Hizb ut-Tahrir
Katika Wilaya ya Sudan